Kauli kama hizi zinakatisha tamaa watanzania wazalendo.....

only83

JF-Expert Member
Oct 15, 2010
5,343
2,525
....Kauli tata zinazotolewa na viongozi wakubwa wa serikali zimeendelea,na wakati huu ilikuwa zamu ya Waziri Omari Nundu alipokuwa akiiongea na wafanyakazi wa shirika la reli mkoani KIGOMA...ishu ilikuwa hivi;wafanyakazi wa shirika la reli KIGOMA walimkumbusha ahadi yake aliyoitoa akiwa MWANZA mwaka jana kuwa serikali itawalipa kifuta jasho wafanyakazi wake baada ya kuingia na kuvunja mkataba na wale wawekezaji dhaifu(RITES)...Baada ya wafanyakazi hawa kumkumbushia ahadi hii waziri alijibu "HAKUNA SUALA LA KIFUTA JASHO,YULE ALIYETAYARI KUFANYA KAZI NA KUIMARISHA TRC ABAKI,YULE ASIYETAKA AONDOKE MWENYEWE MAPEMA,FUTENI KABISA SUALA LA KIFUTA JASHO"

Mawazo yangu:
Kauli kama hizi zimekuwa kawaida kwa wtanzania siku hizi,kuna kipindi walimu waliambiwa asiyetaka kufanya kazi aache nk..Je,serikali hii inayojiita kuwa ni sikivu kwanini inawafanyia hivi watanzania?


Source: Channel Ten News Bulletin
 
Ndivyo inavyowajali kwa kutoa vitisho. Kifuta jasho cha nini wakati tuko bize kufanikisha mchakato haramu wa rasimu ya katiba? Wazee wa Jumuiya ya Afrika Mashariki: Mfano bora wa serikali sikivu kwa watu wake. Hivi unakijua kipaumbele cha ccm kwa sasa? Tazama hapa:

Kazi kubwa iliyobaki kwa ccm ni kujiandaa kikamilifu kushinda uchaguzi wa 2015.
-Steven Wassira.
 
Back
Top Bottom