KCMC wana wahudumu wabovu sijawahi ona!

Eeka Mangi

JF-Expert Member
Jul 27, 2008
3,173
481
KCMC hospitali kubwa inayotegemewa kutoa huduma za hali ya juu lakini ina wafanyakazi bomu kabisa.
Nilikwenda pale leo kupata huduma. Nikapata maelekezo kuwa niweke kadi yangu ili wakatafute faili langu lilipo. Yule mhudumu akatuelekeza tuende pahali pa kulipia hayp mafaili. Nilikaa kwa muda wa saa moja, sikusikia jina langu likiitwa.

Nilirudi pale mapokezi nikakuta kadi yangu iko palepale nilikoambiwa niiweke. Nikauliza kulikoni nikajibiwa nikae kwenye benchi nisubiri. Nikamwambia yule dada kuwa nimekaa zaidi ya saa moja sasa kusubiri faili langu liletwe. Akanishangaa na kuanza kuniambia kuwa mimi ni mwongo. Baada ya majibizano ya muda yule dada akanambia nisimfundishe kazi!

Ilibidi nimwonye kuwa yeye ni mhudumu na ni haki ya mteja kupata huduma kwa wakati. Alituacha pale mapokezi na kurudi nyuma ya meza akaanza kuhangaika na laptop yake pale.

Kusema ukweli tulikaa sana hadi sita na nusu. Doctor wangu baada ya kutokuniona alinipigia simu kujua kulikoni. Nikamweleza yaliyotokea ilibidi aende kutafuta faili na kuja kunitibia ingawa sikufanikiwa kupata vipimo vyote.

Hivi jamani hawa wahudumu wa kutunza kumbukumbu wao ni nani na ni nini kinawapa jeuri kiasi cha kuona wateje/wagonjwa kama takataka fulani hivi? KCMC they need to do something about this!
 
labda nesi alikuwa busy facebook

hakuna meneja wala supervisor hapo kucheki huduma zinaendaje? Maana hizi hospitali zetu huduma zake unaweza kulia.........
 
demoralized people providing services......by the way why generalize to all KCMC staffs? Na mwenzetu hata umepigiwa simu na daktari kwa kweli huduma ilikuwa juu
 
Pole Eeka Mangi kwa yaliyokusibu.

Ila ni kitu kimoja nachoshindwa kabisa kuelewa na sitajakaa nielewe. mtu kazi yako, ni fani yako, uliomba mwenyewe na ukakubalika au kama uliunganishiwa pia ni sawa na unapokea kila mwisho wa mwezi mshahara kutokana na kazi yako. Inakuwaje mtu huyo huyo analeta kiburi na kujua kwingi? Hahudumii wateja kama inavyopaswa? Na hii pia imo sana kwa watu wa records katika ofisi za Umma.

Mimi kwa kweli huwa naogombana nao sijali umenipita umri wala nini. Naongea na wewe mara ya kwanza politely na ya pili politely ya tatu ni ninamletea ukali. maana huwezi nichelewesha mimi kumuona daktari au kupata huduma kwa sababu ya upuuzi wako na uvivu. I don't spare such people.......Pole sana Mangi.
 
Back
Top Bottom