Katiba Mpya: CHADEMA msikubali mkutano wenu na JK kuhusisha vyama vingine, hasa CUF

Rais Kikwete una kazi kubwa mbele yako. Uwe makini katika hili. Soma alama za nyakati.
 
Watanzania Tuwe wazalendo kwa Nchi yetu. Kwa nia njema, CUF wasi husishwe katika mkutano huo, watalaamu wa sheria ambao pia wamo katika Kamati ya Katiba Hasa Felix Mkosamali ( mb) NCCR MAGEUZI wahusishwe kwani walionekana kupinga mswaada huu mbovu tangu kwenye kamati na Hata kutoka Bungeni.
 
Busara zaidi zitumike katika swala zima la mchakato wa kupta ktiba mpya, kwa sababu hakuna Chama chenye Hati miliki ya Katiba Mpya. Katiba mpya ni mali ya watanzania waleo, kesho, na vizazi vijavyo.
 
Can't agree more! |Hata mimi nashangazwa na unafiki huu wa CCM
Kikwete inabidi ajielevate na kujijengea heshima kwa kutokubaliana na uppuzi huu. makundi yanayokwalify kunana na kikwete ni yale yaliyopinga mchakato tangu awali yakiwa ni chadema, nccr- mageuzi, wale majaji wastaafu na lile Jukwaa la Katiba.
Hawa wengine wanataka kuigiza cinema za kinigeria tu
 
mimi naona chadema waachWe wakamuone kama ombilao lilivyo kuwa,arafu pendekezo la ccm lifuate maana wenyewe wanataka kuleta marumbano kama ya bungeni ya kuunga hoja mkono.kuna umuhimu baada ya chadema labda pointi muhimu wale wote waliokuwa wanapinga ndo waunde kamati ya pamoja ikiwa ni ya vyama vya siasa,asasi za kiraia,jukwaa la katiba,wasomi na viongozi wa dini ndo iwe hawamu yapuili kumuona rais

Chedema inaongoza
Peoples power!!!!!!!!!!!!!!!!!!!1
 
Hili ni kosa na kiufundi kabisa liliagizwa na NEC ya CCM eti mkutano ujumuishe vyama vyote vyenye uwakilishi bungeni. WHAT FOR? Na hii inaonyesha dhahili za udhaifu wa CCM ktk kutoa maamuzi. Hawataki kusumbua bongo zao ili wajue nini maana ya mkutano. Mkutano wowote lazima uwe na agenda za kujadiliwa na lazima wahusika wote wawe na hizo agenda kabla ya mkutano. Agenda za DCM ziko wazi na zishatumwa kwa rais na labda ndizo zilizomshawishi akutane nao na zimejengwa na main objective ya kutokukubali mchakato wa kuelekea katiba mpya ulivyofanywa kwa kusoma mara ya pili muswada ambao hauwahi kusomwa mara ya kwanza. Hili liko wazi hata kama CCM, CUF, TLP, UDP wanalikataa. Hoja ya DCM siyo ya vyama vingine kiasi kwamba kutaka kuwachanganya hawa kutaishia kuleta fujo sio kupigana lakini kutoleana vijembe maana vyama vingine vimeamua ku succumb to CCM lies and manipulations na kupuuza Watanzania ktk ujumla wetu huku tukiongozwa na CDM, Wanaharakati, wanataaluma, majaji wastaafu, wafanyakazi, wakulima na chama cha wanasheria wa Tanzania.

Agenda za CDM ziheshimiwe na kama rais atataka kukutana na vyama vyote apange mkutano mwingine na CCM wawepo because all signs reveal they opposition party in waiting
 
Zaidi ya CDM hakuna chama kingine chochote kilichoomba kukutana na JK. Leo hii inakuwaje vilazimishiwe kwenda kuonana nae wakati hawakuwa hata wameandaa ajenda ambayo ingehitaji msaada wa JK! Kweli CCM ni Janga la Kitaifa.

Kwani CCM wanahitaji kuomba kibali cha kuonana na JK? Si wanaye kila siku? Aliyesimamia hayo maamuzi ya hicho kikao ni nani? Mwenyekiti wa vikao vyote huko Dodoma ni JK, sasa wanayetaka kumwona ni JK yupi? Hapo ndo sarakasi inapoanzia!!!
 
Naunga mkono uamuzi wa Raisi kukutana na CMD. Ushauri wa CC ya CCM kwamba akutane na vyama vingine ni kuvuruga nia nzuri ya kuleta maridhiano. Hatutaki Ikulu kugeuka sehemu ya kuvuta ni kuvute. Vyama vingine kuwepo ni dhahiri mkutano hautakwenda salama bila kuvunjika. Tunamwomba Raisi awasikilize hoja za CMD, na baadaye endapo vyama vingine vitaomba pia, anaweza kuwasikiliza pia. Mazungumzo yawe ya utulivu, busara na amani.

Mungu Ibariki Tanzania
 
CHADEMA kama chama walikaa kama cc ndo waliomba kukutana na amri jeshi mkuu, hawajaomba kama kambi ya upinzani bungeni, so yatakuwa maajabu tena ya musa wa kale endapo usanii wa nape kuwajumuisha cuf-ccmB, tlp, nccr, udp na hata wale wasokuwa na wabunge ...........utafikiriwa na jk!
 
Hivi hoja walizonazo CHADEMA kukutana na JK ndio hoja za hivyo vyama vingine CCM wanaoshinikiza wahusishwe?

Hii michezo ya Kitoto CCM wanayofanya ishapitwa na wakati kama CCM wanataka na hivyo vyama vingine vishiriki pamoja waombe miadi na JK na sio kukurupuka eti kisa CDM... CCM wasipotumia busara huu mchakato katiba mpya itakuwa vurugu tupu..
Hii ya CCM ni sawa na kumuona jamaa anaelekea Ubungo ukamfuata wakati wewe ulikuwa huna mpango wa kwenda huko. Chadema ina sababu zake wanapinga mswada kusainiwa sasa CCM au CUF watakwenda na hoja gani, kama hoja yao ni kupinga sawa waunganishe hoja waende pamoja lakini kama wana hoja tofauti na Chadema waombe siku nyingine wakutane na rais hawakatazwi. Hii ni sawa na fujo za kisiasa, halafu toka lini CCM akawa masemaji wa vyama vingine?
 
Chonde chonde viongozi wa Chadema – katika mkutano wenu na JK kuhusu Katiba mpya, kamwe msikubali ujumuishe vyama vingine kama ilivyopendekezwa na Kamati Kuu ya CCM (CC) kwa Rais Kikwete.

Ni vyema kila chama kikakutana na JK peke yake.

Hofu yangu ni kwamba pendekezo hili limetolewa ili kumsaidia JK kukabiliana na hoja za viongozi wa Chadema wtakaokwenda kukutana naye. Wajumbe wa CUF watakaokwenda, ambacho ni chama mshiriki wa CCM huko Zanzibar, wanaweza kuvuruga mkutano huo ukiwa wa pamoja na Chadema ikaonekana haina hoja.

Nasema hivyo kwa sababu tayari CCM inaonekana kuufanya Muungano kuwa ni mtaji wake mkubwa wa kisiasa katika suala la Katiba mpya kwa kuwapa Zanzibar uwakilishi sawa jambo ambalo CDM inalipinga kwa sababu ya kutokuwap pia kwa serikali ya "Tanganyika" katika Muungano.

Ingekuwapo serikali hiyo ya Tanganyika, uwakilishi wa namna hiyo ungekubalika na CDM.

Msifanye makosa CDM kujijumlisha na vyama vingine katika mkutano na JK – na hasa CUF – maana hawa CUF wako zaidi kwa masilahi ya Zanzibar na CCM.

Natoa tahadhari.

Wameogopa mpaka wakampeleka jamaa tuition, lakini haitasaidia, na wala haitabadilisha kitu chochote, wanajua anakwenda kukutana na watalaam wanaojua ni kwa nini Tanzania ni masikini na sio kukaa hapo Dodoma kupiga umbea na kusengenyana. Kama jamaa hatakuwa na majibu ya kuridhisha atawakatisha tamaa wafuasi wake wengi hata akina rejea humu nao wanaweza kukimbia ID zao. Sio chadema tu wamechukizwa na ubabe wa ccm kupitisha huo muswada wa katiba hata ccm wenyewe hawakurizishwa, wanasema hata maoni yao yatasaidia kwa sababu ni watanzania wote wanajenga Tanzania sio kwenda kutumbua kodi za wananchi hapo Dodoma.
 
IIe ya kukutana, mwenyeji (JK) akaamua kuwa na wageni wake wengine wowote kuwalaki wageni wake rasmi Chadema!. Hao wageni wengine wanaweza kuwa CUF, NCCR Mageuzi, UDP na TLP!.
Mkuu katika hayo majadiliano kuna pande mbili tu,moja ni ya CDM na nyingine ni JK na hao 'wageni', wake bila hivyo CDM ni bora wafikirie strategy nyingine hiyo ya kukukutana nae waachane nayo..
 
Vyama vingine havikatazwi kuonana na Rais bali wafanye kwa wakati wao, CDM imebeba ukweli kuhusu sheria ya marekebisho
ya Katiba, kuelekea mchakato wa Katiba mpya pamoja na Muungano. Na ndio sababu Nec ya Ccm wanataka kufunika na
kuvuruga mazungumzo kwa kuwatumia Cuf, Nccr-Mageuzi Mrema pamoja na Dovutwa.
Kilichopo ni kwamba ni CDM ndio walioomba kuongea na Rais wa Tanzania na sio Mwenyekiti wa Ccm Taifa. Chochote kitakacho-
fanyika kinyume cha hapo zitakuwa ni njama za kuvuruga mazungumzo. Zaidi ya hapo ni woga wa Nec ya Ccm kutaka kuyafu-
nika yale ya ukweli ambayo yaliyostahili kufanyika katika kupitisha marekebisho ya Katiba.
 
Kama suala ni kujadili katiba kwa nini vyama vyote visikutane pamoja kuliko kwenda kimojakimoja? acheni ubaguzi, THIS IS NOT A ONE MAN SHOW!
Vingine vimeshajadili na kupitisha maoni yao sasa viende kufanya nini wakati vilikubali kusoma muswada kwa mara ya pili ikimaanisha kuwa haviitaji mjadala zaidi. Hapo ni wabunge wa NCCR na chama cha Chadema. NCCR bado kama chama hakieleweki maana mpaka sasa hamna msimamo wa wazi wa chama, hata kutoka walitoka kwa utashi wa mtu mmoja mmoja sio chama mwanzoni walitoka wabunge wote wa chadema na wawili wa nccr kafulila na mkosamali. machali na yule mwanamke walibaki mpaka kesho yake waliposoma upepo.
 
Watanzania Tuwe wazalendo kwa Nchi yetu. Kwa nia njema, CUF wasi husishwe katika mkutano huo, watalaamu wa sheria ambao pia wamo katika Kamati ya Katiba Hasa Felix Mkosamali ( mb) NCCR MAGEUZI wahusishwe kwani walionekana kupinga mswaada huu mbovu tangu kwenye kamati na Hata kutoka Bungeni.
Well said, lakini kuhusu mkosamali nadhani asiwe pekeyake maana nccr wote walipinga bila kificho kwa hiyo wana sababu ya kuonana na rais. kama watatakiwa kuwakilishwa basi wanaweza wakamchagua yeyote kati yao wanne.
 
Back
Top Bottom