Jamani katika taarifa ya habari ya TBC katika habari kuhusu wananchi wa kilombero kuisihi serikali iwaache wamalizie msimu huu wa kilimo kabla hawajaondoshwa kama ulimuona yule mama aliyekuwa amepiga magoti na kutambaa, na kuongea kilugha akiomba hisani ya serikali alikuwa akitambaa kumwelekea mtu ambaye alimtaja kuwa ni mwanamke mwenzake na anaomba amsaidie wakati akiendelea niliona mguu wa gongo kama lile alilokuwa akilitumia dada yetu Regia. na moja kwa moja nikagundua kuwa alikuwepo kwenye mkutano ule. ila hawakutaka kumwonyesha!! je hi ni kwa sababu za kimaadili au ni nini? kwa maoni yangu naona engekuwa vizuri kama wangemwonyesha ili kuzidi kutufariji kwa kuondoka kwake!! je wewe mdau unaonaje?NawasilishaSource TBC1