Katika katiba ijayo wananchi wapewe haki ya kumiliki ardhi na kuitumia kama mtaji wa kujipatia hisa katika uwekezaji pale wawekezaji wanapotaka kuitumia ardhi hiyo. Hii itawawezesha wananchi kuwa na kipato endelevu inayotokana na ardhi yao waliyopewa na Mungu badala ya mtindo wa sasa ambapo serikali inachukua ardhi na wananchi hupewa fiidia kidogo sana kiasi kwamba wanashindwa kujiendeleza kimaisha hali inafanya wananchi waone uwekezaji kwenye ardhi kuwa kero kwao kwa kuwa hawaoni faida yake.