KATIBA: Askofu Ruzoka amlima barua Waziri

Tatizo hapa si waziri, ambaye ana act kama Kasuku wa ku-echo yale yanayotolewa na bosi wake. Waziri wa katiba kwenye serikali ya ki -authoritarian ya CCM ni mtu mdogo sana aliyewekwa ili apate KULA huku akilinda masilahi ya mabwana zake.

Source kuu ya upupu huu ni CCM na kamati kuu yake ikiongozwa na genge la wapora mali za nchi ya (CC) ambao kwao hawa Tanzania kuwa na system iliyo free from political influence ni kuhatarisha masilahi yao (wao huita ya chama). CCM haina nia wala dhamira ya dhati ya kupata katiba mpya iliyotokana na wananchi bali wanavyotaka kufanya sasa ni kuirubuni jumiya ya kimataifa na wananchi ili ionekane kuwa kuna mabadiliko yametokana na wananchi na kuihalalishia CCM kuendelea michezo michafu wakati wa chaguzi na kuendelea kuwaamulia watanzania nani awaongoze hata kama hawamtaki. Katiba mpya iliyotokana na wananchi ni mwanzo wa mwisho wa viongozi wasiowajibika kwa wananchi na CCM 99% yao ni mfano.

Rejea kauli ya Mkapa - Si vema mabadiliko ya katiba yakaongozwa na wapinzani, serikali lazima ifikirie namna ya kubadili katiba, mantiki ya kauli kama hizi zimeanza kuonekana kwenye miswada ya kidikteta kama huu. Bila shinikizo kutoka kwa wananchi kwa style ya barua kama hizi na umma kusimama imara, CCM hawata na hawapo tayari kufanya lolote litakaloonekana ni kutishia ustawi wao wa kidikteta waliouzoea.

And sad enough ni kuwa kila kete ikikataa watavuruga mchezo. People need to get prepared for gud or for worse hawa watu wanalinda maslahi yao zaidi kuliko maslahi ya taifa ila raia wakikomaa basi jumuia ya kimataifa itawapa tough. Nashukuru baraza la maaskofu kupitia hiyo Idara kwa msimamo wao huo maana mpaka hapo wamesha twist mchezo mpaka wakajipange tena. God is on our side hakuna kitakachoharibika!
 
KATIKA WATU WAJINGA HAPA DUNIANI NAWE NI MMOJA,wewe unawaza negative side mda wote na kudharau huo upande wa pili ambao upo uwezekano wanaelimu na maendeleo kuliko hata familia yako,acha kuwa hasi mda wote na usimsemehe mtu bana,pia usitake kila mtu afanye wewe ufikiliavyo, kama umesoma basi hiyo elimu uliyo nayo haijakukombowa bado ni zuzu wa kufikilia na dictator unayetaka kila jambo lako watu waliunge mkono.

kwa upande wangu namwunga mkono akofu na nimeshachangia juu ya hilo
Inawezekana ni typing error, lakini pia effects za madras !
 
Mzee tatizo ni letter head? Tungejadili content ingependeza zaidi. Unabadili maana nzima ya hoja ukianza masuala ya udini, ni mtizamo wangu tu

Max,

Hii barua inatoa taarifa nyingi kuliko unavyofikiria na fahamu watanzania wa leo sio wale miaka ya 1980 hakuna mtu asiyeelewa nini kinaendelea hapa. Labda nikuchambulie kwanini hoja ya Kupeng'e ni valid:-
a. Askofu kama alitaka kuandika barua kwanini asingelitumia karatasi isiyo na letter head ya TEC, na kuandika barua kutoka kwa Askofu Ruzoka kwenda kwa waziri kama raia wa kawaida mwenye concern na muswada wa katiba.

b. Kwanini ataje title ya yeye anawakilisha Tume iliyo kanisani inashughulika Amani na Haki utafahamu kuwa anaiwakilisha Tume yake kufikisha maoni ya TEC.

c. Title ya barua inasema Hofu na Mashaka ya wananchi, ikimaanisha anawakilisha kundi la wananchi wanaohofia kitu fulani. Wananchi wenye kina nani wakristo wanaowakilishwa na TEC.

d.Reference na Tarehe ya barua inawakilisha rekodi ya mawasiliano which means kuna archive ya taarifa zinawakilisha interest za kanisa.

Tusifanywe wapuuzi wakati wengine tunaelewa nini kinaendelea hapa ijapokuwa maudhui ya barua ni mazuri ila kina kitu kimefichwa nyuma yake na hicho ndio intention ya barua hii ya kipuuzi. Binafsi siiungi mkono waachie wananchi wote wawakilishe mawazo yao bila ya kujali dini wala kabila lao kwani Tanzania ni kwetu sote.
 
Mi nawakubali sana wakatoliki kwa kusimamia ukweli, haki, na usawa, ni dhahiri TECH wamegundua janja inayotaka kufanywa na serikali.Badala ya katiba kuwa ya watanzania, serikali inataka kufanya maamuzi yao ndiyo yawe ya watanzania wote.Ni vyema wasikilize maoni na mapendekezo ya wenye hekima, akili na busara, kinyume cha hapo watakuja kushikishwa adabu na nguvu ya umma wala si muda murefu.God bless watanzania wote wanaoitakia heri nchi yao,
 
Tusifanywe wapuuzi wakati wengine tunaelewa nini kinaendelea hapa ijapokuwa maudhui ya barua ni mazuri ila kina kitu kimefichwa nyuma yake na hicho ndio intention ya barua hii ya kipuuzi.

Hebu tuambie ni nini kinachoendelea na ni nini kilichofichwa.
 
heshima aliyokuwa aipate rais sasa hawezi kuipata tena kwani yeye keshaonekana janja yake ni ipi ...kuanzia sasa nairudisha heshma hyo kwa nguvu ya umma,katiba ijayo ni nguvu ya UMMA na si utashi wa JK ..Amina!

Anajipeleka mwenyewe kwenye moto na mhurumia sana na akianza kuungua ataungua peke yake huku wenzake wakiwa tayari wameshatengeneza escape route.This issue is very complex for him to play with maana wengi hawana maslahi katika hayo wanayoyataka isipokuwa kundi la watu wachache ambao hata kwa mabeberu wa dunia ni rahisi to let them go kwa manufaa ya future yao na kuside na majority.
 
Du..! wadini wapo fasta .... utawajua tuu ... wameshatokea kwenye machimbo yao
 
Kwanini hajaandika barua yeye kama yeye? na kaamua kupitia TEC

Hivi wewe ndiyo mtanzania uliye na madaraka juu ya kila mtu na kila kitu. Kwanza mimi sijakuchagua uniamulie, halafu michango yako inanuka ukosefu wa maadilifu na mwelekeo wakati mwingine unakuwa kama uko chekechea lakini maudhui yako ni kimtindio wa ubongo. JK na serikali yake pamoja na wapuuzi wake kama wewe wametoa mapendekezo yao KWA MASLAHI YAO AMBAYO YANAGUSA TAASISI NA WATU BINAFSI. Wewe unataka tupate idhini toka kwako WHO ARE YOU?
 
Mada imeharibiwa;
Wavaa malapa, watu wa madrasa, wataibuka na tamko, hawana fikra (HAO NILIOWATAJA HAPO NI AKINA NANI?)
Je vinahusianaje na mada hii? Jukwaa limesheheni kejeli, vijembe, dharau, maringo etc...upendo miongoni mwa watanzania unatoweka, tabaka limeshamiri. Great thinkers should all the time refrain from arrogant postings.
 
Huyo askofu anachekesha kweli! Anasema mchakato mzima wa katiba unaanzia kwa Rais unaishia kwenye tume iliyoteuliwa na Rais ambaye ni mwenyekiti wa chama tawala!

Sasa wewe ulikuwa unataka uanze KURASINI baraza la maaskofu uishie KINONDONI ofisi za Chadema?
Kwani Padre Slaa angeshinda si angekuwa Rais pia katibu mkuu mkuu wa Chadema?
 
Huyo askofu anachekesha kweli! Anasema mchakato mzima wa katiba unaanzia kwa Rais unaishia kwenye tume iliyoteuliwa na Rais ambaye ni mwenyekiti wa chama tawala!

Sasa wewe ulikuwa unataka uanze KURASINI baraza la maaskofu uishie KINONDONI ofisi za Chadema?
Kwani Padre Slaa angeshinda si angekuwa Rais pia katibu mkuu mkuu wa Chadema?

Askofu alitaka mchakato wa katiba uanzie TEC ukaishia kwenye ofisi za Chadema hapo ndio utakuwa umewakilisha mawazo ya wananchi halisi wa kitanzania utafikiri Tanzania wakristo wako peke yao such a narrow minded ideology!!!!
 
Je TEC ni chombo cha SIASA?

Je Muhimili wa sheria za nchi (KATIBA), ni swala linalohusu siasa pekee?

Swala zima la kurekebisha katika linagusa sekta zote za nchi na ni vizuri kila sector ikachangia wakati huu ili tuweze kupata katiba itakayo waongoza wananchi wa matabaka/dini/vyama n.k yote. Tusitie shaka sana tunapoona viongozi wa dini wakitoa maoni yao (labda tu pale maoni hayo yanaonekana wazi kutaka kubomoa na sio kujenga).

Nawakilisha
 
vp TEC ingilie kazi ya bunge wao kama nani???

Unaongelea bunge lile lenye wabunge wanaopondaponda kila kipengele cha hoja/mswada/bajeti na kabla ya kukaa anasema anaunga asilimia mia kwa mia?
Bunge ambalo mbunge akitetea maslahi ya wananchi anaitwa kwenye kikao cha chama na kuonywa/kutishwa?
Bunge gani unaloliongelea?
 
Back
Top Bottom