Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Jamani wana JF:
Hii imekaaje? Leo asubuhi katika kipindi cha BBc (swahili) nilimsikia John Selembi akimhoji mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Francis kiwanga kuhusu kifo cha gaidi Osama bin Laden.
kiwanga alisema kuuwawa kwa Osama ni sawasawa kwani yeye pia aliua watu bila hatia.
Kwa mtu wa kawaida kauli hiyo ni sawa, lakini kwa yeye akiwa mkuu wa kituo kinachotetea sheria na haki za binadamu siyo sahihi kabisa. Hawezi akasema hivyo wakati taasisi yake inasimamia na inatetea haki ya binadamu pamoja na utaratibu wa mkondo wa sheria kuhusu watuhumiwa -- kwamba wafikishwe mahakamani ili haki itendeke.
Kauli hiyo ya Kiwanga ina maana kwamba muuwaji akiua naye auwawe bila kufuata mkondo wa sheria, kitu ambacho sicho LHRC inakisimamia.
Selembi alimbana sana kiwanga kwa kauli hiyo naye akarudia tena majibu hayo hayo.
Ni bora Kiwanga angeishia tu kwa kusema: "Kuuwawa kwa Osama ni sawa lakini ni bora angekamatwa na kufikishwa mahakamani."
Hii ingemtakasa Kiwanga na hasa katika kile taasisi yake inachokisimamia -- hata kama suala la kumkamata Osama lilikuwa gumu sana kama inavyoelezwa.
Nawasilisha mada kwa mjadala.