Katika chaguzi kuwe na muda wa kusikiliza malalamiko ya kabla mshindi hajaapishwa

YanguHaki

Senior Member
Oct 11, 2010
129
9
Kuondokana na maneno yanayoweza kutuvunjia amani katika taifa kama "tangazeni kisha wao wataenda mahakamani" tuliyoyasoma humu jamvini napendekeza kwenye chaguzi zote nchini matokeo ya uchaguzi yatangazwe kama kawaida lakini kuwe na chombo ambacho sio mahakama chenye mamlaka ya kusikiliza malalamiko ya wagombea. Kitengue ushindi kama kitajiridhisha kuwa kulikuwa na ukiukwaji wa sheria na kanuni za uchaguzi au kimthibitishe mshindi kama hakuna malalamiko yoyote. Hiki chombo kwanza kitasaidia kuondokana na gharama kwa serikali kuendesha kesi nyingine zisizo na kichwa wala miguu tunazozisikia kwenye vyombo vya habari. Mahakama ibakie kama chombo cha rufani kwa mlalamikaji na pia kesi isizidi miezi mitatu kumalizika toka kuapishwa kwa mbunge.
 
Kuondokana na maneno yanayoweza kutuvunjia amani katika taifa kama "tangazeni kisha wao wataenda mahakamani" tuliyoyasoma humu jamvini napendekeza kwenye chaguzi zote nchini matokeo ya uchaguzi yatangazwe kama kawaida lakini kuwe na chombo ambacho sio mahakama chenye mamlaka ya kusikiliza malalamiko ya wagombea. Kitengue ushindi kama kitajiridhisha kuwa kulikuwa na ukiukwaji wa sheria na kanuni za uchaguzi au kimthibitishe mshindi kama hakuna malalamiko yoyote. Hiki chombo kwanza kitasaidia kuondokana na gharama kwa serikali kuendesha kesi nyingine zisizo na kichwa wala miguu tunazozisikia kwenye vyombo vya habari. Mahakama ibakie kama chombo cha rufani kwa mlalamikaji na pia kesi isizidi miezi mitatu kumalizika toka kuapishwa kwa mbunge au diwani.
Kwa upande wa urais malalamiko yasikilizwe kabla hajaapishwa. Kuwe na muda usiopungua miezi miwili kwa ajili hiyo. Na wakati wote rais atakuwa mteule anasubiri hatma ya kesi ya malalamiko. Ni kituko kwa kiasi fulani na si rahisi kwa jaji ambaye mamlaka ya uteuzi wake ni rais kutenda haki akiletewa shauri kama hilo.
 
Back
Top Bottom