Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,985
- 20,263
Waziri mkuu wa Kenya, Raila Odinga anaomba msaada wa Israel katika kuzuia mashambulio ya kundi la al Shabaab lenye mafungamano na kundi la kigaidi la al Qaeda. Katika taarifa ya serikali iliyotolewa leo Odinga amesema amemuomba rais wa Israel, Shimon Peres,msaada katika kujenga uwezo wa polisi ya Kenya katika kukabiliana na mashambulio ya wanamgambo wa al Shabaab. Vikosi vya Israel ni miongoni mwa vikosi bora kabisa ulimwenguni katika kukabiliana na vitisho vya kigaidi, lakini al Shabaab huenda wakaliona ombi la Kenya kama uchokozi.
Kenya ilituma mamia ya wanajeshi wake kusini mwa Somalia kuwasaka wapiganaji wa al Shabaab, inayowashutumu kwa kufanya mashambulio na utekaji nyara katika ardhi yake. Kwa kujibu hatua hiyo, kundi hilo limeapa kufanya mashambulio ya kigaidi* mjini Nairobi.
Kenya ilituma mamia ya wanajeshi wake kusini mwa Somalia kuwasaka wapiganaji wa al Shabaab, inayowashutumu kwa kufanya mashambulio na utekaji nyara katika ardhi yake. Kwa kujibu hatua hiyo, kundi hilo limeapa kufanya mashambulio ya kigaidi* mjini Nairobi.