tatanyengo
JF-Expert Member
- Mar 30, 2011
- 1,134
- 280
Katiba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) ya mwaka 1984 (Toleo la 2010) katika Kifungu cha 19 (1) inasema:
Kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo, wa imani na wa uchaguzi katika mambo ya dini, pamoja na uhuru wa kubadilisha dini au imani yake.
Kifungu kidogo cha (2) kinasema: Bila kuathiri sheria zinazohusika na kazi ya kutangaza dini na kueneza dini itakuwa huru na jambo la hiyari ya mtu binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.
Kama hivyo ndivyo:
1. Kwa nini Waumini wa dini nyingine (wasio waislamu) huko Zanzibar kwanini wanalazimishwa kuwa na mfungo wa Ramadhan kinyume na imani zao?
2. Kwanini kiongozi wa serikali (SMZ) ahimize kwamba wale wote wataokwenda kinyume na matakwa ya mfungo atachukuliwa hatua za "KISHERIA?"
Kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo, wa imani na wa uchaguzi katika mambo ya dini, pamoja na uhuru wa kubadilisha dini au imani yake.
Kifungu kidogo cha (2) kinasema: Bila kuathiri sheria zinazohusika na kazi ya kutangaza dini na kueneza dini itakuwa huru na jambo la hiyari ya mtu binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.
Kama hivyo ndivyo:
1. Kwa nini Waumini wa dini nyingine (wasio waislamu) huko Zanzibar kwanini wanalazimishwa kuwa na mfungo wa Ramadhan kinyume na imani zao?
2. Kwanini kiongozi wa serikali (SMZ) ahimize kwamba wale wote wataokwenda kinyume na matakwa ya mfungo atachukuliwa hatua za "KISHERIA?"