Katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif aseme mwenyewe chama chake ni cha upinzani au tawala??

eliesikia

JF-Expert Member
Oct 29, 2010
787
755
Habari,
Katika hali ya kawaida kabisa inafahamika Katibu mkuu ndio msimamizi na msemaji mkuu wa chama. Lakini kwa CUF ni tofauti sana hasa wanapotoa kazi hii kwa naibu au mwenyekiti. Mi siijui katiba "vizuri" ya CUF lakini nimeona kwenye katiba yao hayo maelezo ndio yapo.

Kwa kuwa hivi karibuni chama cha CUF na CHADEMA wanagombana sana haswa kwenye swali la nani mtawala na nani ni mpinzani. Basi huu ni wakati muafaka kwa Katibu Mkuu Mhe. Maalim Seif kueleza umma kuwa chama chake ni cha mlengo gani na nia gani na nadhani mabishano yoote haya yataisha.

Pia, CUF wanasema CHADEMA ina "kebehi" serikali ya umoja wa kitaifa ya Zanzibar na kudai kuwa wanataka kuulazimisha UMMA uamini kuwa CUF na CCM ni anko na shangazi wote shuka moja. Lakini kiukweli anaujua huyu katibu mkuu ambaye ndiye msimamizi mkuu wa chama hiki na ndie mshiriki katika hii serikali. JuziJuzi alilalamika kazi za kichama zimekuwa nyingi na anataka msaidizi lakini nadhani kwenye maswala haya ya msingi ni wakati muafaka akajibu kwa umma kuwa wao CUF ni chama tawala au upinzani. Na jee serikali ya kitaifa ina maana gani kama si kushirikiana na CCM???!!

Hapa kuna "mkanganyiko" mkubwa wa mambo haswa:

1. Je wakiunda serikali kivuli pamoja na CHADEMA ni wabunge wapi waingie wale waliotoka kwenye serikali ya umoja Zanzibar au bara?

2. Je hao CUF wanatekeleza sera ipi na ilani ipi ya chama kipi katika serikali ya umoja wa kitaifa?

3. Je hao CHADEMA wakikubali kuungana na CUF ni sera au ilani ya chama gani watakubaliana kuifuata? Eg. CCM wanadai kilimo kwanza lakini CUF wao wanaweza wakataka elimu kwanza na CHADEMA wao wakataka ajira kwanza kwa wananchi. sasa ni sera gani wanaweza kuweka sawa maana naaamini sera ni kama dini ukiamini yabidi kufuata na kabla yahitaji kujitayarisha.

4. Je katika kutekeleza hayo yote CHADEMA hawakuwa na sera ya kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na yeyote hata kama wangeshinda uchaguzi? Kuna hasara na faida ya kufanya hivi. Moja yawezekana "PLANS" zako ukafanikiwa au usifanikiwe kwa hiyo hutaki kumwingiza mwenzako mkaangukia pua pamoja.


Baada ya hizo hoja za msingi na madalizo mbalimbali naamini Mhe. Maalim Seif mwanaCCM wa zamani na MwanaCUF kindakindaki akayaeleza kinaga ubaga ili ubishi woote uishe. Na CUF itakuwa huru kuchagua njia ipi ya kupita kuliko kurukia njia mbili "mtaka mawili moja humponyoka".

MYTAKE:
Mimi nimeona ukimya wa huyu bwana na wenzake kama mgombea mwenza wa Lipumba, Mhe. Duni waziri wa afya na wengine wanaoshiriki serikali ya Umoja wa kitaifa ndio yaliyoleta manung'uniko kwa CHADEMA kupelekea kuwashuku "vibaya" wenzao. Na bado naamini hii siri iliyojificha hapa ndio kisa chenyewe kwa kuwa CHADEMA wanaamini hawa jamaa ndio CUF halisi toka enzi ikianzishwa.


Baadae
Nawasilisha hoja
 
sikiliza kijana wabunge wa cuf au ccm kutoka zanzibar ni wapinzani ndani ya bunge la tanzania,,kwa sababu wao wanatetea maslahi ya zanzibar,sio kutetea maslahi ya chama kama wanavyojitetea chadema,ufahamu kuwa bunge la tanzania siku zote ni against na zanzibar,kuna mabo ambayo sio ya muungano na kuyafanya ya muungano wanayaleta zanzibar,kuna mambo ya muungano wanatayafanya kuwa sio ya muungano.

Kwa hiyo siku zote chama cha cuf kipo kutetea maslahi ya wanachi hata kama kipo madarakani,unapoongea cuf nakujua unaongelea upande wote yaani zanzibar na tanganyika,lakini ufahamu tanganyika wana sera zao na zanzbar kwa cuf wana sera zao,tena tofauti na ndio maana ukaona ndani ya bunge bado wabunge wetu ni wapinzani,na utaendelea kuwepo kutokana wao wanatetea maslahi yetu,,,,

Muungano kwetu ni jinamizi,,,,
 
HAMAD RASHID-GOGORO, CUF-MASLAHI NA CCM-UFISADI MJUE FIKA USALAMA WA NCHI YETU UNAYUMBISHWA NA 'MUAFAKA WA MASLAHI BINAFSI' YA VYEO NA KUJIUNGA KULE NA NGURUWE KULA MABUA NA UFISADI
ULIOKITHIRI NCHINI


Jamani kuna uwezekano Wa-Tanzania tukawa na tofauti nyingi tu nchini zikiwemo zile za kitamaduni, kiimani, kijinsia na kadhalika lakini matatizo yanayotuhatarishia amani nchini, Wakristo kwa Waislmu na kote Bara na Visiwani ni zile zile!!

Nasema matatizo ya kusisitizwa tu AMANI na kufichwa kule kwa HAKI kwa raia ni chanzo cha matatizo kibao yanayotukaba kila siku nchini kama vile: (1) UFISADI uliokithiri ndani ya serikali ya CCM yatuathiri sote, (2) Muafaka wa CUF kujiunga na CCM kula mabua kwa pamoja na kuwaacha wananchi solemba kwenye umasikini wa kutupwa ni letu sote.

Kama haitoshi, pia (3) Utaratibu wa Serikali ya Muungano usiona tija, na fursa sawa wa moja kwa moja kwa mwananchi wa kawaida, (4) ukosefu wa ajira, (5) elimu duni, (6) Maisha kupanda gharama kila kukicha ni letu sote hivyo kwa hali ya kawaida kabisa Mtanzania hahitaji KAMPENI ZA KUTIANA HOFU pale tunapojiunga kama taifa kujikomboa kwa kudai haki zaidi na Katiba Mpya nchini!!!

... hatuwe kujua vizuri; wenzetu wa CCM na CUF waulizwe vizuri juu ya hilo jambo wanaloliona peke yao tu hapa nchini kuhusu usalama kutetereshwa ambalo sisi wengine hatulion.

Lakini kama kudai HAKI SAWA NA MASLAHI KWA UMMA wa Tanzania ndicho hasa kile kinachowakosesha amani wale MAFISADI walioko serikalini na kuitwa KUHATARISHA USALAMA WA NCHI na basi CHADEMA kazeni mwendo mdundo kwa sana tu.

Wa-Tanzania tunaakili sana kote Bara na Visiwani na pia tunafahamu fika kwamba wale wanaoingia muafakaka na serikali ya CCM gizani kwa maslahi binafsi ya kupata vyeo, mijumba, na mashamba ndio hasa wanaoHATARISHA USALAMA WA NCHI YETU.

Ndugu zetu akina Hamad Rashid, CUF-Maslahi na CCM-Ufisadi, acheni mara moja kuchezea akili za Mtanzania wa leo kote Bara na Visiwani tunasema kwamba Hatudanganyiki wala Hatugawanyiki kwenye Kutafuta Maslahi yetu kama Umma wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Maalim Seif bado ni mpinzani. Cheo chake hakimo kwenye KATIBA ya JMT.

Wanasema wamefanya mabadiliko kwenye katiba ya Zanzibar, ambayo utekelezaji wake umeenza kabla ya kuingizwa kwenye katiba ya Jamuhuri. Katiba ya zanzibar inatakiwa iwe ndani ya Katiba ya jamuhuri....., sijui ilikuwajekuwaje?
 
sikiliza kijana wabunge wa cuf au ccm kutoka zanzibar ni wapinzani ndani ya bunge la tanzania,,kwa sababu wao wanatetea maslahi ya zanzibar,sio kutetea maslahi ya chama kama wanavyojitetea chadema,ufahamu kuwa bunge la tanzania siku zote ni against na zanzibar,kuna mabo ambayo sio ya muungano na kuyafanya ya muungano wanayaleta zanzibar,kuna mambo ya muungano wanatayafanya kuwa sio ya muungano.

Kauli zako hazina mashiko wala usajili...Nasikitika mtu kama ww ukiongea pumba nyingi kuliko kukoboa.... Tafadhali fuatilia kabla ya ku-comment... Unasema CCM wapinzani wakati wao pia ni mawaziri kama mwinyi, Nahodha na wameshika wizara nyeti... Acha kupumbaza wenye akili utachekwa...!! Kwa maana ingine CCM na CUF toka zanzibar lao moja si ndio??? tunza kauli
 
Back
Top Bottom