Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Kitendo cha raisi JK kuagiza kuwa suala la ama muungano uwepo au usiwepo lisijadiliwe kwenye mchakato wa katiba mpya ndilo lililoamsha hamasa za majadiliano na malumbano juu ya muungano.
Kikwete alijua kwa ufasaha kuwa kisaikolojia, ukimkabidhi binadamu vitu hata mia ukamwambia kuwa anaruhusiwa kuvichambua vyote, ila kimoja asikiguse, akili ya binadamu huyo inapuuza vile 99 na kudeal na hicho kimoja alichokatazwa huku akiwaza kuwa kuna nini ndani, na kwa nini amekatazwa kugusa hicho kimoja? Ukimuweka mtu kwenye jumba lenye vyumba 20, ukamwambia anaweza kuingia vyote isipokuwa kimoja, then mtu huyo siku hiyo hiyo ataanza juhudi za kujua kuna nini kwenye chumba alichakatazwa kuingia.
Muda mfupi tu baada ya Kiwete kupiga mkwara kuwa suala la muungano lisijadiliwe, ndipo yalipoibuka malumbano mengi ya watu wakuhoji uhalali wa muungano. Itakumbukwa kuwa ni wakati huo ndipo Sitta alipopeleka mswada wa sheria ya marekebisho ya katiba Zanzibar, na mmoja wa Wazanzibar, ambaye kwa sasa ni moja wapo ya viongozi wa UAMSHO aliuchana mswada ule mbele ya Sitta kwa kudai kuwa kama suala la muungano halijadiliwi, then haukuwa na maana.
Hadi wakati huu suala la muungano ndilo linalojadiliwa kuliko masuala yote yanayohusu katiba. Fuatilia mijadala ya kwenye TV na vyombo vingine vya habari, utagundua kwa sasa mjadala ni muungano tu!
Siwezi kusema kuwa Kikwete hakujua hilo maana naamini anao washauri makini, na alifahamu fika kuwa namna peke yake ya kuibua majadiliano makali juu ya uhalali wa muungano, ni kwa 'kukataza usijadiliwe.'
Kwa mtu yeyote makini, na kwa serikali yeyote makini, vurugu za UAMSHO hazikuja ghafla. Kila mtu aliziona zinakuja na serikali iliziona mapema zaidi pale nakala ya mswada wa sheria ilipochanwa mbele ya kiongozi wa serikali.
Hata hivyo kundi hili haramu liliendelea kulindwa na kusaidiwa na serikali hadi lilipofanikiwa kukoleza sumu ya chuki miongoni mwa wazanzibar, ndipo serikali inazuga kulidhibiti.
Kikwete has to be smarter next time, when he wants to play a game...
Kikwete alijua kwa ufasaha kuwa kisaikolojia, ukimkabidhi binadamu vitu hata mia ukamwambia kuwa anaruhusiwa kuvichambua vyote, ila kimoja asikiguse, akili ya binadamu huyo inapuuza vile 99 na kudeal na hicho kimoja alichokatazwa huku akiwaza kuwa kuna nini ndani, na kwa nini amekatazwa kugusa hicho kimoja? Ukimuweka mtu kwenye jumba lenye vyumba 20, ukamwambia anaweza kuingia vyote isipokuwa kimoja, then mtu huyo siku hiyo hiyo ataanza juhudi za kujua kuna nini kwenye chumba alichakatazwa kuingia.
Muda mfupi tu baada ya Kiwete kupiga mkwara kuwa suala la muungano lisijadiliwe, ndipo yalipoibuka malumbano mengi ya watu wakuhoji uhalali wa muungano. Itakumbukwa kuwa ni wakati huo ndipo Sitta alipopeleka mswada wa sheria ya marekebisho ya katiba Zanzibar, na mmoja wa Wazanzibar, ambaye kwa sasa ni moja wapo ya viongozi wa UAMSHO aliuchana mswada ule mbele ya Sitta kwa kudai kuwa kama suala la muungano halijadiliwi, then haukuwa na maana.
Hadi wakati huu suala la muungano ndilo linalojadiliwa kuliko masuala yote yanayohusu katiba. Fuatilia mijadala ya kwenye TV na vyombo vingine vya habari, utagundua kwa sasa mjadala ni muungano tu!
Siwezi kusema kuwa Kikwete hakujua hilo maana naamini anao washauri makini, na alifahamu fika kuwa namna peke yake ya kuibua majadiliano makali juu ya uhalali wa muungano, ni kwa 'kukataza usijadiliwe.'
Kwa mtu yeyote makini, na kwa serikali yeyote makini, vurugu za UAMSHO hazikuja ghafla. Kila mtu aliziona zinakuja na serikali iliziona mapema zaidi pale nakala ya mswada wa sheria ilipochanwa mbele ya kiongozi wa serikali.
Hata hivyo kundi hili haramu liliendelea kulindwa na kusaidiwa na serikali hadi lilipofanikiwa kukoleza sumu ya chuki miongoni mwa wazanzibar, ndipo serikali inazuga kulidhibiti.
Kikwete has to be smarter next time, when he wants to play a game...