Jamani mimi sijaelewa hapa mwandishi wa taarifa hii anaelewaje kauli ya Membe imeanza kumtesa. Acheni ushabiki wa. Kijinga nani ambaye hajui kwamba gazeti hili la Mtanzania ni la Rostam Aziz na nani hajui ukaribu wa Rostamu Aziz na EL. Ni vema tukajadili hoja kuliko opinion zingine zenye ushabiki wa kisiasa. Ikumbukwe kuwa wakati Membe alipozikomalia pesa za Radar kurejeshwa Tanzania toka uingereza, gazeti hili la Mtanzania liliandika taarifa kwamba Membe anawaandama wapinzani wake bila kungalia hoja na maslahi ya nchi. Gazeti hili limegua Wabunge Watatu kuwakilisha
Kwa hakika sijapata kuona uchambuzi finyu na thread ya kishabiki kama hii. Kwanza hata ukiangalia sampling ya wale waliohojiwa na utashi nauelewa wao ni aibu. Iddi Azzan ambaye hakufika hata sekondari ataelewa nini kuhusu uchambuzi na mahojiano ya kisomi kama yale. Kwa watu walio na kiu ya kusoma watakuwa na ufahamu kwamba majina ya wahusika wa mauzo ya rada sasa yako wazi na siyo siri tena. Mtu hapati shida kwamba gazeti la Mtanzania ambao sasa limebaki la kufungia maandazi tu kutokana na kujiua kwake, linasimiamia nini na hata umiliki wake ukoje.
Ukweli unabaki kwamba watu wanajaribu kupika kashfa ambazo kila wakizibandika kwa Membe hazigandi. Suala la deni la Libya kwa wanaojua ni hila za waliokuwa wanazitaka na sasa wameungana na mafisadi wengine kulipa kisasi na katika hili Membe ni mweupe kama pamba. Thread hii haina mashiko na kutapatapa kwa kawaida kwa wale mapacha na wapagazi wao.