Kawambwa ni Mzigo kwa Taifa...

Kwa hili la matokeo na ofisi ya waziri mkuu wawajibike sio kawambwa pekee,yupo waziri anajiita kasimu majaliwa wakati mnyika anatoa taadhali ya mgomo wa walimu yeye aliibuka na kutoa maneno ya dharau,huyu ndie anayeshughulikia elimu ya msingi na sekondari
 
Bora wewe umemuona kama mzigo wa Taifa, mimi namwona kama mzigo wa Misumari/mzigo wa Moto pia - Haubebeki na unamuumiza mbebaji. JK amejitahid kumbeba kwa mbeleko za kila aina ili afike naye anakotaka kufika naye ila huyu Mzee anazichana. Sa sijui anataka kushuka kwenye hiyo mbeleko au hajui maana ya kubebwa!! Mi simuelewi huyu mzee, akumbuke yote haya anayofanyiwa na JK ni kwa cost ya walipa kodi wa Tanzania. Mimi nadhan ilipaswa atumie busara yake ya kawaida tu kustep down na kupisha wengine sio hadi asubiri amuumize mbebaji!!!
 
Tume? Kawambwa kujiuzulu? Pinda kujiuzulu? Ndalichako kujiuzulu?

Haya maswali yanalenga kupoteza mtazamo wa tatizo husika!

Matokeo ya form 4 ni zao la tatizo la mda mrefu, na co kukurupuka tu na kuanza kuongea kwa maswali ya hapo juu!

Cha kujiuliza kwa nn wamefeli? Tuchambue matokeo ya form 4 kwa kuangalia miaka kumi na tano nyuma, ufaulu ulikuwaje?, hali ya elimu ilikuwaje?, mfumo mzima ulikuwaje?, tuangalie kwa kina palitokea nn hapo katikati?.

Mie ntaongelea shule za kata kama chanzo kimoja wapo na athari yake kwa taifa!

Wewe mzazi unampeleka mwanao shule ya kata! Kuna mwalimu mmoja! Yeye ndo mwalimu wa civics, mathematics, geography, physics na etc! Shule haina kitabu hata kimoja! Shule haina maabara (waziri amenukuliwa akisema serikali itaendelea kujenga maabara kwa kutegemea na bajeti) uku curriculum ikiyumbishwa (joseph mungai alilala na akaota, kesho yake akasema masomo ya biashara na kilimo yafutwe) watu wakapiga kelele yakarudishwa kwa kuhofia nguvu ya umma! Bosi wake akafurahishwa na uchapa kazi wake akamzawadia wizara nyingine! Mda ukapita akaja waziri mkuu lowasa na shule za kata, wazazi wakashurutishwa wachangie ujezi, wasomi wakasema hilo ni bomu kubwa sana! Wakapiga kelele mkuu wa nchi akadai hawajui lolote! Tukasahau yote! Juzi mbatia kasema bungeni! Wakamwona mwendawazimu! Leo kila mtu anamtazama kwa jicho husda!

Nini suluhisho! Tuanze upya na tufanye suluisho litalodumu miaka mia mbele na sio hilo la wanasiasa linalodumu siku moja!


Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Jamaa hata ukimuangalia anavyojadili mambo unagundua uwezo wake wa kufkiri ni mdogo mno. Hakutakuwa na mabadiliko chanya katika elimu ya Tanzania endapo watu kama Kawambwa watakabidhiwa dhamana ya kuendeleza elimu nchini. Binafsi nimewahi kukaa na Mh. Kawambwa kwa dakika kadhaa. Jamaa hawezi Kudiscuss issues hata za kawaida. Kwa kifupi, bila kujali taaluma aliyonayo, mazingira yanaonesha jamaa ana uwezo mdogo wa Kufikiri.
 
Hii WIZARA YA ELIMU mkitaka kupima ugumu wake basi awekwe LOWASSA ndo mtaelewa matatizo yake.....ni wizara inayomgusa kila mwananchi ni wizara yenye migogoro isiyoisha....Walimu wanamgomo baridi yani wanafundisha kishikaji matatizo yao yanaeleweka ikiwamo ya maslahi duni na wengine ni voda fasta.....Bunge linahusika kwa kufuta baadhi ya mitihani hasa ya darasa la nne na kidato cha pilli...kwa hayo yote KAWAMBWA anahusika vipi baba wa watu? upole wake isiwe tatizo basi apewe ata MAGUFULI chini ya migogoro iliyopo uone kama kuna jipya...upole wa mtu sio tija mbona SHEIN nae ni mpole lakini mlinganishe na unaemjua......


Humjuwi Kawambwa wewe tena bora unyamaze. Nani kakwambia Kawambwa mpole? Nani kakwambia Shein mpole? Watu hawa noma uliza wanaofanya nao kazi wakueleze madudu yao. Pamoja na ugumu wa wizara ya elimu Kawambwa haiwezi kutokana na uwezo wake mdogo. Matatizo ya wizara ya elimu yanajulikana lakini ya Kawambwa ni zaidi ya hayo. UDSM performance ilikuwa poor, Miundombinu akaharibu zaidi, huyu mwenye uwezo mdogo ilikuwa lazima apewe wizara ngumu kama ni lazima binamu apewe wizara?
 
Anangoja nn? apigwe Chini. Hasara tu na kutupotezea muda tunaotaka maendeleo.
Mr Presidah.......:israel:Remove the rejects
 
Kawambwa ni Mzigo mzito katika Baraza lote la mawaziri yeye ndiye unaongiza kwa Udaifu
 
Wadau tupunguze jazba tuwe objective kwann tunataka mhe. kawambwa aondoshwe. Ni nn alichoshindwa kukifanya? Je km hana delivery capacity kwann anabadilishiwa wizara kila kukicha? Nachojua kawambwa sio mtu wa siasa km wenzake akina mwakyembe,magufuli etc. Inawezekana kinachofanya aonekane ni mzigo ni uwezo/capacity wa kisiasa kutangaza majukwaani yale yaliyofanywa chini ya utawala wake. Nalofikiri mimi kawambwa anatimiza malengo ya aliyemteua kwa 100% vinginevyo asingeendelea kumchagua. Ni ironic kufikiri rais anaweza kuchagua mtu anayemwangusha. Na hata km kuna mapungufu wa kulaumiwa si kawambwa yeye ni mteuliwa tu. Huo ni mtazamo wangu.
 
Bora wewe umemuona kama mzigo wa Taifa, mimi namwona kama mzigo wa Misumari/mzigo wa Moto pia - Haubebeki na unamuumiza mbebaji. JK amejitahid kumbeba kwa mbeleko za kila aina ili afike naye anakotaka kufika naye ila huyu Mzee anazichana. Sa sijui anataka kushuka kwenye hiyo mbeleko au hajui maana ya kubebwa!! Mi simuelewi huyu mzee, akumbuke yote haya anayofanyiwa na JK ni kwa cost ya walipa kodi wa Tanzania. Mimi nadhan ilipaswa atumie busara yake ya kawaida tu kustep down na kupisha wengine sio hadi asubiri amuumize mbebaji!!!
Big up Mkuu, hatimaye hata wabebaji, Chama chake ambacho ndiyo kiko madarakani kimemtangaza rasmi kuwa ni MZIGO KWA TAIFA
 
Afadhali ameanza kujitambua, matokeo ya wanaojiunga na Kidato cha I 2014 yametangazwa na TAMISEMI
 
JK,alisema uRais wangu hauna ubia na mtu,kumbe alikuwa anamjumlisha na KAWA MBWA,ndo waziri aliyevunja rekodi ya TZ toka tupate Uhuru,haijawahi tokea Waziri kubadilishwa kila wizara pindi mwenye ubia nae anapolazimwishwa na BUNGE kufanya mabadiliko.
 
Natofautiana na wewe mkuu.
Yote uliyoyasema juu ya Kawambwa hayana mshiko.
Matatizo ya Wizara ya Elimuyapo hapo siku nyingi sana hata kabla ya yeye kuteuliwa wizarani pale.
Kwa mantiki ya usomi, vijana wa sekondari hukaa shuleni miaka minne, kupata DIV 4 si matokeo ya mwaka mmoja, ni accumulation of failures.
Ni vema ukatueleza wizara iliyoexcel kwa kipindi hiki katika utendaji, kipindi ambacho serikali nzima ina ukata wa kutisha.
Kweli Kawambwa hana machachari wal kujivuna au kupenda mapambano na malumbano, kwa tunao mfahamu hebu mchokoze.

Sasa kwakua amekuta wizara ina matatizo na yeye anayaacha na kuyaongezea mengine?ukimtetea kawambwa unalihujumu Taifa.ok,sasa hana akili ya kupima kuwa ameshindwa kazi?ANASUBIRI NINI KUJIUZULU,ANASHINDWA HATA KUJIONGEZA KICHWANI?KWANINI AKAE KWENYE KITI AMBACHO HAKIMTOSHI?
 
kawambwa ni ndugu wa damu wa kikwete, hawezi kumfuta kazi hata siku moja. tangu mwanzo kawambwa amekuwa akivurunda lakini badala ya kufutwa kazi amekuwa akihamishwa kutoka wizara moja hadi nyingine. haya ndio madhara ya undugunization.
 
Back
Top Bottom