Katiba ikibadilishwa, mtasingizia nini tena?

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,786

Kwa maana leo hii ukimuuliza Mbongo kwa nini nchi yake masikini unapata jibu haraka Katiba mbovu, kwanini watoto hawasomi jibu Katiba mbovu, kwa nini mafisadi wanaitafuna nchi jibu Katiba mbovu, kwa nini UKIMWI unamaliza watu jibu Katiba mbovu, kwa nini ajali zinamaliza watu jibu Katiba mbovu yaani kila kitu jibu lake ni Katiba mbovu!

Sasa swali langu mkipata hiyo katiba mnayoitaka, mtakuja na singo gani nyingine ya kusingizia?
Najua lazima mtaipata kwa maana historia yetu inatuonyesha hivyo kwamba kila wkt tulikuwa tunatafuta kisingizio cha kushindwa kwetu kuendelea kama jamii nyingine Duniani.

Tulianza na utumwa kwamba watu wetu wenye nguvu waliuzwa utumwani hivyo tukakosa watu wa kufanya kazi ndiyo maana tukawa masikini, ikaja Ukoloni Wazungu walitunyonya wakatuibia kwa kutusainisha mikataba ya kilaghai ndiyo maana tukawa masikini, tukapata Uhuru ikaja Wazungu wanatuibia kwa kutumia Ukoloni mamboleo ndiyo maana tumebakia kuwa masikini, ikaja Globalization wakulima wetu wanashindwa kushindana kwa sababu Wazungu wanasubsidies Wakulima wao ndiyo maana tumebakia masikini!

Sasa hiyo singo imeisha na tumepata nyingine ya Katiba kwamba tuna Katiba mbovu ndiyo maana tumebakia masikini ikumbukwe kwamba hii Katiba inayoitwa mbovu inatumika jamii nyingi Duniani kama Uchina, Singapore, Vietnam, ilitumika kujenga Korea Kusini, ikajenga Taiwan, ikaendeleza Ujerumani, Japan, Uingereza, Chile, Afrika Kusini lkn kwetu imeshindwa,

Sasa swali langu Je hiyo mpya italeta miujiza gani kama kwa miaka zaidi ya 200 ingawaje tuliyoyapitia wengine wameyapitia pia kama Ukoloni, Utumwa, Katiba mbovu lkn leo hii wako mbele sana kiuchumi!
 
Wanapoteza muda mwingi kwenye suala la katiba. Halafu wanataka kujenga hoja kuwa katiba ndio kila kitu. Mambo makubwa kiuchumi ambayo Kagame kayafanya Rwanda hayana uhusiano wowote ule na katiba mbovu. Alipoingia madarakani akajenga nidhamu katika kila sekta. Tanzania wajuaji wanapinga kila kitu, wakiambiwa wawahi ofisini wanaanzisha mada za dharau wakati nchini Ghana rais mwenyewe anaamka mapema na kwenda kusimama kwenye milango ya wizara, ili kukagua nani anawahi na nani anachelewa, hapo hakuna suala la katiba ya Ghana ni nidhamu tu. Tanzania tunataka tuishi kwa mtindo wa kwetu wenyewe wa maisha halafu tunataka matokeo mazuri kama wenzetu!. Maendeleo ya Singapore, Thailand na nchi zote za Asia yanatokana na watu kukubali kuongozwa na nidhamu ya hali ya juu. Watanzania tunataka tule bata halafu tupige hatua za kimaendeleo. Halafu wale wenye kufaidika na masuala ya uanaharakati, wanakuwa wa kwanza kuipigania katiba mpya. Katiba ina msaada gani ikiwa watu ni wavivu wenye kujua sana kulalamika na kujenga hoja za kujifanya wanajua kila kitu.
 
Inategemea ni katiba ipi,ya Warioba au Chenge? Rasimu ya Warioba ni sawa,lakini kama ni ile ya Chenge,wa kulaumiwa ni Magufuli.
 
Wanapoteza muda mwingi kwenye suala la katiba. Halafu wanataka kujenga hoja kuwa katiba ndio kila kitu. Mambo makubwa kiuchumi ambayo Kagame kayafanya Rwanda hayana uhusiano wowote ule na katiba mbovu. Alipoingia madarakani akajenga nidhamu katika kila sekta. Tanzania wajuaji wanapinga kila kitu, wakiambiwa wawahi ofisini wanaanzisha mada za dharau wakati nchini Ghana rais mwenyewe anaamka mapema na kwenda kusimama kwenye milango ya wizara, ili kukagua nani anawahi na nani anachelewa, hapo hakuna suala la katiba ya Ghana ni nidhamu tu. Tanzania tunataka tuishi kwa mtindo wa kwetu wenyewe wa maisha halafu tunataka matokeo mazuri kama wenzetu!. Maendeleo ya Singapore, Thailand na nchi zote za Asia yanatokana na watu kukubali kuongozwa na nidhamu ya hali ya juu. Watanzania tunataka tule bata halafu tupige hatua za kimaendeleo. Halafu wale wenye kufaidika na masuala ya uanaharakati, wanakuwa wa kwanza kuipigania katiba mpya. Katiba ina msaada gani ikiwa watu ni wavivu wenye kujua sana kulalamika na kujenga hoja za kujifanya wanajua kila kitu.
Unayoyasema ni kweli tupu, lakini yote hayo yamewezekana sababu ya kuwa na mkuu wa nchi mzuri. Ubovu wa katiba unaonekana zaidi kama mkipata rais boya, asiye mzalendo, asiye jali maslahi ya nchi, anayetumia vibaya madaraka aliyopewa na katiba.

Enzi ya Nyerere watu wengi hawakuona ubovu wa katiba sababu Nyerere alikuwa mzalendo kwa taifa letu. Awamu ya Magufuli tunaweza pia tusione ubovu wa katiba sababu pia naye ni mzalendo kama Nyerere. Awamu ya mkwre watu wamelalamika sana sababu mkwere alikuwa hajali maslahi ya taifa. Nadhani unakumbuka teuzi zake za mwisho mwisho hapa, yaani kila mtu aliona wazi ni kupeana ulaji hakuna lingine. Nadhani unakumbuka wale wabunge 2 walioteuliwa miezi 2 bunge likavunjwa na wakala kiinua mgongo. Nadhani unakumbuka teuzi zake za wakuu wa wilaya. Nadhani unakumbuka frequency za safari zake za nje na msululu wa watu aliokuwa anaenda nao. Haya ni matukio machache yanaoonyesha dhahiri katiba yetu imempa madaraka makubwa sana Rais. He can do whatever he wants, at any time.

  1. Tunahitaji katiba mpya ili imbane Rais asitumie vibaya madaraka yake, hilo tuu!! Kwa Magufuli katiba yo yote kwake ni sawa tu coz ni mzalendo na si mpigaji, ila akiondoka akaingia mwingine ambaye si mzalendo, kwa katiba hii tutalia tena kama ilivyokuwa kwa mkwere
 
Wa tanganyika kazi tunayo, kwa mada ya huyu ndugu tusali sana, hadi humu wapo, una anzisha mada kumbe haujitambui, baba Magufuri waone washauri wetu inauma vumiliatu miaka mitano wata kusoma. Kila la kheri mheshimiwa raisi wetu. I submit.
 
We Barbarosa, kama kweli huoni ubaya wa katiba tulionayo, na unadiriki kufananisha katiba ya Ujerumani na yetu (wao wana majimbo kwa mfano. Huku majimbo CCMscrow walisema ni ukanda/ukabila) basi kazi tunayo kubwa sana hadi tupige hatua za kweli.

Labda unamaanisha katiba ya iliyokua Ujerumani Mashariki. Jiulize iko wapi leo hii.

Lakini kuhusu nidhamu ya kazi na maisha nakubaliana na wewe wengi tunakosa.

Na hiyo inatokana na Rais kuwa na madaraka makubwa na kutoshtakiwa baada ya uongozi. Mwinyi aliruhusu watu wakabweteka sana na hatuna cha kumfanya. Of coz alifanya mengi pia mazuri sikatai.

So, katiba ni lazima. Iweke mambo ambayo rais hawezi amua kubadili tu bila consent mpya ya watu.

Ona elimu kila siku inapigwa danadana. Huwezi kuwa na jamii inayoheshimu kazi ilhali walifaulishwa bila kufanya kazi wajue kusoma, kuandika na kuhesabu vizuri. Na hakuna wa kuadhibiwa ili iwe fundisho.

Mkapa na Kikwete kwa hili la elimu walitakiwa waadhibiwe vikali kabisa. Huyu anafuta michezo shule, huyu anapanua magoli kila mtu afunge.

Lakini angalia ufisadi. Huyu anajiuzia mgodi wa makaa ya mawe Kiwira wakati huyu anajiuzia kipande cha nchi Loliondogate kwa waarabu wanabeba twiga kwenye ndege.

Lakini funika ni huyu aliyeamua kutengeneza mabilionea kwa pesa za BoT, Escrow, kukwepa kodi, madawa kulevya, n.k. Na huna cha kuwaadhibia ili kuleta nidhamu kwa viongozi. Ukumbuke wao ndio mfano.

mito kasema vema. Bila kudhibiti raisi, mengine ni bure. Kama taifa hatuwezi kutegemea utashi tu wa aliepo madarakani.

Au umeleta mada kwa ushabiki, au una ajenda tofauti na ulochokifafanua. Katiba kwa sasa ni suluhisho kubwa sana.
 
Kwa maana leo hii ukimuuliza Mbongo kwa nini nchi yake masikini unapata jibu haraka Katiba mbovu, kwanini watoto hawasomi jibu Katiba mbovu, kwa nini mafisadi wanaitafuna nchi jibu Katiba mbovu, kwa nini UKIMWI unamaliza watu jibu Katiba mbovu, kwa nini ajali zinamaliza watu jibu Katiba mbovu yaani kila kitu jibu lake ni Katiba mbovu!

Mkuu,

Watoto wanasoma isipokuwa hawapati elimu iliyo bora bali wanapata bora elimu. Angalia shule zetu sisi walalahoi ni kwamba watoto wanasoma katika mazingira magumu sana na walimu wanafundisha katika mazingira magumu sana. Hivyo katiba tunayoilalamikia ni kwamba suala la elimu halijapewa kipaumbele yaani imetengeneza mazingira ya kuleana kiasi kwamba mwenye nacho anasoma shule ya elimu bora na asiyenacho anasoma shule ya bora elimu.

Push up 2.jpg


Primary School TZ.jpg


Shule 2.jpg
Shule 2.jpg


Shule 1.jpg



Suala la ajali pia ni matatizo ambayo yapo kwa sababu ya sheria zetu mbovu. Rushwa imetawala katika usimamiaji wa sheria na hakuna wa kuwajibika kutokana na kuleana katika taasisi husika. Barabara ni mbovu ambazo pia ni chanzo cha ajali pia. Kutokana na mfumo mbovu hakuna wa kuwawajibisha makandarasi wanaojengfa chini ya kiwango, na hii ni kutokana na rushwa katika utoaji wa tenda za ujenzi.

Road Mbovu.jpg



Mafisadi wanaitafuna nchi ni kutokana na katiba mbovu ambayo inawalinda. Mtu anafanya kosa la ubadhirifu lakini analindwa na viongozi wa juu, hii ni kuonyesha kuwa mfumo wa uongozi mbaya na katiba inashindwa kuwawajibisha hata huyu kiongozi wa juu ambaye anatetea uovu huo.

Mfano kesi ya ESCROW ipo wazi na ushahidi unaonekana lakini anaibuka kiongozi wa juu na kutetea kuwa siyo kosa. Wale waliochukua pesa benki ya Stanbic hadi leo hawajulikani na pia waliojulikana wa benki ya Mkombozi kesi yao ni kimya imezimwa na kiongozi wa juu. Wananchi tunapata hisia kuwa huenda na huyu kiongozi wa juu anayetetea naye yupo katika mgao wa ESCROW. Na kwa kuwa katiba haina meno ya kumuwajibisha kiongozi ndio imetoka hiyo!!!!!!!!!!

Escow.jpg


Escrow IPTL 02.jpg


Escrow IPTL 03.jpg


Escrow IPTL 04.jpg




Escrow Utata 01.jpg
 
Mkuu,

Watoto wanasoma isipokuwa hawapati elimu iliyo bora bali wanapata bora elimu. Angalia shule zetu sisi walalahoi ni kwamba watoto wanasoma katika mazingira magumu sana na walimu wanafundisha katika mazingira magumu sana. Hivyo katiba tunayoilalamikia ni kwamba suala la elimu halijapewa kipaumbele yaani imetengeneza mazingira ya kuleana kiasi kwamba mwenye nacho anasoma shule ya elimu bora na asiyenacho anasoma shule ya bora elimu.

View attachment 318441

View attachment 318442

View attachment 318443 View attachment 318443

View attachment 318444


Suala la ajali pia ni matatizo ambayo yapo kwa sababu ya sheria zetu mbovu. Rushwa imetawala katika usimamiaji wa sheria na hakuna wa kuwajibika kutokana na kuleana katika taasisi husika. Barabara ni mbovu ambazo pia ni chanzo cha ajali pia. Kutokana na mfumo mbovu hakuna wa kuwawajibisha makandarasi wanaojengfa chini ya kiwango, na hii ni kutokana na rushwa katika utoaji wa tenda za ujenzi.

View attachment 318451


Mafisadi wanaitafuna nchi ni kutokana na katiba mbovu ambayo inawalinda. Mtu anafanya kosa la ubadhirifu lakini analindwa na viongozi wa juu, hii ni kuonyesha kuwa mfumo wa uongozi mbaya na katiba inashindwa kuwawajibisha hata huyu kiongozi wa juu ambaye anatetea uovu huo.

Mfano kesi ya ESCROW ipo wazi na ushahidi unaonekana lakini anaibuka kiongozi wa juu na kutetea kuwa siyo kosa. Wale waliochukua pesa benki ya Stanbic hadi leo hawajulikani na pia waliojulikana wa benki ya Mkombozi kesi yao ni kimya imezimwa na kingozi wa juu. N kwa kuwa katiba haina meno ya kumuwajibisha kiongozi ndio imetoka hiyo!!!!!!!!!!

View attachment 318452

View attachment 318453

View attachment 318454

View attachment 318455



View attachment 318457



Na ndiyo hoja yangu ilipojikita hapo, Je tukipata hiyo inayoitwa Katiba Mpya itabadilisha yote hayo? Yaani ni miujiza gani itatokea kwa maana nijuavyo mimi Katiba ni karatasi iliyoandikwa mambo ambayo yanapaswa kufwatwa lkn wanaopaswa kuifwata hiyo Katiba ni Binadamu yaani sisi Watz sasa hayo maandishi yatabadilisha hulka na desturi yetu iliyojikita mizizi kwa vizazi hadi vizazi?


Kwa maana hata hii tuliyonayo pia imekataza mambo mengi sana lkn Je tunayafwata? Huko mbali turudi kwenye Katiba ya vyama vyetu, Je uteuzi wa fisadi Lowasa na Sumaye ulifwata Katiba ya chadema? Kwa maana nijuavyo mimi Lowasa aliingia chadema ndani ya mda mchache akapewa kugombea Uraisi kinyume na Katiba ya chadema kama alivyosema Katibu Mkuu wa chadema Slaa sasa kama hapa tumekiuka Katiba tuliyojiwekea ili kukidhi haja fulani iweje hiyo Katiba mpya iwe tofauti?

Kumbuka Katiba ni karatsi tu iliyoandikwa na inahitaji binadamu kuyafwata na kuyatii yale yaliyoandikwa na mpaka leo hii hakuna ushahidi kwenye jamii yetu kwamba hilo linawezekana sasa hiyo miujiza itatoka wapi?
 

Na ndiyo hoja yangu ilipojikita hapo, Je tukipata hiyo inayoitwa Katiba Mpya itabadilisha yote hayo? Yaani ni miujiza gani itatokea kwa maana nijuavyo mimi Katiba ni karatasi iliyoandikwa mambo ambayo yanapaswa kufwatwa lkn wanaopaswa kuifwata hiyo Katiba ni Binadamu yaani sisi Watz sasa hayo maandishi yatabadilisha hulka na desturi yetu iliyojikita mizizi kwa vizazi hadi vizazi?


Kwa maana hata hii tuliyonayo pia imekataza mambo mengi sana lkn Je tunayafwata? Huko mbali turudi kwenye Katiba ya vyama vyetu, Je uteuzi wa fisadi Lowasa na Sumaye ulifwata Katiba ya chadema? Kwa maana nijuavyo mimi Lowasa aliingia chadema ndani ya mda mchache akapewa kugombea Uraisi kinyume na Katiba ya chadema kama alivyosema Katibu Mkuu wa chadema Slaa sasa kama hapa tumekiuka Katiba tuliyojiwekea ili kukidhi haja fulani iweje hiyo Katiba mpya iwe tofauti?

Kumbuka Katiba ni karatsi tu iliyoandikwa na inahitaji binadamu kuyafwata na kuyatii yale yaliyoandikwa na mpaka leo hii hakuna ushahidi kwenye jamii yetu kwamba hilo linawezekana sasa hiyo miujiza itatoka wapi?

KWanza uelewe kuwa tunapaswa kuwana katiba yenye meno ya kuwawajibisha waliotenda uovu. Tuna uwezo wa kuwasomesha watoto wetu wakapata Elimu bora, walimu wakapata maslahi stahiki, mazingira mazuri ya kufundishia. Kwa nchi ya Tanzania inawezekana lakini inakuwa ngumu kutokana na katiba ya kuleana ambayo haina meno. Hii ilitengenezwa mwaka 1977 kipindi ambacho hakukuwa na changamoto nyingi za kimaisha tofauti na leo.

Endapo kama vingozi wetu wanaona kuwa hii iliyopo haiwabebi kwa nini wanakataa kuibadilisha baadhi ya vipengele kama jinsi wananchi tunavyotaka???? Ni kwamba wanajua vile vipengele tunavyohitaji vitawabana watashindwa kula. Watoto wa wenye nacho (hasa viongozi) wanasoma shule za private ambazo mimi siwezi hata kulipa ada ya mwezi mmoja kwa kipato changu cha mwezi. Wetu wanasoma shule za bora elimu.

Push up 2.jpg


Shule 1.jpg


Shule 2.jpg



Kuhusu suala la Lowasa kupewa nafasi ya kugombea, naomba niwekee hapa kipengele cha katiba ya Chadema kinachosema kuhusu muda wa mtu kuwa mwanachama na kufikia kupewa nafasi ya kugombea cheo chochote ndani ya chama. Ili nielewe na mimi.
 
katiba ni muhimu yote yanayofanyika sasa mabovu yawe tanzania bara au visiwani yanafanyika kwa ubovu wa katiba tulionayo ,muundo na vipengele vilivyopendekezwa na jaji wa warioba tunaita maoni ya wananchi yasipuuzwe .taifa endelevu lina katiba nzuri yenye miongozo mizuri .tunachopaswa kufanya nii baada ya kupata katiba mpya ni uweledi ya kufuata yale yaliyomo ndani ya katiba hiyo na utii wa sheria na uwepo wa mahakama ya katiba kwa ajili ya kutoa tasfsir sahihi kwa vifungu vyenye migongano .na pia uwepo wa rasilimali watu walioshiriki kwa namna moja au nyingine kwenye katiba hawa ni hazina kwa ajili ya kutoa mihadhara kwenye vyuo vikuu nchini na nje ya tanzania.
 
KWanza uelewe kuwa tunapaswa kuwana katiba yenye meno ya kuwawajibisha waliotenda uovu. Tuna uwezo wa kuwasomesha watoto wetu wakapata Elimu bora, walimu wakapata maslahi stahiki, mazingira mazuri ya kufundishia. Kwa nchi ya Tanzania inawezekana lakini inakuwa ngumu kutokana na katiba ya kuleana ambayo haina meno. Hii ilitengenezwa mwaka 1977 kipindi ambacho hakukuwa na changamoto nyingi za kimaisha tofauti na leo.

Endapo kama vingozi wetu wanaona kuwa hii iliyopo haiwabebi kwa nini wanakataa kuibadilisha baadhi ya vipengele kama jinsi wananchi tunavyotaka???? Ni kwamba wanajua vile vipengele tunavyohitaji vitawabana watashindwa kula. Watoto wa wenye nacho (hasa viongozi) wanasoma shule za private ambazo mimi siwezi hata kulipa ada ya mwezi mmoja kwa kipato changu cha mwezi. Wetu wanasoma shule za bora elimu.

View attachment 318468

View attachment 318469

View attachment 318470


Kuhusu suala la Lowasa kupewa nafasi ya kugombea, naomba niwekee hapa kipengele cha katiba ya Chadema kinachosema kuhusu muda wa mtu kuwa mwanachama na kufikia kupewa nafasi ya kugombea cheo chochote ndani ya chama. Ili nielewe na mimi.



Tofauti yangu na wewe ipo hapa!
Wewe unaamini kwamba matatizo tuliyonayo yanasabishwa na ubovu wa Katiba, wakati mimi napinga kwani matatizo yetu mengi yanasababishwa na Utamaduni wetu sisi na Katiba mpya haiwezi kubadilisha kitu TanZania!


Ngoja nikuulize swali dogo sana kama unafikiri hii Katiba ndiyo imeleta Umaskini TanZania, na Je Mbona Wazungu waliongoza hii nchi kwa kutumia Katiba hii hii? Mbona Wazungu (Waingereza ) wamejenga Australia na New Zealnd kwa kutumia Katiba kama hii ya kwetu yaani Malkia/Mfalme wa Uingeraza alikuwa anateua Gavana anamtuma Australia /New Zealand kama vile kwetu kulikuwa na Wakuu wa province waliokuwa wanateuliwa na Malkia ktk Uingereza moja kwa moja na wao walikuwa wanamwakilisha Malkia/Mfalme moja kwa moja kama vile kwetu Raisi wa JMTZ mbona leo hii Australia ni nchi iliyoendelea?

Singapore mpaka leo hii wanatumia katiba kama yetu mbona imetoka nchi masikini miaka ya 60' mpka nchi ya 4 kwa Utajiri Duniani leo hii na bado wanatumia Katiba kama yetu, kama tatizo letu lingekuwa Katiba basi leo hii Australia, New Zealand, Singapore, Taiwani, Korea Kusini wangekuwa masikini kama sisi kwa maana wanatumia au walitumia Katiba kama yetu tena wengine mbaya zaidi kwa maana kama Singapore madaraka ya Mkuu wa nchi ni makubwa kama ya wa kwetu tu!
 
Tofauti yangu na wewe ipo hapa!
Wewe unaamini kwamba matatizo tuliyonayo yanasabishwa na ubovu wa Katiba, wakati mimi napinga kwani matatizo yetu mengi yanasababishwa na Utamaduni wetu sisi na Katiba mpya haiwezi kubadilisha kitu TanZania!


Ngoja nikuulize swali dogo sana kama unafikiri hii Katiba ndiyo imeleta Umaskini TanZania, na Je Mbona Wazungu waliongoza hii nchi kwa kutumia Katiba hii hii? Mbona Wazungu (Waingereza ) wamejenga Australia na New Zealnd kwa kutumia Katiba kama hii ya kwetu yaani Malkia/Mfalme wa Uingeraza alikuwa anateua Gavana anamtuma Australia /New Zealand kama vile kwetu kulikuwa na Wakuu wa province waliokuwa wanateuliwa na Malkia ktk Uingereza moja kwa moja na wao walikuwa wanamwakilisha Malkia/Mfalme moja kwa moja kama vile kwetu Raisi wa JMTZ mbona leo hii Australia ni nchi iliyoendelea?

Singapore mpaka leo hii wanatumia katiba kama yetu mbona imetoka nchi masikini miaka ya 60' mpka nchi ya 4 kwa Utajiri Duniani leo hii na bado wanatumia Katiba kama yetu, kama tatizo letu lingekuwa Katiba basi leo hii Australia, New Zealand, Singapore, Taiwani, Korea Kusini wangekuwa masikini kama sisi kwa maana wanatumia au walitumia Katiba kama yetu tena wengine mbaya zaidi kwa maana kama Singapore madaraka ya Mkuu wa nchi ni makubwa kama ya wa kwetu tu!

Kwanza kabisa hii katiba tunajua ilitengenezwa mwaka 1977. kabla ya hapa Bara kulikuwa na katiba ya TANU na upande wa Visiwani kulikuwa na ya ASP. Hivyo Wazungu unaosema kama walitumia hii, kumbe ndio maana wazungu walitutawala kimabavu na kututesa. Na sasa ndani ya miaka 52 ya Uhuru ebdapo kama tunatumia ya kikoloni ndio maana hali zetu hazibadiliki na wachache kama ilivyo kuwa enzi za ukoloni watoto wao wanasoma na kupata elimu bora na sisi watawaliwa Watanganyika watoto wetu wanasoma na kupata bora elimu. kwa hili upo sahihi kumbe kama na wazungu walitumia hii.

Kama wazungu walitumia hii kumbe ndio maana Rasilimiali zetu zinasafirishwa na kupelekwa nje ya nchi kama ilivyokuwa enzi za ukoloni.

Twiga atoroshwa.jpg


Twiga.jpg



Na pia ndio maana katika kampeni tulikuwa tunaimba wimbo wa kutaka MABADILIKO ili tutoke katika kuitwa nchi masikini na ikiwa nchi yetu ni tajiri kwa kila kitu kuliko hizo nchi za Ulaya.

Pia ina maana unakubaliana na mimi kabisa kuwa mfumo wetu wa uongozi ni mbovu ndio maana hatuutaki. na bila kubadilisha katiba hakuna mabadiliko yatakayo patikana Tanzania hata miaka 200 ijayo hayapatikani. kwani mfumo ni ule ule hakuna jipya.

Endapo kama Katiba ya sasa ni nzuri kama wao wanavyosema lakini sisi wananchi hatuitaki kwanini viongozi wa CCM wanaing'ang'ania??? Ni kwa sababu inawanufaisha na kulinda masilahi yao kitu ambacho kinatuumiza sisi wananchi tulio wengi.

Viongozi Tanzania hawafiki laki tano lakini Wananchi tupo zaidi ya mil 40. KWa nini wasikubali wapendekezo yetu tulio wengi na wanalazimisha ya kwao?????
 
Kwanza kabisa hii katiba tunajua ilitengenezwa mwaka 1977. kabla ya hapa Bara kulikuwa na katiba ya TANU na upande wa Visiwani kulikuwa na ya ASP. Hivyo Wazungu unaosema kama walitumia hii, kumbe ndio maana wazungu walitutawala kimabavu na kututesa. Na sasa ndani ya miaka 52 ya Uhuru ebdapo kama tunatumia ya kikoloni ndio maana hali zetu hazibadiliki na wachache kama ilivyo kuwa enzi za ukoloni watoto wao wanasoma na kupata elimu bora na sisi watawaliwa Watanganyika watoto wetu wanasoma na kupata bora elimu. kwa hili upo sahihi kumbe kama na wazungu walitumia hii.

Kama wazungu walitumia hii kumbe ndio maana Rasilimiali zetu zinasafirishwa na kupelekwa nje ya je kama ilivyokuwa enzi za ukoloni.

View attachment 318484

View attachment 318485


Na pia ndio maana katika kampeni tulikuwa tunaimba wimbo wa kutaka MABADILIKO ili tutoke katika kuitwa nchi masikini na ikiwa nchi yetu ni tajiri kwa kila kitu kuliko hizo nchi za Ulaya.

Pia ina maana unakubaliana na mimi kabisa kuwa mfumo wetu wa uongozi ni mbovu ndio maana hatuutaki. na bila kubadilisha katiba hakuna mabadiliko yatakayo patikana Tanzania hata miaka 200 ijayo hayapatikani. kwani mfumo ni ule ule hakuna jipya.

Endapo kama Katiba ya sasa ni nzuri kama wao wanavyosema lakini sisi wananchi hatuitaki kwanini viongozi wa CCM wanaing'ang'ania??? Ni kwa sababu inawanufaisha na kulinda masilahi yao kitu ambacho kinatuumiza sisi wananchi tulio wengi.

Viongozi Tanzania hawafiki laki tano lakini Wananchi tupo zaidi ya mil 40. KWa nini wasikubali wapendekezo yetu tulio wengi na wanalazimisha ya kwao?????


Nimekuuliza swali dogo, kama unafikiri sisi hatujaendela kwa sababu ya Ubovu wa Katiba, Je ni kwa nini nchi ambazo zinatumia Katiba kama hii yetu zimeendelea? Nchi kama Singapore, Uchina, Vietnam hapo mwanzo Korea Kusini, Japani, Taiwan n.k!

Nijibu hapo tu, yaani iweje Katiba mbovu iendeleze wengine lkn kwetu ishindwe? Na kama tukibadilisha hiyo miujiza itatokea wapi?
 
Wanapoteza muda mwingi kwenye suala la katiba. Halafu wanataka kujenga hoja kuwa katiba ndio kila kitu. Mambo makubwa kiuchumi ambayo Kagame kayafanya Rwanda hayana uhusiano wowote ule na katiba mbovu. Alipoingia madarakani akajenga nidhamu katika kila sekta. Tanzania wajuaji wanapinga kila kitu, wakiambiwa wawahi ofisini wanaanzisha mada za dharau wakati nchini Ghana rais mwenyewe anaamka mapema na kwenda kusimama kwenye milango ya wizara, ili kukagua nani anawahi na nani anachelewa, hapo hakuna suala la katiba ya Ghana ni nidhamu tu. Tanzania tunataka tuishi kwa mtindo wa kwetu wenyewe wa maisha halafu tunataka matokeo mazuri kama wenzetu!. Maendeleo ya Singapore, Thailand na nchi zote za Asia yanatokana na watu kukubali kuongozwa na nidhamu ya hali ya juu. Watanzania tunataka tule bata halafu tupige hatua za kimaendeleo. Halafu wale wenye kufaidika na masuala ya uanaharakati, wanakuwa wa kwanza kuipigania katiba mpya. Katiba ina msaada gani ikiwa watu ni wavivu wenye kujua sana kulalamika na kujenga hoja za kujifanya wanajua kila kitu.
Kama wewe na mwanzisha mada mnadhani watu wanaodai katiba mpya wanadhani ikipatikana basi kila kitu kitaenda bila mkwamo mna mawazo finyu kabisa! Katiba nzuri ni sehemu ndogo ya mambo mengi yanaweza kufanya serikali iwajibike zaidi na kuleta maendeleo zaidi. Huwezi kutegemea katiba nzuri tu halafu uwe mvivu na mzembe kama ulivyokuwa utawala wa Kikwete na utegemee maendeleo. Kama unashindwa kuelewa chukua mfano huu: Maendeleo ya nchi ni kama mwili wa mwanadamu... unahitaji lishe za aina zote + mazoezi ili uwe kwenye afya njema. Huwezi kuunyima kwa mfano protein (katiba) halafu utegemee afya nzuri. Lakini vilevile protein peke yake tu (katiba) haitaufanya uwe mwili bora kiafya.
 
Unayoyasema ni kweli tupu, lakini yote hayo yamewezekana sababu ya kuwa na mkuu wa nchi mzuri. Ubovu wa katiba unaonekana zaidi kama mkipata rais boya, asiye mzalendo, asiye jali maslahi ya nchi, anayetumia vibaya madaraka aliyopewa na katiba.

Enzi ya Nyerere watu wengi hawakuona ubovu wa katiba sababu Nyerere alikuwa mzalendo kwa taifa letu. Awamu ya Magufuli tunaweza pia tusione ubovu wa katiba sababu pia naye ni mzalendo kama Nyerere. Awamu ya mkwre watu wamelalamika sana sababu mkwere alikuwa hajali maslahi ya taifa. Nadhani unakumbuka teuzi zake za mwisho mwisho hapa, yaani kila mtu aliona wazi ni kupeana ulaji hakuna lingine. Nadhani unakumbuka wale wabunge 2 walioteuliwa miezi 2 bunge likavunjwa na wakala kiinua mgongo. Nadhani unakumbuka teuzi zake za wakuu wa wilaya. Nadhani unakumbuka frequency za safari zake za nje na msululu wa watu aliokuwa anaenda nao. Haya ni matukio machache yanaoonyesha dhahiri katiba yetu imempa madaraka makubwa sana Rais. He can do whatever he wants, at any time.

  1. Tunahitaji katiba mpya ili imbane Rais asitumie vibaya madaraka yake, hilo tuu!! Kwa Magufuli katiba yo yote kwake ni sawa tu coz ni mzalendo na si mpigaji, ila akiondoka akaingia mwingine ambaye si mzalendo, kwa katiba hii tutalia tena kama ilivyokuwa kwa mkwere
Kila rais wa Tanzania anaonekana mwizi, alipoondoka Mwinyi madarakani watu wakasema ndugu zake wa karibu wanafanya biashara chafu. Mkapa naye alipoondoka watu wakaongea sana. Kikwete kaondoka watu wanaongea sana. Magufuli akiondoka naye hatakuwa salama. Hatujawahi kuwa na shukrani kwa viongozi wetu hata kidogo. Huu ni udhaifu wa bara zima la Afrika na sio sisi tu, hivyo sishangai kuwa sababu ya msingi ya mabadiliko ya katiba inayoiona wewe ni kumthibiti rais tu. Hiyo sababu haina nguvu ya kimantiki. Rais ni taasisi yenye majukumu mengi, anaweza kiongozi akawa msafi lakini kazungukwa na wezi. Tuwahurumie marais wetu, tunawabebesha mzigo mkubwa sana wa lawama, tunajenga negative image ya cheo cha urais kitu ambacho sio cha kiungwana.
 
Kama wewe na mwanzisha mada mnadhani watu wanaodai katiba mpya wanadhani ikipatikana basi kila kitu kitaenda bila mkwamo mna mawazo finyu kabisa! Katiba nzuri ni sehemu ndogo ya mambo mengi yanaweza kufanya serikali iwajibike zaidi na kuleta maendeleo zaidi. Huwezi kutegemea katiba nzuri tu halafu uwe mvivu na mzembe kama ulivyokuwa utawala wa Kikwete na utegemee maendeleo. Kama unashindwa kuelewa chukua mfano huu: Maendeleo ya nchi ni kama mwili wa mwanadamu... unahitaji lishe za aina zote + mazoezi ili uwe kwenye afya njema. Huwezi kuunyima kwa mfano protein (katiba) halafu utegemee afya nzuri. Lakini vilevile protein peke yake tu (katiba) haitaufanya uwe mwili bora kiafya.



Haujaelewa hasa ninachommanisha, kama tatizo ni Katiba mbaya, ni kwa nini nchi ambazo zinatumia Katiba kama yetu zimeendelea, tena sana Tu?
 
Wanapoteza muda mwingi kwenye suala la katiba. Halafu wanataka kujenga hoja kuwa katiba ndio kila kitu. Mambo makubwa kiuchumi ambayo Kagame kayafanya Rwanda hayana uhusiano wowote ule na katiba mbovu. Alipoingia madarakani akajenga nidhamu katika kila sekta. Tanzania wajuaji wanapinga kila kitu, wakiambiwa wawahi ofisini wanaanzisha mada za dharau wakati nchini Ghana rais mwenyewe anaamka mapema na kwenda kusimama kwenye milango ya wizara, ili kukagua nani anawahi na nani anachelewa, hapo hakuna suala la katiba ya Ghana ni nidhamu tu. Tanzania tunataka tuishi kwa mtindo wa kwetu wenyewe wa maisha halafu tunataka matokeo mazuri kama wenzetu!. Maendeleo ya Singapore, Thailand na nchi zote za Asia yanatokana na watu kukubali kuongozwa na nidhamu ya hali ya juu. Watanzania tunataka tule bata halafu tupige hatua za kimaendeleo. Halafu wale wenye kufaidika na masuala ya uanaharakati, wanakuwa wa kwanza kuipigania katiba mpya. Katiba ina msaada gani ikiwa watu ni wavivu wenye kujua sana kulalamika na kujenga hoja za kujifanya wanajua kila kitu.
Ujue sisi uelewa wetu mdogo sana. Kama katiba ingempa nguvu mwananchi basi viongozi wa nchi wangeogopa kuleta unyumbu maana wangeogopa kupewa adhabu na raia. Alafu si Kila anayeingia madarakani ni mzalendo, wengine wanaenda kujinufaisha wao na jamaa zao. Kama tutakua Na katiba yenye kumpa raia wa kawaida, heshima itakuwepo kwenye uongozi. Ndio maana tulishuhudia madudu kwenye secta nyingi lakini tulishindwa kufanya maamuzi kwakua hatuna nguvu kikatiba. Leo hii jecha kafuta uchaguzi na matokeo yake zanzibar kwa sababu ya katiba. Sasa mnashindwaje kuelewa umuhimu wa katiba? Au ndo tuseme nyie ni Ccm kindakindaki
 
Ujue sisi uelewa wetu mdogo sana. Kama katiba ingempa nguvu mwananchi basi viongozi wa nchi wangeogopa kuleta unyumbu maana wangeogopa kupewa adhabu na raia. Alafu si Kila anayeingia madarakani ni mzalendo, wengine wanaenda kujinufaisha wao na jamaa zao. Kama tutakua Na katiba yenye kumpa raia wa kawaida, heshima itakuwepo kwenye uongozi. Ndio maana tulishuhudia madudu kwenye secta nyingi lakini tulishindwa kufanya maamuzi kwakua hatuna nguvu kikatiba. Leo hii jecha kafuta uchaguzi na matokeo yake zanzibar kwa sababu ya katiba. Sasa mnashindwaje kuelewa umuhimu wa katiba? Au ndo tuseme nyie ni Ccm kindakindaki



Tatizo lenu ni kwamba mnafikiri Katiba ni mashine ambayo unabonyeza kitufe basi inafanya abc, HAPANA!
Katiba ni Karatasi yenye maandishi ambayo unayasoma na inahitaji binadamu sasa kuyatii na kuyafanya yale yalioandikwa kwende hiyo karatasi, na sasa hapo ndipo tatizo lilipo huyo Binadamu atakaye tii na kufwata hayo maandishi kwenye karatasi atatokea wapi? Ni huyu huyu yaani tuliyeopo hata TanZania au atatokea Mars?
 

Tatizo lenu ni kwamba mnafikiri Katiba ni mashine ambayo unabonyeza kitufe basi inafanya abc, HAPANA!
Katiba ni Karatasi yenye maandishi ambayo unayasoma na inahitaji binadamu sasa kuyatii na kuyafanya yale yalioandikwa kwende hiyo karatasi, na sasa hapo ndipo tatizo lilipo huyo Binadamu atakaye tii na kufwata hayo maandishi kwenye karatasi atatokea wapi? Ni huyu huyu yaani tuliyeopo hata TanZania au atatokea Mars?
Nimekuelewa mkuu. Uelewa wetu unatofautiana. Tuwaachie wanasiasa wafanya yao. Unyumbu wetu utatuponza
 
Back
Top Bottom