Vyombo mbalimbali vimekuwa vikiripoti vipaumbele vya bajeti ya mwaka mpya wa fedha. Suala ambalo limekuwa na mvuto zaidi ni kukatwa kwa posho za vikao kwa wabunge ambapo ni sehemu ya bajeti ya upinzani.
Hapa hakika tumeona jinsi baadhi ya wanasiasa katika nchii walivyo walafi na ni namna gani wanasiasa hawa hawana utu kwa raia ambao ndiyo waliowaweka madarakani. Naibu katibu mkuu wa chama cha MAPINDUZI bwana JOHN CHILIGATI ametoa kauli inayoonyesha jinsi asivyo na utu na pia jinsi asivyo mzalendo.
Kauli ya kwamba Zitto anataka umaarufu kwa vile sitting allowance zimepunguzwa na kusema wazi kuwa CCM watachukua posho hizo na kama wapinzani hawataki waache ni kauli mbovu sana kwa kiongozi wa ngazi ya juu kama yeye.
Ikumbukwe kwamba mshahara wao uko palepale, posho nyingine ziko palepale na wakiwa bungeni wanalipiwa gharama zote muhimu. Kauli hii imedhihirisha wazi kuwa hata hii kampeni ya kujivua gamba ni danganya toto.
Wenzetu Ulaya wanapunguza matumizi sisi tunaongeza kwa mambo yasiyo na msingi? Mtu alipwe milioni saba gari ya zaidi ya milioni sitini marupurupu kibao bado ashindwe kuwa na utu hata chembe moja? Jeuri ya pesa hizi ndiyo imewahamisha majimboni wako hapa mjini wakijivinjari.
Jamani tembeeni Tanzania kuna umaskini mkubwa sana.
Mbunge akilipwa milioni saba adundulize ajinununlie gari lake mwenyewe kwanza atakuwa na uchungu nalo na atalitunza.
Kwa kauli hii ya Chiligati anazidi kuiweka CCM matatani.
Hapa hakika tumeona jinsi baadhi ya wanasiasa katika nchii walivyo walafi na ni namna gani wanasiasa hawa hawana utu kwa raia ambao ndiyo waliowaweka madarakani. Naibu katibu mkuu wa chama cha MAPINDUZI bwana JOHN CHILIGATI ametoa kauli inayoonyesha jinsi asivyo na utu na pia jinsi asivyo mzalendo.
Kauli ya kwamba Zitto anataka umaarufu kwa vile sitting allowance zimepunguzwa na kusema wazi kuwa CCM watachukua posho hizo na kama wapinzani hawataki waache ni kauli mbovu sana kwa kiongozi wa ngazi ya juu kama yeye.
Ikumbukwe kwamba mshahara wao uko palepale, posho nyingine ziko palepale na wakiwa bungeni wanalipiwa gharama zote muhimu. Kauli hii imedhihirisha wazi kuwa hata hii kampeni ya kujivua gamba ni danganya toto.
Wenzetu Ulaya wanapunguza matumizi sisi tunaongeza kwa mambo yasiyo na msingi? Mtu alipwe milioni saba gari ya zaidi ya milioni sitini marupurupu kibao bado ashindwe kuwa na utu hata chembe moja? Jeuri ya pesa hizi ndiyo imewahamisha majimboni wako hapa mjini wakijivinjari.
Jamani tembeeni Tanzania kuna umaskini mkubwa sana.
Mbunge akilipwa milioni saba adundulize ajinununlie gari lake mwenyewe kwanza atakuwa na uchungu nalo na atalitunza.
Kwa kauli hii ya Chiligati anazidi kuiweka CCM matatani.
"AFRICA POLITICS IS AN INVESTIMENT JUSTFY"