FisadiKuu
JF-Expert Member
- Nov 19, 2015
- 8,108
- 13,346
We kweli kilaza.. Hivi unajua Forbes wanafanyaje research zao kupima utajiri wa mtu?? Au unafikiri wanafanya kwa hisia?? Nenda mitandaoni usome criticism za Forbes Africa. Hivi unawezaje kusema Bakhressa ana net worth ya $ 650 M wakati kumfata ukakaa nae hujawahi.. Maana kama umri tu unashindwa kuujua ina maana umepima utajiri wake kwa hisia na si uhalisia. Kama wangekuja kukaa na Bakhressa au Mengi lazima swali la kwanza lingekuwa Jina kamili, Umri, ulikozaliwa na biashara ulianza lini.Mimi siyo muumini wa ngonjera bali tarakimu kwa hiyo ulichoninukuu nacho ni nonsense tupu.
Wewe usiyehongwa ungeweka net worth hapa siyo porojo tu.
Kama picha na umri vingekuwa muhimu kwenye hiyo orodha wange-download hata mitandaoni.
Kwani MO akiwa wa kwanza au wa mwisho Mimi inanisaidia nini? Ninachohoji mimi ni figures basi.
Again,do you know the shareholders of Chemi&Cotex au umekariri kila kampuni inamilikiwa na mtu mmoja?
Wabongo acheni ujuaji nendeni chimbo muwakosoe Forbes kwa tarakimu siyo story za vijiweni.
Kuna yeyote mwenye ushahidi wa Forbes kuhongwa humu? Uwekeni tuuone.
Chemi & Cotex wako shareholders wangapi? Mohamed yeye unafikiri ile biashara anamiliki mwenyewe?? Chemi and Cotex wanauza bidhaa zao kwenye nchi 13 za Africa.
Hapa hakuna anayeshindania nani tajiri kuliko nani, get your facts right. Tunachoongea hapa ni huyo Mo kuwa overrated kuliko anavyopambwa. Kama Mzee Mengi ilivyotoka hiyo list yao ya Forbes Africa alisema huo si utajiri wake halisi na wala hakuwahi kufatwa wala kupigiwa simu na hao watu bali ni hisia zao tu