Elections 2010 Katika hili Zitto unakwenda na wakati!!

Nicky82

JF-Expert Member
Mar 14, 2009
941
64
Wadau nimetembelea blogu ya Zitto Kabwe na kufurahishwa na jinsi Kampeni zake zinavyoendelea kule Jimboni kwao. Haya ndo mambo ambayo CHADEMA nzima walipaswa kuyafanya. Jambo ambalo inambidi Zitto afanye sasa ni kushare experience hii pamoja na mkurugenzi wake wa habari wa chama.
Kwa Tanzania yetu, hii inaweza kuwa ndio 21st Century campains.
Habari iko kwenye link hii.
Zitto na Demokrasia
 
Iko poa sana hata mimi nashangaa kwa nini chadema hawafanyi hivyo
 
Iko poa sana hata mimi nashangaa kwa nini chadema hawafanyi hivyo
Chadema gani unayoisema ya Kenya Zitto anaomba kura zake na za Slaa wa Chadema au mi sikuona vizuri.
Hebu check:





 
Last edited by a moderator:
Zitto ni mtu mkubwa CHADEMA, ni naibu katibu mkuu na ni kijana kwa hiyo anatakiwa ahakikishe chama kinafanya haya.

Ni kosa lake kama CHADEMA haifanyi hivi. Ikiwa aliwaambia CHADEMA wakakataa sio kosa lake
 
kizuri kinapongezwa,nami nimeona nimpe pongezi zitto kwa ubunifu huo unaopaswa kuigwa na wanamageuzi wengine............japo mimi binafsi nabaki palepale kukosa kumuunga mkono alipoamua kuisaliti tanzania iliyomwamini kwa kushawishiwa kuilazimisha serikali inunue mitambo ya richmond........yaani sijapenda kwa yeye kuwa\ mwepesi wa kununuliwa............na ana malengo binafsi mno kuliko wengine wanavyoelewa..
 
Wadau nimetembelea blogu ya Zitto Kabwe na kufurahishwa na jinsi Kampeni zake zinavyoendelea kule Jimboni kwao. Haya ndo mambo ambayo CHADEMA nzima walipaswa kuyafanya. Jambo ambalo inambidi Zitto afanye sasa ni kushare experience hii pamoja na mkurugenzi wake wa habari wa chama.
Kwa Tanzania yetu, hii inaweza kuwa ndio 21st Century campains.
Habari iko kwenye link hii.
Zitto na Demokrasia


Asante Nicky82 kutuwekea hii ya Zitto.


Hiki tunachokishuhudia hapa,
Zitto na Demokrasia , ni moja ya faida kubwa ya exposure aliyonayo Zitto, over and above viongozi wengine wote wa Chadema ndio maana anapiga kampeni Ki Obama Obama.

Kwa vile Zitto namfahamu kwa karibu, kuna uwezekano wa moja kati ya haya mawili, au yote kwa pamoja.

1. Zitto aliyapendekeza haya yote kwa Chadema, na yakapuuzwa, hivyo yeye binafsi ameamua kuendelea nayo.
2. Kuna uwezekano wametofautiana mahali, ndani kwa ndani, hivyo Zitto ameamua kubaki kivyake, na kuondesha kampeni zake kisasa zaidi ndio maana ile siku ya uzxinduzi wa kapeni yao pale Jangwani, nilitegemea kumuona Zitto ni miongoni mwao, laki nin siku hiyo hiyo Zitto naye alikuwa akizindua kampeni jimboni kwake Kigoma.

Na kufuatia kumfahamu Zitto, his biggest strength is his head, brain, he is bright na briliant up stairs na ana amaizing convincing power, yaani ana nguvu kubwa ya ushawishi kufuatia kujua kupanga na kujenga hoja za nguvu.


His greates weakness, his failure to see the diferent point of view. Vision yake inona only one side of view, the right way, and that is his view no any other view. Akitaka kitu, lazima akipate na akigive in, he is wounded, ndio maana aliwahi kuutaka uenyekiti wa Chadema, na ile kauli yake ya kugombea urais 2015 ni kutuma ujumbe kuwa Slaa hapiti, rais ni JK, hivyo anampata tahadhari Dr. Slaa asijaribu mwaka 2015, itakuwa ni zamu yake.


Kwa maoni yangu, that is wrong, angetakiwa kusubiri uchaguzi umekwisha ameshachaguliwa kurudi mjengoni ndipo aanzishe hako kawimbo ka urais, na ikitokea mjengoni asirudi, huo urais wa 2015 atauanzia wapi!. Msicheze na CCM Jamani, japo watu wa Kigoma, nawaaminia, Mlingotini ni cha mtoto!.
 
So uko ndo alikosema anataka gombea uraisi 2015!
Kaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaazi kweli kweli!
 
Asante Nicky82 kutuwekea hii ya Zitto.

Hiki tunachokishuhudia hapa, Zitto na Demokrasia , ni moja ya faida kubwa ya exposure aliyonayo Zitto, over and above viongozi wengine wote wa Chadema ndio maana anapiga kampeni Ki Obama Obama.

Kwa vile Zitto namfahamu kwa karibu, kuna uwezekano wa moja kati ya haya mawili, au yote kwa pamoja.
1. Zitto aliyapendekeza haya yote kwa Chadema, na yakapuuzwa, hivyo yeye binafsi ameamua kuendelea nayo.
2. Kuna uwezekano wametofautiana mahali, ndani kwa ndani, hivyo Zitto ameamua kubaki kivyake, na kuondesha kampeni zake kisasa zaidi ndio maana ile siku ya uzxinduzi wa kapeni yao pale Jangwani, nilitegemea kumuona Zitto ni miongoni mwao, laki nin siku hiyo hiyo Zitto naye alikuwa akizindua kampeni jimboni kwake Kigoma.

Na kufuatia kumfahamu Zitto, his biggest strength is his head, brain, he is bright na briliant up stairs na ana amaizing convincing power, yaani ana nguvu kubwa ya ushawishi kufuatia kujua kupanga na kujenga hoja za nguvu.

His greates weakness, his failure to see the diferent point of view. Vision yake inona only one side of view, the right way, and that is his view no any other view. Akitaka kitu, lazima akipate na akigive in, he is wounded, ndio maana aliwahi kuutaka uenyekiti wa Chadema, na ile kauli yake ya kugombea urais 2015 ni kutuma ujumbe kuwa Slaa hapiti, rais ni JK, hivyo anampata tahadhari Dr. Slaa asijaribu mwaka 2015, itakuwa ni zamu yake.

Kwa maoni yangu, that is wrong, angetakiwa kusubiri uchaguzi umekwisha ameshachaguliwa kurudi mjengoni ndipo aanzishe hako kawimbo ka urais, na ikitokea mjengoni asirudi, huo urais wa 2015 atauanzia wapi!. Msicheze na CCM Jamani, japo watu wa Kigoma, nawaaminia, Mlingotini ni cha mtoto!.

Pasco, you are right in some ways:

1. Nimependa sana ubunifu wa local campaigns. Ingawa zinahitaji pesa lakini pia kuwa na kile Zitto anachoita "Grass Root Movement" ni muhimu. Hiki ndich anachojaribu kama vile Obama alivyopewa support na MoveOn.org: Democracy in Action

2. Kitu ambacho kwa uhakika kimekosekana Chadema ni coordination ya kampeni. Nilikuwa nategemea hapa DSM ambapo ndiyo centre ya Media kuwe na daily Update ya kampeni zote kwa uzito Mkuu wakati wengine wako field. Zito in his own way so far amekuwa na updates nyingi katika media next to Slaa and may be Ndesamburo. Hata Mbowe hatumsikii kabisa. Kulikoni?

3. Binafsi niliwahi kutaka kuanza initiatives za kutaka CUF, CHADEMA na NCCR na UDP waungane. Aiseeee, huwezi amini ubinafsi unatawala vyama vyote. Zitto alikukuwa open minded kwa hilo. Nampongeza na amekuwa akilisema.

4. Zitto hawezi kugombea urais 2015 kwa kuwa atakuwa hajafikisha 40. Kwa nini alisema, I dont know. lakini kwangu mimi naona ni strategy ya kampeni. ukiangalia baada ya kusema vile Media yote waliipa kipaumbele the next day. Huu ni ubunifu.

5. Ila kimoja, Zitto ajifunze "Kwa pamoja Tutasonga Mbele" katika siasa za Kitanzania zenye kada za namna tofauti, zinahitaji uvumilivu wa hali ya juu. Hata kama wengi wanaweza kuelewa, bado maslahi binafsi pia yanatawala kuliko utaifa. wengine tumejifunza mengi katika uongozi.

Naomba kuwakilisha
 
kaka umejitahidi na hasa baada ya kuiga some styles za kikwete kuwa more socialized hongera, ila siwaige hao wenzio kufanya siasa za maji taka
 
duh mimi Zitto namkubali sana ila ananitia hofu yuko kama anatumika/anaushirikiano na mafisadi . kikwete kakwepa kwenda jimboni kwake pinda kunawakati alimshauri akaze buti mjengoni atapasikia , kuna nini katikati yao????????????????????????:confused2:
 
Asante kwa post yako.

Nampongeza Zito.

Chadema ni lazima ilifanyie kazi suala la kupata matukio ya mikutano ya kampeni. Tukitegemea vyombo vya ccm hatuambulii kitu. Tazama picha za wapinzani anazotela michuzi, ovyooooooo. Afadhali angeacha tu. Linganisha na za ccm anazoleta.

Wiki tatu zilizopita tulilalamika kuwa michuzi haleti habari kwa uwiano sawa wengine wakamtetea. Lakini ukifuatilia habari za kampeni huhitaji kuambiwa kuwa ameegemea kwa upande gani. Kwa hakika yupo mpiga debe wa ccm 99%. Fuatilia habari na picha anazotuma utaona.

Kwa maoni yangu michuzi aache kuleta matukio ya kampeni ya vyama vya upinzani. Aambatane na ccm na Jk wake, kuliko kutuhadaa.
 
Asante Nicky82 kutuwekea hii ya Zitto.

Hiki tunachokishuhudia hapa, Zitto na Demokrasia , ni moja ya faida kubwa ya exposure aliyonayo Zitto, over and above viongozi wengine wote wa Chadema ndio maana anapiga kampeni Ki Obama Obama.

Kwa vile Zitto namfahamu kwa karibu, kuna uwezekano wa moja kati ya haya mawili, au yote kwa pamoja.
1. Zitto aliyapendekeza haya yote kwa Chadema, na yakapuuzwa, hivyo yeye binafsi ameamua kuendelea nayo.
2. Kuna uwezekano wametofautiana mahali, ndani kwa ndani, hivyo Zitto ameamua kubaki kivyake, na kuondesha kampeni zake kisasa zaidi ndio maana ile siku ya uzxinduzi wa kapeni yao pale Jangwani, nilitegemea kumuona Zitto ni miongoni mwao, laki nin siku hiyo hiyo Zitto naye alikuwa akizindua kampeni jimboni kwake Kigoma.

Na kufuatia kumfahamu Zitto, his biggest strength is his head, brain, he is bright na briliant up stairs na ana amaizing convincing power, yaani ana nguvu kubwa ya ushawishi kufuatia kujua kupanga na kujenga hoja za nguvu.

His greates weakness, his failure to see the diferent point of view. Vision yake inona only one side of view, the right way, and that is his view no any other view. Akitaka kitu, lazima akipate na akigive in, he is wounded, ndio maana aliwahi kuutaka uenyekiti wa Chadema, na ile kauli yake ya kugombea urais 2015 ni kutuma ujumbe kuwa Slaa hapiti, rais ni JK, hivyo anampata tahadhari Dr. Slaa asijaribu mwaka 2015, itakuwa ni zamu yake.

Kwa maoni yangu, that is wrong, angetakiwa kusubiri uchaguzi umekwisha ameshachaguliwa kurudi mjengoni ndipo aanzishe hako kawimbo ka urais, na ikitokea mjengoni asirudi, huo urais wa 2015 atauanzia wapi!. Msicheze na CCM Jamani, japo watu wa Kigoma, nawaaminia, Mlingotini ni cha mtoto!.

Very objective. Asante sana. Mapungufu ni sehemu ya ubinaadamu na yanarekebishika na nipo tayari kwa hilo siku zote.

Mie nimetoka familia masikini sana, nimekwenda shule mpaka darasa la pili pekupeku. Kutokana na kuwa msikivu nimefika hapa nilipo. Kwa ushauri wa watu kama ninyi nitafika mbali zaidi.

Namsikiliza mtu mwenye nia njema hata akinisema vibaya namna gani. Ninafunga masikio kwa yeyote mwenye nia mbaya, chuki na mwenye kuhukumu hata akinisema vizuri namna gani.

Maoni yako ni objective sana. Weaknesses noted brother
 
Very objective. Asante sana. Mapungufu ni sehemu ya ubinaadamu na yanarekebishika na nipo tayari kwa hilo siku zote.

Mie nimetoka familia masikini sana, nimekwenda shule mpaka darasa la pili pekupeku. Kutokana na kuwa msikivu nimefika hapa nilipo. Kwa ushauri wa watu kama ninyi nitafika mbali zaidi.

Namsikiliza mtu mwenye nia njema hata akinisema vibaya namna gani. Ninafunga masikio kwa yeyote mwenye nia mbaya, chuki na mwenye kuhukumu hata akinisema vizuri namna gani.

Maoni yako ni objective sana. Weaknesses noted brother

Kwa vile u msikivu, endelea kusikia ya wakubwa na wadogo. Usidharau mtu wala maoni yake, mwisho wa siku mwenye maamuzi ni wewe. Waase na wafuasi, wapenzi, washabiki na wanachama wa CHADEMA kufuata nyayo zako katika hili.
 
duh mimi Zitto namkubali sana ila ananitia hofu yuko kama anatumika/anaushirikiano na mafisadi . kikwete kakwepa kwenda jimboni kwake pinda kunawakati alimshauri akaze buti mjengoni atapasikia , kuna nini katikati yao????????????????????????:confused2:

Nimefanya kazi Kigoma Kaskazini, nimepiga mzigo wa nguvu. Pinda ilikuwa porojo za kisiasa. Kikwete simpangii ratiba mimi. Nani kakwambia kuwa harudi tena Kigoma? Hata dokta Slaa hajaenda majimbo yote, kanda majimbo ambayo tuna nguvu ya kushinda. Sasa unataka CCM wapoteze muda wao kwangu wakati watashika third place?
 
Pasco, you are right in some ways:

1. Nimependa sana ubunifu wa local campaigns. Ingawa zinahitaji pesa lakini pia kuwa na kile Zitto anachoita "Grass Root Movement" ni muhimu. Hiki ndich anachojaribu kama vile Obama alivyopewa support na MoveOn.org: Democracy in Action

2. Kitu ambacho kwa uhakika kimekosekana Chadema ni coordination ya kampeni. Nilikuwa nategemea hapa DSM ambapo ndiyo centre ya Media kuwe na daily Update ya kampeni zote kwa uzito Mkuu wakati wengine wako field. Zito in his own way so far amekuwa na updates nyingi katika media next to Slaa and may be Ndesamburo. Hata Mbowe hatumsikii kabisa. Kulikoni?

3. Binafsi niliwahi kutaka kuanza initiatives za kutaka CUF, CHADEMA na NCCR na UDP waungane. Aiseeee, huwezi amini ubinafsi unatawala vyama vyote. Zitto alikukuwa open minded kwa hilo. Nampongeza na amekuwa akilisema.

4. Zitto hawezi kugombea urais 2015 kwa kuwa atakuwa hajafikisha 40. Kwa nini alisema, I dont know. lakini kwangu mimi naona ni strategy ya kampeni. ukiangalia baada ya kusema vile Media yote waliipa kipaumbele the next day. Huu ni ubunifu.

5. Ila kimoja, Zitto ajifunze "Kwa pamoja Tutasonga Mbele" katika siasa za Kitanzania zenye kada za namna tofauti, zinahitaji uvumilivu wa hali ya juu. Hata kama wengi wanaweza kuelewa, bado maslahi binafsi pia yanatawala kuliko utaifa. wengine tumejifunza mengi katika uongozi.

Naomba kuwakilisha

On number 4 mark your words. There are so many misconceptions on this issue. I handle it with care. On the other way, it is campaigns. It is about BASE consolidation. Watu waelewe hili kama ulivyosema.
Watu wawe nje ya BOX maana kampeni ni mbinu za kushinda na kama mimi natafuta ushindi wa HESHIMA ie ushindi wa kuonyesha a BASE....!
 
Nimefanya kazi Kigoma Kaskazini, nimepiga mzigo wa nguvu. Pinda ilikuwa porojo za kisiasa. Kikwete simpangii ratiba mimi. Nani kakwambia kuwa harudi tena Kigoma? Hata dokta Slaa hajaenda majimbo yote, kanda majimbo ambayo tuna nguvu ya kushinda. Sasa unataka CCM wapoteze muda wao kwangu wakati watashika third place?

Mkuu Zitto,

Tafadhari ujitahidi pia kutenga muda wako na kuwasaidia wagombea wengine kwenye majimbo yenye uwezekano wa kushinda ili tuweze kuongeza idadi ya Wabunge wa upinzani.
 
Mkuu Zitto,

Tafadhari ujitahidi pia kutenga muda wako na kuwasaidia wagombea wengine kwenye majimbo yenye uwezekano wa kushinda ili tuweze kuongeza idadi ya Wabunge wa upinzani.
Kumbe na wewe unamfagilia Zitto? OMG
 
Back
Top Bottom