Kazi na umri

KICHAPO

Member
Oct 19, 2010
51
0
Wana JF habari za weekend,hivi inakuwaje taasisi au shirika linatangaza nafasi za kazi halafu wanaweka kitu wanaita AGE LIMIT yaani kuna umri ukiwa umezidi hapo usiombe.Zaidi wanapenda not more than 35 yrs,sasa wanaosoma wakiwa over 35 waende wapi?
 
Ni labour exploitation tu ya taasisi na mashirika yetu ya hapa bongo,I think wanaona wenye miaka michache hawana experience kubwa so they will not need too much salary na hawana familia kubwa.ukiangalia job adverts za organizations nyingi za nje hawaangalii umri wao wanaangalia yo qualifications. na pia wanapenda utume resume ambayo sio lazima uonyeshe birth date
 
Inashangaza sana! Wanaume wananyanyapaliwa ktk ajira pamoja na age limit. Utakuta wanaandika Coy X is an equal opportunity employer, however Women are encouraged to apply. Na ukiona hivyo athubutu mwanaume ku apply, ataishia kuuza sura tu. Harafu, hii ni nchi pekee ambayo haithamini ajira za wazawa. Secular ya ajira iko wazi kuwa wageni wanaakiriwa ktk nafasi ambazo wenyeji hawaziwezi lakini kuna mameneja wengi wanaajiliwa kwa kazi za kawaida kabisa!
 
Inashangaza sana! Wanaume wananyanyapaliwa ktk ajira pamoja na age limit. Utakuta wanaandika Coy X is an equal opportunity employer, however Women are encouraged to apply. Na ukiona hivyo athubutu mwanaume ku apply, ataishia kuuza sura tu. Harafu, hii ni nchi pekee ambayo haithamini ajira za wazawa. Secular ya ajira iko wazi kuwa wageni wanaakiriwa ktk nafasi ambazo wenyeji hawaziwezi lakini kuna mameneja wengi wanaajiliwa kwa kazi za kawaida kabisa!

Shida yenu wabongo siyo waaminifu ndo maana wanawekwa foreigners. Wewe unakuta mtu ana mkopo wa 10billion, biashara bado haija anza kuchanganya ili alipe mkopo lakini wabongo (mameneja) wanataka kupiga deal.
 
Suala la umri kazini linazingatiwa kwasababu kuna kazi zinahitaji vijana wenye nguvu. Kazi kama hizo watasema umri usizidi kwa mfano miaka 35. Kuna kazi kama za ulinzi unaohitaji ukakamavu, watataka unapoomba kazi usiwe zaidi ya 30.

Kuna nyingine zinahitaji uzoefu wa muda mrefu na busara, haitegemewi eti kijana ana miaka 25 alafu anakuwa mkurugenzi. Kazi kama hizo watataka mtu awe na zaidi ya miaka 40.

Kuna kazi nyingine, muajii anataka kumtumia mfanyakazi kwa muda mrefu kabla hajastaafu, muajiri wa namna hiyo atasema kuwa muombaji asizidi miaka 45 kwa mfano.

Kwa hiyo kuna vigezo vinavyokuwa vinatakiwa na muajiri ambavyo vinakuwa reflected na umri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom