Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,462
- 39,929
Mabadiliko ya Katiba yafanyike ili yamnufaishe nani? Je mabadiliko mnayopendekeza kufanyika, nani atanufaika zaidi CCM au Wapinzani? Utaona kuwa hakuna mtu ambaye atafanya mabadiliko ambayo yatamwondolea ulaji, kumpunguzia ujiko, na kumfanya akose nafasi fulani za kutanua!! Ni kwa sababu hiyo, basi ombi la kufanya mabadiliko ya Katiba litaendelea kuwa sawa na kumpigia mbuzi gitaa, kwani hata iwe ni Pase posa.. mbuzi hachezi!!! Ataendelea kula majani, na kuendelea kunya!!!
Ninachotaka kusema ni kuwa, kutegemea na kuombea kuwa serikali ya CCM italeta mabadiliko Bungeni ili kuweka mazingira ambayo Wapinzani watanufaika ni kujidanganya!!! Haitatokea, na itabakia kuwa ni ndoto ya Alinacha!! Sasa sizungumzii kama ipo haya ya kufanya mabadiliko ya Katiba, kwani najua ipo, na mapendekezo mnayoyasema ni miongoni mwa mambo muhimu. Binafsi, sioni haja ya kufanyika kwa mabadiliko viraka ya Katiba, haja iliyopo ni ya kuandika Katiba mpya kabisa, ambayo itaondoa utata, mgongano, na kutokueleweka kwa namna yoyote ile. Katiba hiyo itazingitai historia yetu, baada ya karibu miaka 50 ya uhuru na mang'amuzi ya nchi nyingine juu ya masuala mbalimbali ya kisheria. Katiba tuliyo nayo sasa imetufaa kwa muda huu tangu uhuru (na muungano) lakini ilikuwa iwe ya mpito, na wakati umefika kwa Taifa kuwa na Katiba mpya. Hata hivyo, mabadiliko tunayoyazungumzia au hata uandikaji mpya wa Katiba unakosa nguvu ukizingatia kuwa hivi karibuni tutaingia kwenye Shirikisho la Afriya ya Mashariki.
Kwa sababu hiyo, nguvu zote zielekezwe kwenye Katiba ya Shirikisho hilo kwani kwa huko tunakokwenda hiyo ndiyo itakuwa na nguvu zaidi na matokeo zaidi katika maisha ya watu wa Afrika ya Mashariki.
Hata hivyo, kama kuna kitu wapinzani wanaweza kufanya ili angalau sheria kadhaa zibadilishwe ni kwa wao kuungana na kuwa chama kimoja chenye nguvu, na kwa kufanya hivyo wanaweza kupata viti vingi Bungeni na kusababisha mabadiliko ya kisheria wanayolalamikia!!! Hiyo ndiyo njia nyepesi zaidi.
Kutegemea wema na huruma ya CCM katika kuwaletea mabadiliko, wapinzani wanajidanganya (Sikiliza mada niliyozungumzia hilo kwenye archives za KLH News)!!!
Ninachotaka kusema ni kuwa, kutegemea na kuombea kuwa serikali ya CCM italeta mabadiliko Bungeni ili kuweka mazingira ambayo Wapinzani watanufaika ni kujidanganya!!! Haitatokea, na itabakia kuwa ni ndoto ya Alinacha!! Sasa sizungumzii kama ipo haya ya kufanya mabadiliko ya Katiba, kwani najua ipo, na mapendekezo mnayoyasema ni miongoni mwa mambo muhimu. Binafsi, sioni haja ya kufanyika kwa mabadiliko viraka ya Katiba, haja iliyopo ni ya kuandika Katiba mpya kabisa, ambayo itaondoa utata, mgongano, na kutokueleweka kwa namna yoyote ile. Katiba hiyo itazingitai historia yetu, baada ya karibu miaka 50 ya uhuru na mang'amuzi ya nchi nyingine juu ya masuala mbalimbali ya kisheria. Katiba tuliyo nayo sasa imetufaa kwa muda huu tangu uhuru (na muungano) lakini ilikuwa iwe ya mpito, na wakati umefika kwa Taifa kuwa na Katiba mpya. Hata hivyo, mabadiliko tunayoyazungumzia au hata uandikaji mpya wa Katiba unakosa nguvu ukizingatia kuwa hivi karibuni tutaingia kwenye Shirikisho la Afriya ya Mashariki.
Kwa sababu hiyo, nguvu zote zielekezwe kwenye Katiba ya Shirikisho hilo kwani kwa huko tunakokwenda hiyo ndiyo itakuwa na nguvu zaidi na matokeo zaidi katika maisha ya watu wa Afrika ya Mashariki.
Hata hivyo, kama kuna kitu wapinzani wanaweza kufanya ili angalau sheria kadhaa zibadilishwe ni kwa wao kuungana na kuwa chama kimoja chenye nguvu, na kwa kufanya hivyo wanaweza kupata viti vingi Bungeni na kusababisha mabadiliko ya kisheria wanayolalamikia!!! Hiyo ndiyo njia nyepesi zaidi.
Kutegemea wema na huruma ya CCM katika kuwaletea mabadiliko, wapinzani wanajidanganya (Sikiliza mada niliyozungumzia hilo kwenye archives za KLH News)!!!