Nimezunguka jana na leo karibu kila nilipotembelea nimesikiliza watu katika makundi kwa furaha au huzuni wakizungumza kuhusu dhana ya kujivua gamba kwa wanachama na viongozi wa CCM. Katika hili hakuna asiye na upande, wapo ambao wanashangilia kuwa kundi pinzani ndani ya chama limepoteza shina na mhimili wake kwa maana ya nguvu ya kifedha aliyonayo Bw. Rostam Aziz. Wapo wanaohuzunika kwa kuondokewa na msamaria mwema wa chama na wanachama wake. Wako wanaosema CCM kwisha habari yake. Wako wanaosema kuwa sasa chama kimeanza kufanikisha ajenda yake ya kujivua gamba na kwa hiyo tutarajie kuona umaarufu wa chama ukirejea kwa haraka kwa sababu waharibifu wake wataondoka mmoja baada mmoja.
Si nia yangu kuunga mkono au kupingana na kundi lolote katika hayo ambayo maoni yake nimeyatoa kwa kifupi hapo juu, bali nataka kutoa tahadhari kwa wote na misimamo yao. Kwa maoni yangu vumbi ndiyo limeanza kutimka, bado tuna njia ndefu sana kuona kile ambacho tunakitegemea sasa.
Kwa kifupi na kwa kurejerea maneno ya RA jana ni kwamba anahasira na watu ndani ya chama chake, anahasira na uongozi wa chama na anahasira na maoni ya watu kuwa yeye ni fisadi. Wananchi wa Igunga wanahasira na chama chao, wanahasira na uongozi wa juu wa chama chao, wanahasira na msimamo hasi wa watu wengine juu ya aliyekuwa Mbunge wao.
Mimi siami na sifikirii kuwa ipo siku Rostam atakiasi chama chake, lakini pia siamini kuwa atakuwa na nafasi ya kuwazuia wanachama wa ccm jimboni kwake wenye mapenzi nae wasiasi na pengine huu ndio utashi wake ingawa ameahidi kuwa mwanachama mtiifu. CCM iliyopokea ajenda CDM kumchafua RA haiwezi kuthubutu kuimba wimbo wa utakatifu wa Rostam mbele ya wananchi wa Igunga, swali je Nnauye na timu yake ya kampeni watabeba ujumbe gani kwenda kumwombea mgombea wao kura kwa wananch wa Igunga. Kiungwana itabidi waimbe wimbo wa Jembe ni jembe maana yake waendelee kuwambia wananchi wa Igunga uchafu wa RA na pia wawe tayari kujibu maswali ya Wanaigunga kwa kile wananachodhani kuhusu Mbunge wao. Maswali yenyewe ni madogo lakini yatakuwa yamebeba ujumbe mzito nayo baadhi nahisi yatakuwa kama ifuatavyo nini hasa dhambi ya RA, kuhusu Richmond watauliza hivi yeye kwenda kuomba kazi serikalini kuna ubaya gani wakati serikali ilikuwa na nafasi ya kumjibu kuwa hatoshi kufanya kazi hiyo badala yake ikampa kwa nini kosa hili la serikali kushindwa kufanya maamuzi sahihi atupiwe RA? Mbona tunasikia hela za Kagoda zilifanya kazi ya kampeni ya Chama iweje leo kosa liwe na RA na mengineyo mengi.
Kisiasa RA amejeruhiwa sana, lakini sasa kutoka kwake katika siasa ni mlima mkubwa kwa chama chake kuepuka kupata jeraha tena sehemu nyeti na ngumu kutibika hata kama daktari ni bingwa kwa sababu kuna uwezekano mwili kushindwa kuhimili tiba hiyo.
Je huu ndio mwanzo wa kuporomoka kwa Chama Tawala, Je turufu ya CCM kuendelea kuwa chama chenye nguvu iko mikononi mwa watu ambao wanaitwa magamba na chama chenyewe? Je Rostam ataendelea kuwa adui wa watanzania na kuhesabika kama mkosaji au kujiondoa kwake katika siasa na majukumu nya kisiasa ni nafasi nzuri ya kuwafanya watanzania watafakari upya ili wamjue na pengine kumtetea kuwa yeye ni mwanakondoo tu katika siasa za ndani ya chama chao?
CCM MNAYO KAZI NA PENGINE HUO MWELEKEO NDIO MUGUMU KULIKO MISUKOSUKO AMBAYO MUMEWAHI KUPATA KATIKA KIPINDI CHOTE CHA MIAKA ZAIDI YA 60 YA UHAI WA CHAMA.
Si nia yangu kuunga mkono au kupingana na kundi lolote katika hayo ambayo maoni yake nimeyatoa kwa kifupi hapo juu, bali nataka kutoa tahadhari kwa wote na misimamo yao. Kwa maoni yangu vumbi ndiyo limeanza kutimka, bado tuna njia ndefu sana kuona kile ambacho tunakitegemea sasa.
Kwa kifupi na kwa kurejerea maneno ya RA jana ni kwamba anahasira na watu ndani ya chama chake, anahasira na uongozi wa chama na anahasira na maoni ya watu kuwa yeye ni fisadi. Wananchi wa Igunga wanahasira na chama chao, wanahasira na uongozi wa juu wa chama chao, wanahasira na msimamo hasi wa watu wengine juu ya aliyekuwa Mbunge wao.
Mimi siami na sifikirii kuwa ipo siku Rostam atakiasi chama chake, lakini pia siamini kuwa atakuwa na nafasi ya kuwazuia wanachama wa ccm jimboni kwake wenye mapenzi nae wasiasi na pengine huu ndio utashi wake ingawa ameahidi kuwa mwanachama mtiifu. CCM iliyopokea ajenda CDM kumchafua RA haiwezi kuthubutu kuimba wimbo wa utakatifu wa Rostam mbele ya wananchi wa Igunga, swali je Nnauye na timu yake ya kampeni watabeba ujumbe gani kwenda kumwombea mgombea wao kura kwa wananch wa Igunga. Kiungwana itabidi waimbe wimbo wa Jembe ni jembe maana yake waendelee kuwambia wananchi wa Igunga uchafu wa RA na pia wawe tayari kujibu maswali ya Wanaigunga kwa kile wananachodhani kuhusu Mbunge wao. Maswali yenyewe ni madogo lakini yatakuwa yamebeba ujumbe mzito nayo baadhi nahisi yatakuwa kama ifuatavyo nini hasa dhambi ya RA, kuhusu Richmond watauliza hivi yeye kwenda kuomba kazi serikalini kuna ubaya gani wakati serikali ilikuwa na nafasi ya kumjibu kuwa hatoshi kufanya kazi hiyo badala yake ikampa kwa nini kosa hili la serikali kushindwa kufanya maamuzi sahihi atupiwe RA? Mbona tunasikia hela za Kagoda zilifanya kazi ya kampeni ya Chama iweje leo kosa liwe na RA na mengineyo mengi.
Kisiasa RA amejeruhiwa sana, lakini sasa kutoka kwake katika siasa ni mlima mkubwa kwa chama chake kuepuka kupata jeraha tena sehemu nyeti na ngumu kutibika hata kama daktari ni bingwa kwa sababu kuna uwezekano mwili kushindwa kuhimili tiba hiyo.
Je huu ndio mwanzo wa kuporomoka kwa Chama Tawala, Je turufu ya CCM kuendelea kuwa chama chenye nguvu iko mikononi mwa watu ambao wanaitwa magamba na chama chenyewe? Je Rostam ataendelea kuwa adui wa watanzania na kuhesabika kama mkosaji au kujiondoa kwake katika siasa na majukumu nya kisiasa ni nafasi nzuri ya kuwafanya watanzania watafakari upya ili wamjue na pengine kumtetea kuwa yeye ni mwanakondoo tu katika siasa za ndani ya chama chao?
CCM MNAYO KAZI NA PENGINE HUO MWELEKEO NDIO MUGUMU KULIKO MISUKOSUKO AMBAYO MUMEWAHI KUPATA KATIKA KIPINDI CHOTE CHA MIAKA ZAIDI YA 60 YA UHAI WA CHAMA.