Ufunguo
JF-Expert Member
- Aug 18, 2012
- 330
- 231
Hivi Rais anaposema,
"Nawaambieni, mkifanya mchezo ipo siku mtakuja kujuta maana mkishamchagua kiongozi asiyefaa, mtalazimika kuwa naye huyohuyo hadi 2017, na kama Waswahili wanavyosema majuto ni mjukuu," (Mwananchi, Octoba 27, 2012)
And,
"siku zilizopita vitendo vya rushwa vilikuwa vikihusishwa zaidi na wanaume, lakini sasa hata makundi ya kina mama nao wameanza kujihusisha na rushwa (Mwananchi, Oct 27, 2012).
Mimi mlalahoi sipati picha.
Au anasema kwamba sasa rushwa inazidi kuota mizizi na muda si mrefu hata watoto wetu wataanza kuomba rushwa?, maana baba tayari, mama naye tayari, Kijana nae kama baba, kama mama. Kwa hiyo kwa hesabu zile za kale kama A=B=C =D then B=C=D=?.
Au anataka kusema kwamba taasisi zilizopo za kupambana na rushwa zimeshindwa kazi na kama ndo hivyo kwanini zinaendelea kuwepo?, kwani madaraka aliyonayo kazi yake ni nini?
Halafu anaposema mkichagua asiyefaa mtaendelea kuwa naye huyohuyo hadi mwaka 2017 maana yake ninii?. Anataka kusema hata kama mtu ni kilaza kwasababu tu amechaguliwa ndani ya CCM ataendelea kuongoza hadi uchaguzi mwingine ufanyike?. Au ansema mfumo wa uongozi ndani ya chama ni mbovu kiasi kwamba haiwezekani kumwajibishwa mwenye makosa?.
Napata kizungumkuti, sielewi hata Madaraka ya Rais yako wapi,
Naomba ushauri.
"Nawaambieni, mkifanya mchezo ipo siku mtakuja kujuta maana mkishamchagua kiongozi asiyefaa, mtalazimika kuwa naye huyohuyo hadi 2017, na kama Waswahili wanavyosema majuto ni mjukuu," (Mwananchi, Octoba 27, 2012)
And,
"siku zilizopita vitendo vya rushwa vilikuwa vikihusishwa zaidi na wanaume, lakini sasa hata makundi ya kina mama nao wameanza kujihusisha na rushwa (Mwananchi, Oct 27, 2012).
Mimi mlalahoi sipati picha.
Au anasema kwamba sasa rushwa inazidi kuota mizizi na muda si mrefu hata watoto wetu wataanza kuomba rushwa?, maana baba tayari, mama naye tayari, Kijana nae kama baba, kama mama. Kwa hiyo kwa hesabu zile za kale kama A=B=C =D then B=C=D=?.
Au anataka kusema kwamba taasisi zilizopo za kupambana na rushwa zimeshindwa kazi na kama ndo hivyo kwanini zinaendelea kuwepo?, kwani madaraka aliyonayo kazi yake ni nini?
Halafu anaposema mkichagua asiyefaa mtaendelea kuwa naye huyohuyo hadi mwaka 2017 maana yake ninii?. Anataka kusema hata kama mtu ni kilaza kwasababu tu amechaguliwa ndani ya CCM ataendelea kuongoza hadi uchaguzi mwingine ufanyike?. Au ansema mfumo wa uongozi ndani ya chama ni mbovu kiasi kwamba haiwezekani kumwajibishwa mwenye makosa?.
Napata kizungumkuti, sielewi hata Madaraka ya Rais yako wapi,
Naomba ushauri.