Kauli hii ya Wilson Mukama...

Easyway

JF-Expert Member
Oct 5, 2012
2,606
3,702
Kwenye ripoti ya kamati ya waziri Nchimbi , Mukama alitoa pendekezo lifuatalo,ninanukuu "Katibu mkuu wa CCM Wilson Mukama,alishauri kufanyiwa marekebisho kwenye sheria ya vyama vya siasa namba 5 ya mwaka 1992 itakayoweka wazi shughuli ya vyama vya siasa baada ya uchaguzi mkuu. Akisisitiza kuwa shughuli ya za siasa baada ya uchaguzi mkuu zihamie bungeni kwa wanasiasa kuhoji mipango ya maendeleo ya Serikali na matumizi ya rasilimali za nachi na wananchi waachwe wachape kazi zao za maendeleo" mwisho wa kunukuu.

Nina maoni yafuatayo kwa Mukama:

Kazi mojawapo ya vyama vya siasa ni kufanya siasa muda wote bila kujali kama kuna uchaguzi mkuu au hakuna ili visiitwe vyama vya msimu na lengo la kufanya hivyo ni kujitangaza kwa kueneza sera zao na mikakati yao ili kujiandaa kwa uchaguzi mkuu unaofuata na uchaguzi wa serikali za mitaa kama uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2014.

Hakuna mwananchi anayelazimishwa kushiriki kwenye shughuli za siasa hivyo si kweli kwamba shughuli za siasa zinasababisha wananchi wasichape kazi zao za maendeleo.

Je,kwa vyama ambavyo vilishiriki kwenye uchaguzi mkuu na havikupata mbunge/wabunge wao watahamishiaje shughuli za siasa bungeni? tusitunge sheria kwa sababu ya kukizuia chama fulani kufanya kazi zake za kujenga chama tuache wananchi wenyewe waamue kama waende kwenye mikutano ya vyama vya siasa au la.
 
Moja ya gonjwa kubwa (Cancer) ndani ya CCM ni kuchaguana kwa kujuana na kimtandao! Mukama hafai hata kuwa mpiga debe wa CCM ni janga!
 
Kuna watu wengine wanatakiwa wanyongwe tu kwasababu hawana maana yeyote duniani......afadhali hata nguruwe anatoa mbolea na nyama yake ni tamu sana kwa wale watumiaji....!!!
 
oh dear!

Gabbage in gabbage out! Mauaji yametokea Iringa, kamati inamfuata Mukama Dar na kumuuliza uendeshwaji wa shughuli za vyama vya siasa! Na wakifanya kama anavyotaka Mukama ina maana Lumumba including yeye Mukama watakuwa hawana kazi!

Pili, aliyeuliwa ni mwandishi wa habari tena akiwa kazini na sio mwanasiasa!

Nadhani kuna haja ya kuangalia tena hukumu alizowahi toa huyo Jaji (mstaafu) Ihema. Amefanya kazi tofauti na hadidu rejea zilivyoeleza, lakini kubwa, ilikuwaje Jaji akaongoza kamati-batili?
 
Uongozi wenyewe aliomba kwa kubembeleza na mkuu wake hupenda kuchagua vilaza ili awaburuze sasa ulitarajia nini.kama methali zingekuwa na maana ya moja kwa moja ningejua hana akili maana akili ni nywele.hii chadema hii itawaua miaka hii.
 
oh dear!

Gabbage in gabbage out! Mauaji yametokea iringa, kamati inamfuata mukama dar na kumuuliza uendeshwaji wa shughuli za vyama vya siasa! Na wakifanya kama anavyotaka mukama ina maana lumumba including yeye mukama watakuwa hawana kazi!

Pili, aliyeuliwa ni mwandishi wa habari tena akiwa kazini na sio mwanasiasa!

Nadhani kuna haja ya kuangalia tena hukumu alizowahi toa huyo jaji (mstaafu) ihema. Amefanya kazi tofauti na hadidu rejea zilivyoeleza, lakini kubwa, ilikuwaje jaji akaongoza kamati-batili?
kwa sababu jaji mwenyewe ni batili.
 
Back
Top Bottom