Wazee mmeiona katuni ya kipanya leo kwenye gazeti la mwananchi ukurasa wa 6,ipo safi sana! Eti CHADUMAA wanazika tu watu kwa siasa zao zinazofanikiwa sana kwa sasa za umwagaji damu ya watanzania maskini na wenye uelewa mdogo
Ujumbe wake hauna mshiko kihiiivyo! Kumwaga damu si vizuri, lakini hata usipomwaga damu, damu yako itakaushwa mwilini na utazikwa vilevile na hao wakausha damu. Tena wakausha damu wanauwezo wa kukausha damu ya watu wengi zaidi kuliko ya wanaomwaga damu. Unaweza ukamwaga damu ili wakausha damu wasiwe tena na chance ya kukausha damu za wanyonge. Watu wamechoka na wachache wamehamua kumwaga damu zao ili damu ya wengi isiendelee kukaushwa na watu wachache. Watu hawaogopi tena vitisho, kwani kufa ni kufa tu, au umekufa kwa kumwaga damu au kwa kukaushwa damu vyote ni vifo, ila wanaokufa kwa kukaushwa damu wamekuwa ni wengi ndio maana sasa watu wamehamua kujitolea kumwaga damu zao ili kuwanusuru wengi zaidi kukaushwa damu zao na watu wachache.