nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
MWENYEKITI wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila, amewataka Watanzania kuunda katiba mpya itakayotambua serikali ya Tanganyika iliyokufa baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964.
Akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya ofisi za chama hicho, zilizoko Ilala Mchikichini, Mtikila alisema uhuru wa Tanganyika wa Desemba 9 mwaka 1961 uliporwa na Muungano uliovunja serikali ya Tanganyika na kuiacha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Wito huo wa Mtikila nakuja siku kadhaa baada ya Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, kupitisha marekebisho ya katiba ya Zanzibar, inayompa mamlaka Rais wa Zanzibar kugawa mipaka ya visiwa hivyo bila kushauriana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwa mujibu wa Mtikila mabadiliko hayo yamevunja rasmi muungano na kwamba sasa ni wakati wa Watanganyika kutafuta upya uhuru wao.
"Hatimaye Wazanzibari wamejirudishia rasmi utaifa wao, kwa kurejesha rasmi hadhi yao kikatiba kwamba wao ni nchi kamili. Watanganyika wamebaki wakia wameduwaa," alisema Mtikila.
Alisema Muungano huo, haukuhusiana na mikakati ya Umoja wa Afrika uliopiganiwa na aliyekuwa Rais wa Ghana Kwame Nkrumah na waasisi wengine wa uhuru wa Afrika.
Alidai kuwa Muungano wa Tanzania, uliundwa ili kulinda maslahi ya taifa la Marekani katika kilele cha vita baridi dhidi ya dola la mwisho.
Akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya ofisi za chama hicho, zilizoko Ilala Mchikichini, Mtikila alisema uhuru wa Tanganyika wa Desemba 9 mwaka 1961 uliporwa na Muungano uliovunja serikali ya Tanganyika na kuiacha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Wito huo wa Mtikila nakuja siku kadhaa baada ya Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, kupitisha marekebisho ya katiba ya Zanzibar, inayompa mamlaka Rais wa Zanzibar kugawa mipaka ya visiwa hivyo bila kushauriana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwa mujibu wa Mtikila mabadiliko hayo yamevunja rasmi muungano na kwamba sasa ni wakati wa Watanganyika kutafuta upya uhuru wao.
"Hatimaye Wazanzibari wamejirudishia rasmi utaifa wao, kwa kurejesha rasmi hadhi yao kikatiba kwamba wao ni nchi kamili. Watanganyika wamebaki wakia wameduwaa," alisema Mtikila.
Alisema Muungano huo, haukuhusiana na mikakati ya Umoja wa Afrika uliopiganiwa na aliyekuwa Rais wa Ghana Kwame Nkrumah na waasisi wengine wa uhuru wa Afrika.
Alidai kuwa Muungano wa Tanzania, uliundwa ili kulinda maslahi ya taifa la Marekani katika kilele cha vita baridi dhidi ya dola la mwisho.