Katibu wa CHADEMA Kinondoni azua balaa kwenye kikao

Red one

Member
Apr 22, 2011
99
26
siku ya leo ndani ya wilaya ya kinondoni kulikuwa na kikao cha kamati ya ushauri cha wilaya yaani DCC, katika kikao hicho ambacho wajumbe wake nipamoja na vyama vya siasa waliyopo ndani ya wilaya husika.

kikao kilianza saa 9:30 asubuhi, kasheshe ilianza kwenye kupitisha agenda, ndipo alipo simama katibu wa chadema mkoa wa kinondoni bwana KILEWO, nanukuu maneno yake.

1. ndugu m/kiti kikao hiki kwa mujibu washeria nikikao batili mpaka sasa, kwanini nasema ni batili, nikwakuwa toka tulipo kutana hapa aprl mwaka jana ni mwaka mmoja na mwezi mmoja sasa, wakati kanuni na seria zinasema DCC ikutane mara 2 kwa mwaka.

2. nikwanini tunakaa DCC wakati tayari RCC imekwisha kukaa mara 2 mwaka huu yaani april na may? wakati kanuni na sheria zinasema DCC ndiyo inapswa kuiandaa RCC? huoni hapa tumekuja kupena posho na kuchekeana huku wananchi wetu wakiwa wanamambo ya msingi wakikosa fursa ya kusikilizwa?

3. DCC inapswa kukaa kabla ya baraza la bajeti la madiwani ili dcc ipendekeze mambo ya msingi yatakayo ingizwa kwenye vikao rasmi vya bajeti, maana hapa leo tutajadili bajeti ambayo imekwisha fanyiwa kazi na hatuwezi batilisha jambo lolote lile, mh m/kiti huu ni uvujanji mkubwa na matumizi mabaya ya fedha za wananchi wetu.

mimi ningependekeza kikao hiki kiahirishwe ilituondoke tusichukue hizi pesa za bure za wananchi wetu huu ni uhuni mnatufanyia. mwisho wa kunukuu.

majibu ya mkuu wa wilaya;
mbona mjumbe unaongea kwa jazba na huheshimu wakubwa zako? kilewo taarifa m/kiti futa kauli yako yakusema naonga kwa jazba kuheshimu wakubwa nataka ufahamu ukishakuwa kiongozi hakuna cha ukubwa au udogo, m/kiti kaachini> kilewo sikai nomba niishie hapo kwanza.
 
Muda wote huo mwenyekiti alikuwa wapi hajaitisha kikao? Huyo mwenyekiti anatikiwa apelekwe keko, hafai hata kidogo.
 
Chadema ni chama kilicho jaliwa viongozi makini kila idara, kwa hili nakupongeza kamanda KILEWO kwakusimamia kanuni na taratibu zilizo wekwa, ila mleta hoja hii hujatuambia kikao kiliendelea au kilivunjika kama alivyotaka kilewo.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
haya ndo mambo yanatakiwa wakubwa ndo nini?usipofuata sheria whether ni mkubwa ni mdogo mpana au vipi haihusu! alitakiwa ajibu hoja si kumuambia anaongea kwa jazba au kisa posho imetajwa ha ha ha
 
Chadema ni chama kilicho jaliwa viongozi makini kila idara, kwa hili nakupongeza kamanda KILEWO kwakusimamia kanuni na taratibu zilizo wekwa, ila mleta hoja hii hujatuambia kikao kiliendelea au kilivunjika kama alivyotaka kilewo.

mkuu kikao kiliendelea kwakutumia nguvu ya watumishi pale walipo piga kura wengi wakasema kiendelee ila iwe mwanzo na mwisho, ila KILEWO hakuvunjika moyo aliendeleza makombora makali na kukosekana majibu, makombora hayo nikama ifuatavyo
1. nikutaka manspaa kutoa taarifa ya tume ya lukuvi juu ya viwanja vya wazi, jibu. swala hilo lipo mahakamani.
2. kupatiwa taarifa juu ya soko la big brother, jibu tunaomba radhi kwakutoiweka taarifa hii kwenye agenda za kikao hiki.
3. kupatiwa mapato halali yanayo patikana kwa mwekezaji wa MLIMANI CIT, jibu hatuna data za kutosha kwakuwa mweka hazina hayupo.
4.tunapenda kufahamu miradi ya maji iliyopo ndani ya wilaya ya kinondoni, jibu. tuliwaomba idara ya maji wafike hapa leo ila hawajafika wao ndiyo wangekuwa na majibu sahihi , ila kwasisi hatuna majibu sahihi tutawaletea mirsdi hiyo kwenye kikao kijacho. hayo ndiyo aliyo uliza bwana kilewo ila yalikosa majibu, bravo MNYIKA kwakukuza jembe lingine kijana leo alikomaa nanafasi yako haikuonekana kupwaya
 
jaman kwenye JF inabid tuwaeleze viongoz wa sirikal nn maana ya kabla na baadae,hongera jk na semina teketeza mal za umma
 
mkuu kikao kiliendelea kwakutumia nguvu ya watumishi pale walipo piga kura wengi wakasema kiendelee ila iwe mwanzo na mwisho, ila KILEWO hakuvunjika moyo aliendeleza makombora makali na kukosekana majibu, makombora hayo nikama ifuatavyo
1. nikutaka manspaa kutoa taarifa ya tume ya lukuvi juu ya viwanja vya wazi, jibu. swala hilo lipo mahakamani.
2. kupatiwa taarifa juu ya soko la big brother, jibu tunaomba radhi kwakutoiweka taarifa hii kwenye agenda za kikao hiki.
3. kupatiwa mapato halali yanayo patikana kwa mwekezaji wa MLIMANI CIT, jibu hatuna data za kutosha kwakuwa mweka hazina hayupo.
4.tunapenda kufahamu miradi ya maji iliyopo ndani ya wilaya ya kinondoni, jibu. tuliwaomba idara ya maji wafike hapa leo ila hawajafika wao ndiyo wangekuwa na majibu sahihi , ila kwasisi hatuna majibu sahihi tutawaletea mirsdi hiyo kwenye kikao kijacho. hayo ndiyo aliyo uliza bwana kilewo ila yalikosa majibu, bravo MNYIKA kwakukuza jembe lingine kijana leo alikomaa nanafasi yako haikuonekana kupwaya


Kama hawana majibu ya haya maswali manne wameitisha kikao cha nini. Kupata vitafunwa?
Katiba mpay inakuja, tukumoshe kabisa hii tabia ya kuteuwa viongozi kama mkuu wa wilaya na mkoa. tena mkuu wa wilaya wa kazi gani? hawa watu wamekuwa kama mchwa. si mitaro ya kupitisha maji machafu, si taa za barabarani, na sasa wala hawajui ni miradi gani ya maji iko ndani ya eneo la kazi. Kwa hiyo huyu mkuu wa wilaya kila akiaga asubuhi familia yake kuwa anaenda kazi anafanya nini kama hata hana majibu kwa maswali manne tu?

No wonder this country is in a mess!
 
kwa maswali hayo yote yaliyo ulizwa na majibu kukosekana nidhahiri kwamba sasa serikali haina majibu kwenye maswala ya kijamii, serikali hiii sasa haina maana kwetu, bravo KILEWO
 
CHADEMA ni moto wa kuotea mbali. Wachana nao bwana. Wana viongozi wenye akili mno! sio majinga kama ccm!
 
Tuwekee majina ya Mwenyekiti wa hicho kikao tafadhali na wajumbe wengine kama inawezekana
Nampa bigup Kilewo,
 
Jana baada ya kikao nikiwa na wenzangu tulipata nafasi ya kuongea naye, nikijana asiye penda kuropoka nikijana mwenye busara sana kwenye mambo ya msingi. Nikataka kujua nini hatua zaidi atakazo chukua kwakuwa maswali yake yalikosa majibu.

Alinijibu hivi: sasa ndiyo nimeanza kutilia mashaka juu ya ulipaji wa kodi wa mwekezaji wapale mlimani, nitaanza kulifuatilia swala hili kwa karibu sana pamoja na wadau mbali mbali ilikubaini ukweli uliyopo pale,

Maana pale mtu mwenye kupangisha kwa nje hulipa si chini ya sh 7mil kwa mwezi( kama samaki samaki) nilikuwa natarajia majibu kama walivyokuwa wazi kwa mwekezaji wa pale kocoberch, ila wakashindwa so kuna kitu pale lazima tukijue
 
Corruption destroys guilty conciousness, Mitaa mingi bajet hata hazijapelekwa, kwa sababu ya viongozi wabovu wa CCM. They have to go out next election.:mod:
 
CDM wapo juu hakuna ubishi....inaelekea mkuu wa wilaya hajui hata maana ya collective responsibility, maana isingetakiwa aseme mweka hazina hayupo au dawasco hawapo alitakiwa kuwa na majibu yote.

CCM ni wahuni na wanafanya mambo yao kihusni ndio maana mambo km haya wanashindwa kujibu.

Bravo Kilewo
 
Hii ni hatua inayotia moyo sana...!
Kiongozi kama huyu akiwa eneo langu ni lazima nimchague bila kujali chama chake!

Akae sawa maana magamba wanaweza kumfuatilia huyu!
 
Mwenyekiti ni DC.......Kada wa CCM naturally

DC=Mwenyekiti wa Kikao= Bw. Jordan Rugimbana.


  1. Ni mmoja wa waanzilishi wa Kambi ya Vijana - UVIKIUTA iliyopo Chamazi. Kambi hiyo ilianzia kituo cha kulelea Watoto wa Mitaani Kanisa Katoliki Kurasini.
  2. Kada Mzuri wa CCM
  3. Alishawahi kuwa kiongozi wa mbio za mwenge baadaye Mkapa akampa UDC Mwanga. Alipata sifa ya kujenga shule nyingi za sekondari kata.
  4. Elimu yake ni Fomu Six ya Kujiendeleza.
 
Back
Top Bottom