Nono
JF-Expert Member
- Feb 11, 2008
- 1,536
- 643
Kwanza kabisa, naunga naunga mkono waraka wa Kanisa (hakuna swali hapa).
Ila, kauli ya viongozi wa TUKTA inakatisha tamaa kiasi kikubwa na kuonyesha jinsi viongozi hawa wanavyojipenda wenyewe kuliko Watanzania na vizazi vijavyo. Iweje leo hii waone sababu ya kuandaa waraka baada ya kuambulia ongezeko la 4000 kwenye mishahara yao? Je, wafanyakazi wakiHONGWA hiyo 315,000 wataacha uchafu uendelee kama kawaida? Je, hi sio njia ya kutafuta nafasi ambayo wanashtuka leo kuwa waliachwa nje? Wako wapi siku zote kukemea maovu yote yanayoendelea? Hii nchi imekuwa ya makundi ya maslahi tu!
Ila, kauli ya viongozi wa TUKTA inakatisha tamaa kiasi kikubwa na kuonyesha jinsi viongozi hawa wanavyojipenda wenyewe kuliko Watanzania na vizazi vijavyo. Iweje leo hii waone sababu ya kuandaa waraka baada ya kuambulia ongezeko la 4000 kwenye mishahara yao? Je, wafanyakazi wakiHONGWA hiyo 315,000 wataacha uchafu uendelee kama kawaida? Je, hi sio njia ya kutafuta nafasi ambayo wanashtuka leo kuwa waliachwa nje? Wako wapi siku zote kukemea maovu yote yanayoendelea? Hii nchi imekuwa ya makundi ya maslahi tu!
TUCTA yaikamia CCM 2010
TAMKO lililotolewa na viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), huku wakitangaza kuunga mkono waraka wa Kanisa Katoliki, linahofiwa kuweza kukisambaratisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa uchaguzi mkuu mwakani, baada ya serikali kuongeza sh 4,410 kwenye mshahara wa kima cha chini.
……………………Huku akishangiliwa na wafanyakazi walioshiriki maandamano hayo, Mgaya alisema vyama vya wafanyakazi havikuhusishwa kuandaa ongezeko hilo kama yalivyo makubaliano ya TUCTA na serikali, bali limetolewa kinyemela, hatua aliyotahadharisha kuwa ni hatari, kwani inawagonganisha viongozi wa TUCTA na wafanyakazi.
………………..Alisema TUCTA inaitaka serikali ilipe sh 315, 000 kama kima cha chini kwa mwezi, vinginevyo hawataiunga mkono katika uchaguzi mkuu ujao.
……………………………………….."Tunapenda kuitahadharisha serikali kwamba kupuuza suala la mishahara ya wafanyakazi ni jambo la hatari sana na kwa vyovyote vile, litaigharimu kwenye uchaguzi mkuu mwakani," alisema.
…………………."Wafanyakazi wote tumeungana chini ya umoja wetu kudai haki kwa amani, hizo zote ni ishara za watu kuchoka, wanajua jinsi wakubwa wanavyoitafuna nchi kwa ufisadi, wananchi hao wakiungana na waraka wa Kanisa Katoliki, CCM imekwisha," alisema mfanyakazi, Musa wa mkoani hapa.
………………………."Sisi wafanyakazi ni waelewa na ni wasomi, endapo tutaamua kwa nguvu kusimamia msimamo wetu kuungana na waraka huo, itakuwa hatari kwa CCM, kwani inaweza kusambaratika, maana laana ya kuwadharau wafanyakazi itawatafuna," alisema.
Source: http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=8791