samirnasri
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 1,388
- 213
Mtangazaji wa ATN kelvini moto amewazulia jambo katibu mkuu wa chadema dr. Slaa na mwenyekiti wake freeman mbowe kwa kudai kwamba wameenda libya kuhudhuria mkutano wa vyama vya demokrasia. Moto ameyasema hayo wakati akisoma uchambuzi wa magazeti katika television ya ATN leo asubuhi. Licha ya gazeti la nipashe kuandika kwa maandishi makubwa kwamba slaa, mbowe waenda liberia mtangazaji huyo wa ATN kwa kukosa umakini alisema wameenda libya na hata alipoisoma kwa kina alirudia kusema wameenda libya kuhudhuria mkutano wa vyama vya demokrasia. Mbali na kosa hilo kelvin motto aliendelea kukosea kutamka majina mbalimbali kama dr. Kingwalala badala ya dr kigwangala na mkanyanga badala ya mkajanga. Namshauri kelvin motto yeye kama mwandishi wa habari awe makini katika kazi zake vinginevyo atapotosha umma.