Kazi ipo kweli, inamaana CAG na ripoti ya Jairo haaminiki?

Dahh! napita tu


Aoccdrnig to rscheearch at Cmabrigde Uinervtisy, it deosn't mttaer in waht oredr the ltteers in a wrod are, the olny iprmoatnt tihng is taht the frist and lsat ltteer be at the rghit pclae. The rset can be a toatl mses and you can sitll raed it wouthit a porbelm. Tihs is bcuseae the huamn mnid deos not raed ervey lteter by istlef, but the wrod as a wlohe.
 
Kwa hili mimi ningependa kutofautiana na wachangiaji wengi. CAG hana makosa. Ripoti yake ipo sahihi kabisa. Yeye alipewa ANSARD ya Bunge ambayo akatakiwa alinganishe kilichoandikwa ndani ya Ansard kama kinaendana na uhalisia wa kilichofanyika. Kwenye Ansard imeandikwa kuwa zilizochangishwa ni shilingi Bilioni moja kutoka Idara 20. Wakati wa uchunguzi ikaja kuonekana kuwa kilichochangishwa ni Shilingi Milioni 500 kutoka katika Idara 4.

Kwa hiyo alichotakiwa kuwakilisha ni kama tuhuma za Bilioni moja ni za kweli, akakuta si za kweli na Je tuhuma ni Idara ishirini ni za kweli akakuta kwamba si za kweli. Ripoti yake akaikabidhi kwamba alichokikuta ni tofauti na kilichoandikwa basi!

Lakini hakusema kwamba eti Jairo si Mwizi. Lakini Luhanjo ndiye aliyerukia na kudai kwamba kwa sababu tu pesa inayotajwa kwamba Jairo ameiba ni tofauti na ile iliyokutwa ameiba, basi waliomshitaki Imekula kwao. Kwa hiyo hakuona haja ya kuendelea na hatua ya pili ya Uchunguzi ambao ungewashirikisha Polisi na Takukuru.

Siku ya Ukombozi wa nchi hii kuna watu watachinjwa kama kuku pamoja na familia zao. Labda waikimbie nchi!
 
CAG kathibitisha kwamba 500+ mil ndizo zilizohamishwa na siyo 1.0 bil. Cag hakusema kwa kufanya hivyo ni sahihi au la.

Maswali ya kujiuliza:
1. Je kanuni na sheria za fedha zinamruhusu Jairo kufanya alichofanya?
2. Nani waliolipwa fedha hizo?
3. Malipo haya yalitoka katika mafungu yapi na je yalikasimiwa kwa ajili hii?
4. Je kuhamisha sh.500mil badala ya sh. 1.0bil aliyotuhumiwa nayo kunamwondolea kosa?
CAG hakuyasema haya au mimi ndiye sikuyasikia.

Yapo maswali mengi kuliko majibu!! Sijui kama Luhanjo alifanya meditation before he convened the press conference.
 
wabongo sijui mpaka muone nini ndio mjue CAG na taasisi za namna hiyo hazina uwezo wa kuchunguza na kugundua madudu report zao nyingi ni cut and paste.
Kama mtadurufu report ya procurement audit ya tanesco 2007 ndio mtaona tofauti na kwanini PCCB walichemka, ningeshauri kamati ya bunge iteue consultant kauzu aende between lines.
 
Kwa nini watanzania wengi wameshindwa kuamini maamuzi ya serikali (kupitia Ikulu) juu ya suala la Jairo, je ofisi ya CAG haiaminiki tena?
Well tell me if there is any Best Practices there, a good audit report should be able to reach a conclusion beyond any doubt, audit ya huyu bwana ilikuwa na subject ambaye is in relation to the auditor hence conclusion is most likely to be driven in way to please the client who is the auditors boss, hebu ingia kwenye taaluma hii ndipo unaweza kuelewa. CAG is not independent.!
 
Well tell me if there is any Best Practices there, a good audit report should be able to reach a conclusion beyond any doubt, audit ya huyu bwana ilikuwa na subject ambaye is in relation to the auditor hence conclusion is most likely to be driven in way to please the client who is the auditors boss, hebu ingia kwenye taaluma hii ndipo unaweza kuelewa. CAG is not independent.!
Nakubaliana na wewe mkuu,
Ingawa kitaaluma, Auditor huwa hawezi kumshitaki au kumtuhumu mtu ktk ripoti, ila yeye huripoti alichokiona na mtoa maamuzi ni mwingine, so mwenye makosa hapo anaweza kuwa Luhanjo
 
Hivi sakata la Jairo halikuwapa kibarua TAKUKURU i.e. haikuwa assignment ya Dr. Hosea pia ni Utoh tu?
 
Hivi sakata la Jairo halikuwapa kibarua TAKUKURU i.e. haikuwa assignment ya Dr. Hosea pia ni Utoh tu?
Tatizo ni uchanganyaji wa majukumu, CAG kazi yake ni kutoa ripoti, na implication ya maamuzi huwa si yake bali ni uongozi (kwa hili suala ni serikali), kwa hiyo wao walitakiwa waichambue na kuangalia implication ya alichoandika CAG, then wafanye maamuzi, ila kwa hili maamuzi ya serikali yalikuwa ndiyo hayo, ila watanzania ndiyo hatutaki, kwa nini?
 
Kwa nini watanzania wengi wameshindwa kuamini maamuzi ya serikali (kupitia Ikulu) juu ya suala la Jairo, je ofisi ya CAG haiaminiki tena?
Sijui kama kulikuwa na umuhimu wa CAG,
swala ni kuuliza taasisi ziseme ndio au hapana.
TAASIS si zinzjulikana????
Nawe pia ni gamba kumbe
 
CAG kathibitisha kwamba 500+ mil ndizo zilizohamishwa na siyo 1.0 bil. Cag hakusema kwa kufanya hivyo ni sahihi au la.

Maswali ya kujiuliza:
1. Je kanuni na sheria za fedha zinamruhusu Jairo kufanya alichofanya?
2. Nani waliolipwa fedha hizo?
3. Malipo haya yalitoka katika mafungu yapi na je yalikasimiwa kwa ajili hii?
4. Je kuhamisha sh.500mil badala ya sh. 1.0bil aliyotuhumiwa nayo kunamwondolea kosa?
CAG hakuyasema haya au mimi ndiye sikuyasikia.

Yapo maswali mengi kuliko majibu!! Sijui kama Luhanjo alifanya meditation before he convened the press conference.
Siasa mchezo mchafu??????..
Utoh kumbe nae mwanasiasa???
Nchi imekwisha.
 
Inachekesha kumpa kazi mkaguzi mkuu kazi ya kukagua fedha zilizokusanywa kifisadi kwa ajili ya mtumizi y kifisadi. Anaeyejua accounting atakwambia CAG atatoa ripoti kwamba fedha zimetumika kwa kusudio sawa! Hii haina maana Jairo hakua na makosa, kimaadili Jairo ni fisadi aliyekusanya fedha kifisadi, kwa rukhsa ya wakuu wake mafisadi na kuitumia kifisadi, na huu ni ufisadi! Kwa hili Jairo, Malima, Ngeleja wangekua kwenye serikali makini yenye maadili wangekua jela hivi sasa! Lakini kwa serikali ya mzee wa kufuturisha, yeye yuko busy kujikusanyia thawabu kwa kufuturisha!

Ngeleja aliacha kushiriki vikao vya bunge dodoma akakimbilia dar kumlaki Jairo, unadhani ni bure? hawa watu walikuwa wanakula pamoja hasa zile 10% za wanaijiita wawekezaji! kuna tetesi kuwa jairo alihongwa na Wachina kwenye mradi wa gas karibu sh. 3b! ndio maana jana Ngeleja anamkumbatia Jairo utadhani mkewe! Lol!
 
Back
Top Bottom