Keenja: Sasa tuivunje Dar es Salaam

Naona haya ni sehemu ya majibu(japo si rasmi) ambayo Kingobi kajibu kutokana na maoni haya ya Keenja


Jiji: Hatuhusiki na tatizo la foleni Dar es Salaam

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Jiji, Bakari Kingobi amesema mfumo wa ushirikiano kati ya halmashauri hiyo, halmashauri za manispaa na Wakala wa Barabara (Tanroads), unakanganya hata wawekezaji, huku akisisitiza kuwa ofisi yake haihusiki na tatizo la foleni Dar es Salaam.

Akizungumzia changamoto mbalimbali zinazolikabili jiji hilo pamoja na uwezo wake kimapato katika mahojiano maalumu na HABARI LEO, Kingobi alisema kwa sasa majukumu ya Jiji ni pamoja na kuzika watu wanaokufa na kukosa ndugu au wanaokufa kwa magonjwa ya mlipuko.

Alifafanua kuwa fedha inazokusanya jiji ambazo hazijafikia Sh bilioni tano tangu wameanza
kuwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, mbali na kuzika watu hao pia zinatumika katika
uzoaji wa takataka na mradi wa gesi ya taka unaoendeshwa eneo la Mtoni na Pugu na kulipa
posho za madiwani katika mabaraza ya madiwani ya jiji.

Akielezea mkanganyiko huo, Kingobi alisema ingawa barabara zote za Dar es Saalam ni za Jiji, lakini katika ujenzi wanaohusika ni Halmashauri za manispaa na Tanroads na wao ni
washiriki tu wa usimamizi.

Alitoa mfano kwamba kuna kipande cha barabara kutoka Bendera Tatu kuja mjini ambacho kuna mamlaka mbili zinazohusika na ujenzi wake ambazo ni Halmashauri ya Wilaya ya
Ilala na Tanroads.

Alielezea kisa cha wataalamu wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) waliokwenda ofisini kwake kuzungumzia ufadhili wa sehemu hiyo ya barabara, na
kushangazwa waliposhauriwa kuwa watalazimika kuzungumza na Tanroads na Halmashauri ya Wilaya Ilala kuhusu ujenzi wa mradi huo.

Mhasibu anayehusika na matumizi ya Jiji, Fadhili Izumbe, alitaja miradi mingine aliyosema fedha hizo za Jiji zimekuwa zikitumika, ambayo hata hivyo imeshakamilika au haipo chini
ya Jiji ukiwemo Mradi wa Mabasi yanayokwenda kasi Dar es Salaam (DART) ambao sasa upo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi).

Kwa mujibu wa Izumbe, mapato hayo pia yalitumika katika ujenzi wa shule ya Benjamin Mkapa ya Kariakoo, kuchangia hisa Benki ya Wananchi Dar es Salaam na ukarabati
wa taa za barabarani kwa mfano katika Barabara ya Nyerere (Pugu Road).

Takwimu ambazo gazeti hili linazo zinaonesha kuwa mwaka 2000 mapato ya Jiji yalikuwa Sh bilioni 7.2, lakini ilihusisha Jiji pamoja na manispaa zake tofauti na sasa kila Halmashauri
ina maeneo yake ya kukusanya mapato.

Takwimu zinaonesha kuwa ukusanyaji wa mapato katika mwaka wa fedha wa 2004/2005, Sh bilioni 3.516, 2005/06 Sh bilioni 3.760, 2006/07 Sh bilioni 3.771, 2007/08 Sh bilioni 4.014 na mwaka 2008/09 hadi Machi ilikusanywa Sh bilioni 2.720.

Mradi mkubwa unaoipatia jiji mapato Kituo cha Mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani cha Ubungo (UBT) ambacho kilichangia Sh milioni 964.095 katika mwaka wa fedha 2007/2008.

Hata hivyo, miradi mingi ambayo inapaswa kutumia mapato ya Jiji ambayo ilitajwa tayari, ilishakamilika kabla ya awamu hii ya uongozi.

Kwa mfano, Kingobi alisema yapo matumizi mengine lakini hayaonekani kwa wazi katika kulipa mishahara ya maofisa wasaidizi wasiolipwa kwa ruzuku ya Serikali Kuu, miradi yamaendeleo kama wa maboresho ya maeneo ambayo hayajapimwa (CIUP) na Jengo la Machinga Complex ambalo bado halijakabidhiwa kwa Jiji kutoka Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Jiji ambayo baadhi ya majukiumu yake yalirithiwa na Halmashauri ya Jiji, Charles Keenja aliliambia gazeti hili kuwa maendeleo ya jiji, yanahitaji
utekelezaji zaidi kuliko maneno matupu yenye mipango lukuki isiyotekelezeka.

Alisema hajui kiasi halisi cha mapato cha mwaka huu kwa halmashauri zote nne (Temeke, Ilala, Kinondoni na Jiji) lakini anaamini mapato yameongezeka zaidi kama Jiji pekee bila halmashauri hizo inakusanya Sh bilioni 4.

"Jiji lina shida kubwa ya maji ingawa serikali inajitahidi kulipatia ufumbuzi, asilimia zaidi ya 75 ya mapato ya nchi hii, yanatoka Dar es Salaam, lakini bado masuala ya miundombinu
ya barabara imekuwa hadithi, mimi niliahidiwa barabara za juu pale Ubungo mpaka nimechoka ni zaidi ya miaka mitatu sasa," alisema Keenja.

Source: Gazeti la Habari Leo
 
Mimi kwa maoni yangu whether Dar inavunjwa au haivunjwi lakini hili la kutengeneza drainage systems za jiji ili ziendeane na hali halisi ya umati wa watu uliofurika Dar halikwepeki hata kidogo. Hatuwezi kuendelea kuwa na jiji ambalo population yake imeongezeka kwa asilimia kubwa sana ukilinganisha na miaka ya 60 ambapo haikufika hata watu laki mbili na sasa kuna watu zaidi ya milioni 4.

Ni lazima katika bajeti inayokuja zitengwe kati ya shilingi bilioni 500 hadi bilioni 700 kwa miaka mitatu ili kuanza kuboresha drainage systems kuanzia katikati ya jiji na baadaye katika vitongoji vyake vyote na kazi hii ikabidhiwe kwa kampuni ya kimataifa yenye ujuzi na uzoefu wa kufanya kazi kubwa kama hii, hili kama halikufanyika itafikia wakati shughuli za jiji itabidi zisimame kabisa kila kutapokuwa na mvua kubwa na pia kunaweza kutokea upotevu mkubwa wa maisha ya wakazi wa jiji na mali zao.

Nazionea huruma hizo bilioni 500-700 kwani hata zikiwekwa zitaishia kudakwa na mijitu yenye uroho wa kuua na isiyo na uzalendo hata chembe.Tatizo lipo kwenye shina bado si matawi.
 
Wazo Langu

Ushauri wa Keenja unatekelezeka kwa sasa?

Imeandikwa na Lucy Lyatuu wa Habari Leo

NI kweli kabisa kama kuna kero kubwa inayowasumbua wakazi wa Dar es Salaam ni foleni kubwa ya magari pamoja na uchafu katika karibu kila kona.

Foleni hiyo huwalazimu watu kudamka mapema kuepuka foleni huku wakiwa hawana uhakika wa muda watakaofika kazini kusukuma gurudumu la maendeleo na kulijenga Taifa kwa ajili ya manufaa ya sasa na ya vizazi vijavyo.

Licha ya wakazi wengi wa jiji kujikuta kila mara wamechelewa kufika katika vituo vyao vya kazi ingawa walidamka alfajiri, kujazana kwao katika usafiri wa umma huwaadhiri baadhi yao ambao hujikuta wakianguka ovyo katika daladala kwa kukosa hewa safi.

Wasafiri wengi wamekuwa wakijadili mara kwa mara kuwa kama inawezekana barabara za vichochoroni ambazo zinapitika ziboreshwe zaidi ili kupunguza idadi kubwa ya magari yanayopita katika barabara kuu lakini mawazo na ushauri wao huishia katika majadiliano hayo wawapo ndani ya daladala.

Ni kweli kuwa foleni kubwa inawakwaza sana wasafiri kwa mfano, mtu anaweza kutoka Tabata kwenda Posta, ikiwa atatumia barabara ya Mandela na Uhuru, atalazimika kukaa katika daladala kwa saa zaidi ya mbili.

Yawezekana Mbunge wa Ubungo, Charles Keenja amewahi kukutana na maswali kutoka kwa wapiga kura wake kuhusu jinsi ya kuwaondolea kero hiyo, pindi alipogombea nafasi hiyo kwa msimu uliopita, lakini alishindwa kutoa jawabu ama aliona kama muda bado haujafika.

Lakini sasa ameamua kutoa ushauri huo, ikizingatiwa kuwa kero hiyo, imesababisha kila mmoja kuwaza kununua gari ili akwepe kusimama kwa muda mrefu katika daladala huku akiwa na hatari ya kuambukizwa magonjwa mengine yanayosambazwa kwa njia ya hewa.

Keenja ameshauri njia pekee ya kuepukana na kero za usafiri jijini ni kuondoa ujenzi holela unaosababisha barabara kuwa finyu na kufanya magari mengi kujaa barabarani huku askari wa usalama barabarani wakijikuta wakilazimika kuwajibika kupunguza foleni.

Ameshauri jiji la Dar es Salaam livunjwe hasa sehemu zilizojengwa holela kwa kuwa itakuwa msaada kwa kupunguza kero ya usafiri, lakini pia akashauri kabla ya yote ni vyema huduma za jamii zikaanza kusambazwa katika maeneo mbalimbali ili isimlazimu mtu kwenda umbali mrefu kufuatilia kitu kidogo ambacho angeweza kukipata umbali mfupi.

Ushauri wa Keenja unastahili kufanyiwa kazi na kutekelezwa lakini pia kwa upande mwingine inatia wasiwasi kama inawezekana sasa ikizingatiwa kuwa imekuwepo mipango mbalimbali yenye kuboresha usafiri wa jiji lakini utekelezaji wake hauonekani.

Nasema hivyo kwa kuwa zaidi ya miaka miwili iliyopita kuna mradi wa mabasi yaendayo kasi (DART) ambao katika mipango ya mradi huo, mwaka 2010 ndio wakazi wa Dar es Salaam wangeanza kunufaika na mabasi hayo lakini hadi sasa haijulikani walikofikia.
 
Hii nchi imejaa blabla tu. Dodoma Dodoma kisha kimya....
Flyovers flyovers kimya .......
DRT kimya...

Sana sana utasikia tunaunda kamati ya kuratibu uboreshaji wa jiji ambayo itaanza na study tour za kufa mtu na matumizi balaa wakati hali inazidi kuwa mbaya. Zimevunjwa nyumba moja (single storey) yakajengwa majengo ya ghorofa zaidi ya 10 na bado yanaota kama uyoga miundombinu iliangaliwa kabla ya kutoa vibali hivyo?

Hiyo response kweli ni ya kiongozi wa jiji kama ni yeye basi kazi tunayo. Unaulizwa uboreshaji wa jiji unatoa takwimu zako za kiaina. Hata wazo hana zaidi ya kusukuma mpira mara Tanroads, Municipal etc. Kuna kazi ya ziada. Uboreshaji wa jiji ni process kitendo cha kujua nini kitakaa wapi in say 5 years to come na ukasimamia iwe hivyo tayari ni way forward ambayo itazuia mtu kufanya development itakayoharibu mpango huo. Tatizo tunakimbilia kuvunja nyumba na kulipa fidia jamaa akipewa anatafuta maeneo yale yale unplanned. Tafuta eneo jenga appartments kidogo kidogo hamisha hao watu watakaoathirika kule full stop!

Viongozi wetu wanaonyesha wanahitajin kutawaliwa bado. Mawazo ni mafupi tu leo hadi uchaguzi ujao kisha ule mwingine nk.
 
....................kuhamisha ofisi za wizara; serikali, na balozi kwenda makao makuu ya nchi kule Dodoma; kutasaidia kupunguza Msongamano DSM. Serikali ianze kuivunja Dar kwa kutekeleza hilo kwa vitendo. Maana kuna watumishi wengi walikwisha lipwa fedha za uhamisho kwenda Dodoma lakini hadi leo bado wapo Dar katika ofisi zilezile walimohamishwa, na hela wametumia. Na sina shaka watastaafu wakiwa Dar. TUHAMIE DODOMA; DSM TUWAACHIE WENYE MJI WAO!!1

Aibu zaini ni wale miundombinu...wamejazana pale Holland house jengo la NHC wakati wan ofisi kule keko matokeo yake Samora yoote wanapaki wao hata pasipo napapingi...ile Idara ya maelezo nao si wahamie mwenge(TBC)maana nao wanaleta foleni....the list is everlong
 
....................kuhamisha ofisi za wizara; serikali, na balozi kwenda makao makuu ya nchi kule Dodoma; kutasaidia kupunguza Msongamano DSM. Serikali ianze kuivunja Dar kwa kutekeleza hilo kwa vitendo. Maana kuna watumishi wengi walikwisha lipwa fedha za uhamisho kwenda Dodoma lakini hadi leo bado wapo Dar katika ofisi zilezile walimohamishwa, na hela wametumia. Na sina shaka watastaafu wakiwa Dar. TUHAMIE DODOMA; DSM TUWAACHIE WENYE MJI WAO!!1

Kuonyesha mfano ofisi ya waziri kuu ilikuwa ya kwanza kuhama, lakini ikarudi haraka sana da res salaam mpaka leo imeng'ang'ania kama luba
 
acheni mambo yenu nyiee...yani tuhamie dodoma??...naona nyie nanyi mmekosa busara kama kibabu chenu kilichokuja na wazo la cda dodoma mwaka 1973...hivi huko dodoma hata lami hakuna haya ma-vogue na escallade zetu zitapita hewani??...na huko dodoma tukitaka kuogelea tuogelee bwawa gani?...bora hata morogoro mji kasoro bahari...HATUHAMI DAR MPAKA KIELEWEKE...kama kuhama hamisheni majengo ya
1- white house, 2- Liyumba house, 3- Wazungu house ili viza zote za kwenda uyala tukachukulie hapohapo dodoma...
 
Mawazo ya Keenja ni mazuri na ni muhimu kwa serikali kufuatilia ushauri wa namna hiyoo.. Tatizo la nchi yetu ni upangaji wa mamlaka na madaraka hauko sawia. Ikitokea kuwa na kiongozi mkuu (RAISI) anayeamini katika utendaji wa dhati na kusimamia kwa makinii utekelezaji wa mipango ya serikali huwa ufanisii unaonekana.

Mwalimu Nyerere alijitahidii kusimamiaa kwa dhati mipango ila alizidiwaa na vipaumbelee ndio maana kuna maeneo ambayoo hata yeye ailikuwa ndoto. Mfano kwa nia ya kuhamia dodoma yeye ndio pekee angewezaa kuonyeshaa njia kwa kutekelezaa kwa vitendo. angewezaa kuhamiaa dodoma na serikali yote ingefuataa.

hili la jiji kwa kweli maamuzii magumuu ni muhimu sana tena kwa haraka. msongamano tulionao ni wa kujitakia tuu. kwa mfano kuna haja gani ofisi zote muhimu za umma ziwe katikati ya jiji? Maeneo kibao nje ya jiji yanakua kwa kasi na bado yanwezaa kuwa na ofisi za umma zenye kutumiwa zaidii katika hudumaa.

barabara za pembezoni kama zile za kibamba-tegeta/bagamoyo, kimara-airport, kituoa cha mabasi, bagamoyo -msata, tanga,moshi arusha, ni sehemu tuu ya kupunguza msongamano katikati ya jiji.

halafu hili la mitaro hata meya na wasaidizii wakee hawana upeo nalo??????? la uchafuu ndo tabuu zaidii...
 
Angelifanya yeye alipokuwa Mkurugenzi wa jiji! sasa ametoka ndio anaanza kuwaambia wengine! Kwa ufupi ni gharama sana! Ukiweka na ubabaishaji wa Kibongo its completely imposible, can you imagine mandela raod imechukua karibia miaka miwili sasa kibarabara cha KM 10-15, kwa mtindo huu utavunja jiji kweli?

Nasikia hizo settellite towns sasa ngoja tusizubirie - Daraja na Kigamboni na Mji mpya kwa kigamboni hata dalili hakuna wanasubiri watu wajenge vibanda vyao. walitakiwa sasa hivi wawe wametoa stop order na watu wamelipwa ili wasiendeleze na wao bila kuchelewa waanze ujenzi wa mji. lakini tunavyoongea watu wanaporomosha migorofa bila kufuata ramani mpya.
Kifupi huyu mweshimiwa angesema hayo miaka 10 iliyopita ningemsifu. anyway ushauri mzuri ni challenges kwa waliopo madarakani, its true hiyo ndiyo njia pekee.

Tatizo sisi wabongo ni viwete wa kuchukua maamuzi magumu kwa wakati muafaka ukijumlisha na rushwa na siasa basi ni matatizo matupu mimi naungana na mdau kwamba kwa Bongo hii hili ni ndoto tena ya mchana.
 
Idea ni nzuri sana lakini swali kwake kwa hadhi ya ubunge aliyokuwa nayo kwa miaka kumi ameshindwaje kutekeleza hata sehemu ya hayo anayoyasema kwa jimbo la ubungo ili ma jimbo mengine yaige mfano au anataka apate ulaji wa kuwa meya baada ya kuona jimboni ushindani ni mkali ubunge kwa ubungo hapati tena
 
Tatizo la nchi yetu ni uongozi mbovu. Kiujumla hatuna viongozi tuna wafanya biashara na majungu. Kuna watu wakipewa nafasi huwa hawafanyi ajizi ila kwa sababu za masilahi binafsi na roho ya kutu wanafunikwa kwa manufaa ya kundi fulani. Mimi ninaamini tukiwa na kina MAGUFULI Kumi kwenye wizara tutaendelea.

Magufuli ni mtendaji mzuri sana ila anapigwa zengwe. Huyu bwana alikuwa pale miundombinu wakati wa Mkapa alifanya kazi nzuri sana, Muungwana alimuweka wizara ya ardhi alikuwa na vision nzuri sana aliisha sema kama mtu ana kiwanja ameshindwa kukiendeleza atanyang'anywa apewe mwenye uwezo. Kwa kuwa viongozi wengi serikalini wameshikilia viawanja kibao sehemu mbalimbali za jiji wakisubiri vipande bei wauze kwa mamilioni wakati walipewa kwa maelfu tu wakamuwekea fitina muungwana nae akamuhamishia wizara ya uvuvi.

Tatizo letu ni kukosa viongozi basi ila kitu kinawezekana. Kuwapatia watu kama kina Magufuli sehemu muhimu wakafanya kazi nzuri haimaanishi watakuwa tishio kwa wenye uroho wa urais 2015 waliokaribu na muungwana. Tufanye mambo kwa kulisaidia taifa siyo kuwalinda watu fulani. Tanzania yenye maendeleo na utendaji mzuri inawezekana mradi tu watendaji wazuri wapewe nafasi ya ku-impliment idea zao bila kuingiliwa na mtu kwa sababu zozote zile
 
acheni mambo yenu nyiee...yani tuhamie dodoma??...naona nyie nanyi mmekosa busara kama kibabu chenu kilichokuja na wazo la cda dodoma mwaka 1973...hivi huko dodoma hata lami hakuna haya ma-vogue na escallade zetu zitapita hewani??...na huko dodoma tukitaka kuogelea tuogelee bwawa gani?...bora hata morogoro mji kasoro bahari...HATUHAMI DAR MPAKA KIELEWEKE...kama kuhama hamisheni majengo ya
1- white house, 2- Liyumba house, 3- Wazungu house ili viza zote za kwenda uyala tukachukulie hapohapo dodoma...

White House ipo chamwino classic state house, Liyumba house inaweza kumushroom, " wakiamua", wazungu house na wazungu plots zipo zimetengwa kwa ajili ya diplomats. Vogue na escallade sidhani kama zinahitaji lami kwa uimara wake na confort bila lami twende tu. Pamoja na barabara mbaya lakini inachukua at most 20 minutes kutoka home mpaka ofisini na dakika chache toka ofisi moja kwenda nyingine.

Lami inanisaidia nini wakati natumia masaa matatu kutembea kilomita 20, haileti maana kabisa.
 
Naona haya ni sehemu ya majibu(japo si rasmi) ambayo Kingobi kajibu kutokana na maoni haya ya Keenja


Jiji: Hatuhusiki na tatizo la foleni Dar es Salaam

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Jiji, Bakari Kingobi amesema mfumo wa ushirikiano kati ya halmashauri hiyo, halmashauri za manispaa na Wakala wa Barabara (Tanroads), unakanganya hata wawekezaji, huku akisisitiza kuwa ofisi yake haihusiki na tatizo la foleni Dar es Salaam.

Akizungumzia changamoto mbalimbali zinazolikabili jiji hilo pamoja na uwezo wake kimapato katika mahojiano maalumu na HABARI LEO, Kingobi alisema kwa sasa majukumu ya Jiji ni pamoja na kuzika watu wanaokufa na kukosa ndugu au wanaokufa kwa magonjwa ya mlipuko.

Alifafanua kuwa fedha inazokusanya jiji ambazo hazijafikia Sh bilioni tano tangu wameanza
kuwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, mbali na kuzika watu hao pia zinatumika katika
uzoaji wa takataka na mradi wa gesi ya taka unaoendeshwa eneo la Mtoni na Pugu na kulipa
posho za madiwani katika mabaraza ya madiwani ya jiji.


Akielezea mkanganyiko huo, Kingobi alisema ingawa barabara zote za Dar es Saalam ni za Jiji, lakini katika ujenzi wanaohusika ni Halmashauri za manispaa na Tanroads na wao ni
washiriki tu wa usimamizi.


Alitoa mfano kwamba kuna kipande cha barabara kutoka Bendera Tatu kuja mjini ambacho kuna mamlaka mbili zinazohusika na ujenzi wake ambazo ni Halmashauri ya Wilaya ya
Ilala na Tanroads.

Alielezea kisa cha wataalamu wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) waliokwenda ofisini kwake kuzungumzia ufadhili wa sehemu hiyo ya barabara, na
kushangazwa waliposhauriwa kuwa watalazimika kuzungumza na Tanroads na Halmashauri ya Wilaya Ilala kuhusu ujenzi wa mradi huo.

Mhasibu anayehusika na matumizi ya Jiji, Fadhili Izumbe, alitaja miradi mingine aliyosema fedha hizo za Jiji zimekuwa zikitumika, ambayo hata hivyo imeshakamilika au haipo chini
ya Jiji ukiwemo Mradi wa Mabasi yanayokwenda kasi Dar es Salaam (DART)
ambao sasa upo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi).

Kwa mujibu wa Izumbe, mapato hayo pia yalitumika katika ujenzi wa shule ya Benjamin Mkapa ya Kariakoo, kuchangia hisa Benki ya Wananchi Dar es Salaam na ukarabati
wa taa za barabarani kwa mfano katika Barabara ya Nyerere (Pugu Road).

Takwimu ambazo gazeti hili linazo zinaonesha kuwa mwaka 2000 mapato ya Jiji yalikuwa Sh bilioni 7.2, lakini ilihusisha Jiji pamoja na manispaa zake tofauti na sasa kila Halmashauri
ina maeneo yake ya kukusanya mapato.

Takwimu zinaonesha kuwa ukusanyaji wa mapato katika mwaka wa fedha wa 2004/2005, Sh bilioni 3.516, 2005/06 Sh bilioni 3.760, 2006/07 Sh bilioni 3.771, 2007/08 Sh bilioni 4.014 na mwaka 2008/09 hadi Machi ilikusanywa Sh bilioni 2.720.

Mradi mkubwa unaoipatia jiji mapato Kituo cha Mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani cha Ubungo (UBT) ambacho kilichangia Sh milioni 964.095 katika mwaka wa fedha 2007/2008.

Hata hivyo, miradi mingi ambayo inapaswa kutumia mapato ya Jiji ambayo ilitajwa tayari, ilishakamilika kabla ya awamu hii ya uongozi.

Kwa mfano, Kingobi alisema yapo matumizi mengine lakini hayaonekani kwa wazi katika kulipa mishahara ya maofisa wasaidizi wasiolipwa kwa ruzuku ya Serikali Kuu, miradi yamaendeleo kama wa maboresho ya maeneo ambayo hayajapimwa (CIUP) na Jengo la Machinga Complex ambalo bado halijakabidhiwa kwa Jiji kutoka Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Jiji ambayo baadhi ya majukiumu yake yalirithiwa na Halmashauri ya Jiji, Charles Keenja aliliambia gazeti hili kuwa maendeleo ya jiji, yanahitaji
utekelezaji zaidi kuliko maneno matupu yenye mipango lukuki isiyotekelezeka.

Alisema hajui kiasi halisi cha mapato cha mwaka huu kwa halmashauri zote nne (Temeke, Ilala, Kinondoni na Jiji) lakini anaamini mapato yameongezeka zaidi kama Jiji pekee bila halmashauri hizo inakusanya Sh bilioni 4.

"Jiji lina shida kubwa ya maji ingawa serikali inajitahidi kulipatia ufumbuzi, asilimia zaidi ya 75 ya mapato ya nchi hii, yanatoka Dar es Salaam, lakini bado masuala ya miundombinu
ya barabara imekuwa hadithi, mimi niliahidiwa barabara za juu pale Ubungo mpaka nimechoka ni zaidi ya miaka mitatu sasa," alisema Keenja.

Source: Gazeti la Habari Leo

Kichwa kinauma kwa kweli, aliyewaajiri hao watu nadhani akisoma atawagombeza sana. Anatakiwa yeye ndio afukuzwe kazi yaani mkurugwnzi unaanza kuelezea changamoto kubwa la jiji ni kuzika watu wasio na ndugu ni kuonyesha ni jinsi gani huyu bwana hayuko focused yuko out of touch na hajui kwa nini ameajiriwa at most hii ni kejeli kwa wakazi wa Dar Es Salaam.

Jukumu la pili ni posho za madiwani, mradi wa gesi taka na uzoaji wa taka. Mungu wangu huyu mkurugenzi anaishi Dar es salaam kweli au na anendaje kazini maana Dar es salaam yote ni chafu isipokuwa mlango wa kuingilia ikulu ambapo wamepanda maua na parking zote zimeondololewa. Hiyo tu ndo sehemu safi Dar.

Anasema barabara ni zetu lakini ujenzi ni halmashauri na Tanroads, huu ni wehu utasemaje kiwanja ni changu lakini jukumu la kujenga nyumba sio langu na nataka nyumba hapa, kama sio maajabu ni nini?????

Mhasibu naye anachekesha zaidi anataja mradi wa Mabasi ya Kasi ambayo imekuwa hekaya ya abunuwasi miaka nenda miaka rudi, anataja shule ya Benjamin Mkapa ambayo hawajajenga wao alijenga Keenja yaani ni ajabu kweli. Hisa za benki ya wananchi ambayo faida inatakiwa iwe accounted for in forms of dividends. Taa za barabarani ambazo hazipo yaani maajabu tu.

Kwenye chanzo cha mapato mbona hazungumzii National Parking systems??????? Wanaingiza kiasi gani.

Hawa ndio viongozi wetu tutafika kweli.
 
Tatizo la nchi yetu ni uongozi mbovu. Kiujumla hatuna viongozi tuna wafanya biashara na majungu. Kuna watu wakipewa nafasi huwa hawafanyi ajizi ila kwa sababu za masilahi binafsi na roho ya kutu wanafunikwa kwa manufaa ya kundi fulani. Mimi ninaamini tukiwa na kina MAGUFULI Kumi kwenye wizara tutaendelea.

Magufuli ni mtendaji mzuri sana ila anapigwa zengwe. Huyu bwana alikuwa pale miundombinu wakati wa Mkapa alifanya kazi nzuri sana, Muungwana alimuweka wizara ya ardhi alikuwa na vision nzuri sana aliisha sema kama mtu ana kiwanja ameshindwa kukiendeleza atanyang'anywa apewe mwenye uwezo. Kwa kuwa viongozi wengi serikalini wameshikilia viawanja kibao sehemu mbalimbali za jiji wakisubiri vipande bei wauze kwa mamilioni wakati walipewa kwa maelfu tu wakamuwekea fitina muungwana nae akamuhamishia wizara ya uvuvi.

Tatizo letu ni kukosa viongozi basi ila kitu kinawezekana. Kuwapatia watu kama kina Magufuli sehemu muhimu wakafanya kazi nzuri haimaanishi watakuwa tishio kwa wenye uroho wa urais 2015 waliokaribu na muungwana. Tufanye mambo kwa kulisaidia taifa siyo kuwalinda watu fulani. Tanzania yenye maendeleo na utendaji mzuri inawezekana mradi tu watendaji wazuri wapewe nafasi ya ku-impliment idea zao bila kuingiliwa na mtu kwa sababu zozote zile

Sawa Mkuu nimekusoma. Maamuzi magumu yamefanyika na jiji la Dar Es Salaam limevunjwa rasmi. Suala ni kama kuvunjwa kwa jiji la Dar Es Salaam kutasaidia kutatua matatizo yaliyotajwa kwenye hii thread. Only time will tell.
 
Nyerere aliliona hili tangu 1973 na lingefanyika ilivyopangwa Dar isingekuwa na population kubwa kuliko uwezo wake na Dodoma mji ambao uko planned ndio ungemeza population ya watz wengi kwani shughuli nyingi za kiserikali na kibiashara zingekuwa hapo. Lililofanyika sana sana ni mjengo wa Bunge.........
Haya tayari wamehamia Dodoma , kuna mabadiliko ?
 
Back
Top Bottom