Kati ya Mkapa na Kikwete nani zaidi?

Kabla ya mashirika ya umma kuuzwa mnaomlaumu Mkapa. Lakini inatakiwa pia kukumbuka ktk kipindi Cha Nyerere na Mwinyi ni makupuni mengi yalikufa kuliko aliyoyauza Mkapa.

Na makapuni mengi yaliyokufa kipindi hicho , baadhi yake Mkapa aliyafufua na kuyapiga bei. Watanzania naona wanapenda kuangalia likampuni limekufa kuliko kuliuuza kwa bei nafuu na hapo hapo likaajiri wa tanzania zaidi ya elfu kadhaa na kusongesha maisha mbele.

Nadhani unalokosea ni kule kuchukulia kuwa watu wanamlaumu Mkapa kwa kuuza mashirika tu; hapana,kosa lake ni lile la kuuza mashirika hayo bila kuzingatia maslahi ya Taifa. Ni kweli mashirika yote yalikuwa ni mzigo kwa serikali na ilikuwa ni lazima yauzwe. Kwa kufuata maneno ya Dr. Gates, "....there is a smart way of doing things and there is a stupid way of doing things;" Mkapa alifuata hiyo njia ya pili katika kuuza mashirika. Mkapa mwenyewe alishakiri kwa mdomo wake kuwa kweli aliboronga katika kuuza mashirika yale.
 
Nadhani unalokosea ni kule kuchukulia kuwa watu wanamlaumu Mkapa kwa kuuza mashirika tu; hapana,kosa lake ni lile la kuuza mashirika hayo bila kuzingatia maslahi ya Taifa. Ni kweli mashirika yote yalikuwa ni mzigo kwa serikali na ilikuwa ni lazima yauzwe. Kwa kufuata maneno ya Dr. Gates, "....there is a smart way of doing things and there is a stupid way of doing things;" Mkapa alifuata hiyo njia ya pili katika kuuza mashirika. Mkapa mwenyewe alishakiri kwa mdomo wake kuwa kweli aliboronga katika kuuza mashirika yale.

Mkuu
Ni kweli unaloongelea, lakini unapokua ktk hali ngumu gari lako la milioni kadhaa si ajabu ukaliza kwa laki kadhaa. Na unapo solve tatizo unaona ala! kweli nilifanya makosa kuliuza lakini at a time t wakati kulipokuwapo tatizo ulikua huna jinsi.

Haya makosa ya namna hii sio makosa karibu kila mwanadamu anayafanya
 
..kinachomshinda JK kurekebisha makosa ya Mkapa ni nini?

..nini kinachomzuia JK kupitisha sheria ya madini inayozingatia maslahi ya taifa?

NB:

..I dont believe kwamba wanaomuangusha JK ni watendaji wabovu.
 
Tatizo la viongozi wetu ni kwamba kila anayeshika madaraka anataka kujionyesha ni mujuaji kuliko waliomtangulia badala ya kuboresha na kuendeleza yale mema yaliyofanywa na hao waliotangulia.
 
Kichuguu,
Ni wapi Kikwete alisaidia kufumbua matatizo ya Zimbabwe? Huyu si alikuwa upande wa Mugabe pale mataifa ya nje yalipomwekea vikwazo Mugabe? Hakuwa na msimamo. Kwenye suala la Kenya CCM ilimwunga mkono Kibaki, na ilipoonekana kuwepo lazima ya maafikiano baada ya Wakenya kuchinjana ndipo akakimbia kumshauri Kibaki kuwa PM yuko chini ya rais, mfano wa Tanzania ambao usingefanya kazi katika coalition govermnent.
 
Huu upuuzi utakwisha lini?..
Kiongozi mzima cha chama ambaye anaweza kuwa rais anakuja kuelezea ushindani wa viongozi waliochemsha. Mkapa kafanya mazuri yapi zaidi ya uzushi mtupu. Matumizi ya Macroeconomics hayakuanzishwa na Mkapa to our advantage, hivyo sioni sifa ya kuiga Macroeconomics ya kitabuni ku apply ktk nchi yenye mazingira tofauti kuwafilisi..na sidhani kama kuna mmoja wenu anaweza kunambia faida zake zilikuwa zipi kama sii hadithi za Alinacha za GDP.

Sifa kubwa anayopewa ni utaratibu wa ukusanyaji kodi ambao ni mbaya sijawahi kuona..Hizo barabara za lane moja au mbili wakati magari nimara kumi ya uwezo sijui ndio tumefanya kitu gani. Barabara zote kuu kwenda miji ya mikoani ni mtego wa mauti kuwa na lane moja twoway traffic hazina mitaro ya maji na ikipita katikati mijini na vijijini, jambo ambalo hadi leo tumeshindwa kuelewa sababu ya vifo vingi barabarani.

Labda sisi ni wepesi sana wa kusahau kwamba kufikia mwaka 1999 deni la External Payment Arrears (EPA) lilifikia Usd 677 millioni ambazo tulishindwa kuzilipa, na through Paris Club tulipata msamaha kushusha deni hilo hadi kufikia Usd 233/m ambazo kati ya hizo Usd 133/m watu wamelamba. wala hatujui kama deni lilizobakia lilipwa au kulimbikizwa.

Ni wakati wa Mkapa Barricks Gold wameingia nchini 1999 na kuchukua Bulyanhulu kwa kuua wachimbaji wadogo wadogo...ama kweli hakujali maneno ya watu, but what have we gained.
Ni wakati wa Mkapa viongozi wote walijichotea mali na kujilimbikiza Utajiri hali wananchi wakifa njaa mikoa ya kati, kanda ya ziwa wakila mapanki (mabaki ya samaki) utadhani mipaka chume.
Ni wakati wa Mkapa tumeona mauaji ya kinyama toka Wapinzani (Pemba) na Bara, Uhuru alokuwa huyo Lipumba hakuwa nao kabisa.
Ni wakati wa Mkapa ameweka ushuru mkubwa kwa wananchi wafanya biashara wadogowadogo hali akiwapa nafuu matajiri wageni ambao hadi leo miaka 15 baadaye hawajalipa kodi zilizotakiwa.

Yaani list goes on and on kiasi kwamba Kikwete ni cha mtoto kabisa kumlinganisha na Mkapa katika kuchafua..JK hawezi ni kiongozi dhaifu hivyo kutomweza kwake Mkapa ni kushindwa kufanya maamuzi mazito lakini results zake wote wameshindwa ku deliver,k kwahiyo huyu Lipumba anaposema Kikwete hamwezi Mkapa kwa maana kwamba Mkapa alichukua maamuzi sahihi basi isingekuwa wananchi wanamchukia Mkapa kuliko kiongozi yeyote aliyewahi kutawala nchi yetu.
Hakuna Ubishi kabisa kwamba JK ni dhaifu na hafai kuwa kiongozi lakini huwezi kumlinganisha na Mkapa aliyefilisi nchini akiongoza kwa ncha ya Upanga..Na hakika sidhani kama Lipumba anafaa kuchukua uongozi wa nchi ikiwa kweli kaona Mkapa alikuwa mbora baina ya viongozi hawa.. Hakuna UOZO uliokuwa na nafuu zaidi ya mwingine.
 
Kichuguu,
Ni wapi Kikwete alisaidia kufumbua matatizo ya Zimbabwe? Huyu si alikuwa upande wa Mugabe pale mataifa ya nje yalipomwekea vikwazo Mugabe? Hakuwa na msimamo. Kwenye suala la Kenya CCM ilimwunga mkono Kibaki, na ilipoonekana kuwepo lazima ya maafikiano baada ya Wakenya kuchinjana ndipo akakimbia kumshauri Kibaki kuwa PM yuko chini ya rais, mfano wa Tanzania ambao usingefanya kazi katika coalition govermnent.



Nafikiri hiyo ndiyo weakness ya Kikwete; huwa ana tabia ya kulinda status quo hata kama kufanya hivyo ni makosa. Hata hivyo, kwenye migogoro ya kisiasa ya Kenya na Zimbabwe, Kikwete alikuwa ni one of the strong forces zilizopelekea kuwepo kwa makubaliano ya serikali za mseto akiwa mwenyekiti wa African Union:

Zimbabwe's rival political parties signed a landmark power-sharing deal today which will see President Robert Mugabe ceding some of his powers for the first time in nearly three decades of iron rule.
Mugabe, main opposition Movement for Democratic Change leader Morgan Tsvangirai and Arthur Mutambara - who heads a breakaway MDC faction - signed the agreement at a hotel in the capital, Harare, after weeks of tense negotiations.

The audience in the hotel cheered as the agreement was signed in front of African leaders including Tanzania's Jakaya Kikwete, chairman of the African Union, and South African President Thabo Mbeki, who brokered the deal.
As chairman of the African Union, Kikwete has recently emerged as a key ally and kingpin of the US in the region. Although this same message had already been passed to Kibaki by US Secretary of State Condoleezza Rice, who had visited Nairobi barely a week earlier, Kikwete's intervention was bound to meet with a better reception in Nairobi considering that he came to the Kenyan capital wearing two hats - president of a neighbouring fellow member of the East African Community as well as chairman of the African Union.
His visit to Nairobi had added significance in the wake of thinly-veiled threats by the US government, the European Union and even the United Nations of an intervention in the country if the mediation talks failed.
It was US top diplomat Jendayi Frazer who early this month on the sidelines of a summit meeting of the African Union in Ethiopia first issued the threat that the international community would impose a solution on Kenya if the mediation process led by Kofi Annan collapsed. If any such intervention was indeed being contemplated, the person who would have known its scope and full consequences would have been the chairman of the African Union.
Hence, the theory that Kibaki capitulated in the face of the threat of an AU-led military intervention in the Kenyan crisis. It appears that the US and other Western powers were worried that without concerted and sustained pressure, the AU would treat the Kenyan crisis with the same lukewarm approach it has adopted on Zimbabwe. Kikwete's intervention indicates that the Tanzanian president, who came to power in 2005, is gradually becoming the linkman of the US in the region, having replaced Uganda's President Yoweri Museveni. Signs that the US now considers President Kikwete its chief regional ally came in September 2006 when it emerged, to Nairobi's fury, that Kikwete had discussed Kenya's "instability" with President Bush during a visit to the White House.
Kikwete's rise as a regional kingpin has been bolstered by a high-profile anti-graft campaign he recently launched that has seen former powerful members of Tanzania's ruling party, Chama cha Mapinduzi (CCM), fall one after another - allowing him to redraw power centres and reform the grand old party. He dissolved the Cabinet after he had accepted the resignation of his prime minister, Edward Lowassa, and two other ministers, Nazir Karamagi and Ibrahim Msabaha, who were both implicated in a major corruption scandal. The ministers and several other officials were accused of interfering with an energy contract to favour the US-based Richmond Company, contravening laws and rules on procurement.
Siyo kwamba namfagilia Kikwete, ila sipendi pia kudharau mafanikio yake japo ni madogo.
 
Wakuu mimi naona mambo tofauti. Ngojeni niwape msemo wa Kiingereza ambao ni kifupishi cha nitakayo yasema. "Politicians come and go but public servants remain". Kwamba wanasiasa wata hama hama nafasi kila wakati lakini watumishi wa umma wengine wanakaa ofisi moja au wana baki kwenye field moja maisha yao yote ya utumishi. Hawa watu ndiyo wenye fani yao na ndiyo wenye uzoefu katika mambo mbali mbali ya kiserikali. Tatizo ni kwamba wanasiasa wana puuzia watumishi wa umma na kila mwanasiasa ana jiona mtaalamu katika kila jambo. Matokeo yake ni wanasiasa kuto kusikiliza ushauri na kufanya mambo kutokana na hisia zao tu.

Kwa nini nasema hivi. Ni kwamba watumishi wa umma kama nilivyo sema wana fani zao na wana uzoefu na pia wengi wao wata tumikia serikali mpaka watakapo staafu. Ina maana watumishi wa umma wanajua zaidi kuhusi "ins & outs" za serikali kuliko hata wanasiasa wenyewe. Kama watumishi wa umma wange pewa uhuru wa kufanya kazi yao(na hii iwe kisheria) basi hata tuweke raisi mwenda wazimu basi serikali itaendeshwa na nchi itaendelea. Tunabidi tuwape watumishi wetu wa umma kufanya kazi yao na si kuburuzwa buruzwa na matakwa ya wanasiasa.

Kwa sababu niliyo orodhesha juu ndiyo maana leo hii ukiniambia JK ana wasaidizi wabovu sielewi. Kwa sababu baraza la mawaziri lime badilika, raisi ame badilika lakini watumishi wa umma waliyo mtumikia Mkapa ndiyo hao hao wanaomtumikia JK. Kama watumishi wa umma wange tumiwa ipasavyo basi kupokezana madaraka kati ya wanasiasa isingekua kama kuanzia mwanzo kama ilivyo sasa. Raisi anaye chukua madaraka inakua haanzi tokea mwanzo bali anakua muendelezo wa awamu iliyopita.

Kwa hiyo kwangu mimi naona ili nje iendelee basi haya yanabidi yatokee....
a)Serikali ivutie vijana wanao maliza shule kujiunga na serikali badala ya vijana wote kukimbilia kwenye sekta binafsi. Of course kila mtu ana angalia maslahi yake kwa hiyo neno uzalendo isiwe kigezo pekee cha kuvutia vijana bali serikali kweli itoe incentives ya watu kutaka kuitumikia serikali. Nasema hivi kwa sababu kijana anaye toka shule na kujiunga serikalini akisha fikisha tu umri wa miaka thelathini na kitu basi atakua na uzoefu na kutokana na kupanda cheo pia ataweza kumudu maisha yake.
b)Serikali ithamini wafanyakazi wake haswa wana taaluma wake. Watu hawa wapewe mshahara mzuri itakayo wawezesha kumudu maisha yao na pia wapewe uhuru wa kufanya kazi zao. Hamna furaha kama mtu kuweza kufanya kazi anayo ipenda sasa mtu akiwa ana buruzwa buruzwa kama mtoto hata kua na changamoto ya kufanya kazi.
c)Vyeo vya serikalini visiwe kisiasa!!! Mtu apandishwe cheo kutokana na ufanyaji kazi wake na uzoefu wake. Vyeo visi tolewe na wanasiasa kama zawadi kwa watu wao. Mtu apandishwe kazi kutokana na uwezo wake na si kuangalia umri tu kama inavyo onekana sasa.

Ndugu wana JF wenzangu tukiweza kufanya hivi basi wala kuta kuwa hakuna shida ya kuongelea raisi yupi aliye bora maana nchi itakua inaendeshwa na watu wenye uwezo na uzoefu. Watumishi wakiruhusiwa kufanya kazi zao ipasavyo na wanasiasa wabaki kwenye nafasi ya kuhakikisha tu kwama sheria zenye manufaa kwa taifa ndizo zina pitishwa basi iwe raisi ni Nyerere, Mwinyi, Mkapa, JK au hata mwenzangu na mie basi mtaona maendeleo yaki chipuka.
 
Mwanafalsafa1,
Mkuu kuanza kufkiria nje ya Uongozi mbovu ni mwanzo wa kuharibikiwa kabisa. Hizi ngojera zooote zinazotokea sasa hivi ni kutufanya wananchi tufikirie kwamba tatizo ni JK hali Uongozi mzima wa CCM umetufikisha hapa tulipo. Utendaji kazi siku zote unafuata Uongozi na sheria zilizopo..Sisi tunaitwa Wavivu tuko nchi za hawa jamaa na tunachapa kazi kuliko hata Wazungu wenyewe.

Kuna Mtanzania hapa Toronto Canada ni Chief Survey wa mji mzima (City) huyu angekuwa bongo angevulunda tu..Kuna mwingine hapa ni mtaalam wa madini kiasi kwamba serikali na mashirika wanamtumia kufanya kazi zao lakini huyu angekuwa Bongo leo hii ni kilevi.. Kwa hiyo tukianza kuwatukuza viongozi wabaya na kujaribu kutafuta mchawi mwingine hapo ndipo tutakapo poteza mwelekeo..CCM has to go -Period.
 
Lipumba yuko sahihi kwa kiasi kikubwa. Katika kipindi chake cha kwanza, Raisi Mkapa aliongoza nchi vizuri sana; mara nyingi nimekuwa nachukulia kuwa huenda alikuwa anaogopa kufanya madudu asije kukemewa na Nyerere. Baada ya Nyerere kufariki, ndipo Mkapa akawa kichwa ngumu katika kipindi chake cha pili na kuanza kuboronga. Mabaya yote yaliyofanbywa na Mkapa ambayo ndiyo wananchi wengi wanakumbuka ni yale aliyofanya katika kipindi cha pili; alipoanza kuwa mjasiliamali basi akauza nchi yote kwa mabavu hata pale ambapo ilikuwa ni wazi kabisa kuwa uamuzi wake haukuwa na faida kwa nchi; alichjali zaidi ni msalahi yake binafsi kuliko yale ya taifa. Unfortunately, historria huwa inajua kuadhibu watu wa aina hiyo kwa sababu huwa inakumbuka zaidi mabaya yao kuliko mema yao.

Mkuu your theme in this part of the post ni kwamba Mkapa ali tupigisha hatua moja mbele aka turudisha hatua mbili nyuma. Sawa kwa kufuata maneno yako mkuu tuchukulie kweli katika kipindi cha kwanza Mkapa alifanya mazuri. Lakini kama ni hivyo si atakua alivunja kila kitu alicho jenga katika kipindi chake cha kwanza? Watu wengine wana sema Mkapa ali kuza uchumu etc lakini ni wakati wa uongozi wake ndipo madudu kama EPA yalipo tokea. Kuna faida gani kukuza uchumi kisha kuruhusu ubadhilifu wa mabilioni ya fedha za umma? Ndiyo yale yalle ya hatua moja mbele hatua mbili nyuma.

Kwa upande wa Kikwete, siyo kweli kuwa hajafanya mazuri. Kikwete amefanya mambo kadhaa yanayoheshimika kimataifa; kwa mfano alikuwa msitari wa mbele katika kutatua migogoro ya kisiasa ya Kenya na Zimbabwe, amesaidia sana kujenga amani katika eneo la maziwa makubwa, na mengineyo mengi katika bara la Afrika. Utawala wake pia umeimarisha urafiki na nchi za nje hasa Marekani ambapo siku hizi tu watalii wengi wa Kimarekani wanakwenda Tanzania kuliko Kenya, kinyume na zamani. Ameiwezesha Tanzania kuwa nchi ya kwanza ya Afrika kuwa mwenyeji wa mkutano wa WEF ambao umekuwa ukifanyikia Davos miaka yote. Kwa hiyo ana mambo mazuri aliyofanya ingawa yote hayo hayamsaidii raia wa kawaida aliyepiga kura na kumpangisha Kikwte kwenye lile kasri la Magogoni.

Hayo yote uliyo yasema ni mafanikio katika stage ya kimataifa mkuu. Kumbuka JK ni raisi wa Jamhuru wa Muungano wa Tanzania. Wajibu wake wa kwanza ni kwa wananchi wake na siyo jamii ya kitaifa. Mafanikio ya kimataifa yaambantane na maendeleo ya kitaifa. Hatuwezi kuita mafanikio kama raisi ame fanikiwa kwenye stage ya kimataifa lakini hajafanya chochote kwa wananchi wake wa kawaida waliompigia kura.
 
Mwanafalsafa1,
Mkuu kuanza kufkiria nje ya Uongozi mbovu ni mwanzo wa kuharibikiwa kabisa. Hizi ngojera zooote zinazotokea sasa hivi ni kutufanya wananchi tufikirie kwamba tatizo ni JK hali Uongozi mzima wa CCM umetufikisha hapa tulipo. Utendaji kazi siku zote unafuata Uongozi na sheria zilizopo..Sisi tunaitwa Wavivu tuko nchi za hawa jamaa na tunachapa kazi kuliko hata Wazungu wenyewe.
Mkuu I think you got me wrong.m Sija sema tatizo siyo viongozi. ndiyo maana ningesema watumishi wa umma wange pewa uhuru wa kufanya kazi zao na hao wanasaisa basi tusinge kua hapa tulipo. Wanasiasa wetu wanapenda kufanya maamuzi ya kitaaluma bila kufuata ushauri wa wataalamu. Kwa hiyo yes first and for most ni hao wanasiasa. Na unaongelewa kuongoza kwa sheria huku una sahau wanasiasa ndiyo wana tunga sheria. Wange tunga sheria za kuwapa uhuru watumishi wa umma basi tusinge kuwa hapa tulipo. Kwa hiyo sija sema utumishi wa umma ndiyo tatizo bali wao ndiyo suluhisho.


Kuna Mtanzania hapa Toronto Canada ni Chief Survey wa mji mzima (City) huyu angekuwa bongo angevulunda tu..Kuna mwingine hapa ni mtaalam wa madini kiasi kwamba serikali na mashirika wanamtumia kufanya kazi zao lakini huyu angekuwa Bongo leo hii ni kilevi.. Kwa hiyo tukianza kuwatukuza viongozi wabaya na kujaribu kutafuta mchawi mwingine hapo ndipo tutakapo poteza mwelekeo..CCM has to go -Period.

Lakni si unaona mkuu kwamba huyo mwenzio anafanya vizuri kwa sababu kapewa uhuru wa kufanya kazi yake bila kuingiliwa na siasa au wanasiasa? That is exactly my point. Tunabidi tuwe na mfumo mzuri ambao upo flexible hata tunapo pata viongozi wabaya kwa sababu ukweli una baki pale pale kuwa huwezi kupata viongozi wazuri kila wakati. Ndiyo maana kwa nchi hata kama Marekani hata walipo pata raisi ovyo kama Bush bado alikua na limits zake kisiasa.
 
Mwanafalsafa1,
Mkuu nilikuelewa vizuri sana na ndio maana nikasema tusitake kupotosha Ubovu wa viongozi wetu kwa kufikiria nje ya hapo. Hawa jamaa wangu nilowataja hawafanyi kazi na viongozi wa nchi hii isipokuwa Uongozi na sheria zilizopo zinawalazimu wafanye mazuri pasipo kufikiria Rushwa wala kuiba. Ni kweli kabisa mfumo wao ni wa kiongozi sii Kitawala hivyo marais wetu pamoja na nguvu kubwa wameshindwa kabisa kutusogeza hatua moja mbele..

Na hatuwezi kufanya mabadiliko ya aina yoyote ile pasipo kuwaondoa CCM kwa sababu hawa wooote wameisha fanya madudu mengi na makubwa, hivyo huwezi kutegemea ushirikiano wao hali wanajua fika kwamba wanapotakiwa kuwa ni jela na kufilisiwa mali zao.. Hata mimi ningekuwa nafasi ya JK ningekuwa na wakatimgumu sana kufanya maamuzi magumu kwa sababu I'm part of the problem... Waswahili wanasema Simba akisha onja nyama ya Binadamu hataachi kula, hivyo kufikiria kuwa naye karibu hawa Simba kunaweza kubadilisha tabia zao bila shaka tunajidanganya..nadhani ndio tutakuwa tumemsogezea chakula mdomoni..
Hivi kuna tatizo gani kuwaondoa CCM katika mawazo yetu na kufikiria mwanzo mpya?..
 
Mwanafalsafa1,
Mkuu nilikuelewa vizuri sana na ndio maana nikasema tusitake kupotosha Ubovu wa viongozi wetu kwa kufikiria nje ya hapo. Hawa jamaa wangu nilowataja hawafanyi kazi na viongozi wa nchi hii isipokuwa Uongozi na sheria zilizopo zinawalazimu wafanye mazuri pasipo kufikiria Rushwa wala kuiba. Ni kweli kabisa mfumo wao ni wa kiongozi sii Kitawala hivyo marais wetu pamoja na nguvu kubwa wameshindwa kabisa kutusogeza hatua moja mbele..

Na hatuwezi kufanya mabadiliko ya aina yoyote ile pasipo kuwaondoa CCM kwa sababu hawa wooote wameisha fanya madudu mengi na makubwa, hivyo huwezi kutegemea ushirikiano wao hali wanajua fika kwamba wanapotakiwa kuwa ni jela na kufilisiwa mali zao.. Hata mimi ningekuwa nafasi ya JK ningekuwa na wakatimgumu sana kufanya maamuzi magumu kwa sababu I'm part of the problem... Waswahili wanasema Simba akisha onja nyama ya Binadamu hataachi kula, hivyo kufikiria kuwa naye karibu hawa Simba kunaweza kubadilisha tabia zao bila shaka tunajidanganya..nadhani ndio tutakuwa tumemsogezea chakula mdomoni..
Hivi kuna tatizo gani kuwaondoa CCM katika mawazo yetu na kufikiria mwanzo mpya?..

Nime kusoma sana mkuu. Ndiyo maana nasema kila kitu ni mfumo mkuu. Nikirudia mfano wangu wa Marekani mkuu haijalishi kama madarakani wapo Democrats au Republicans. Katika historia ya karne ya 20 ya Marekani hadi sasa hakuna chama kilicho wahi kutoa maraisi watatu mfululizo. Kwa maana hamna chama kinacho onekana ni Mungu mtu. Kwetu sisi wengi wana jiuliza kama siyo CCM basi nani. Taizo ni chama mbadala na iwe ni mfumo wetu au wananchi wenyewe bado hatuja toa chama mbadala. Kwa hiyo mimi nadhani kabla ya kuongelea kuiondoa CCM tuangalie mbadala yake ni nini. Isije ikawa swala tu la kumtoa zimwi mmoja na kumuingiza zimwi mwingine. In my opinion mkuu bado hatuja pata chama mbdala na pindi tuta kapo pata chama mbadala basi hata CCM wenyewe ita walazimu kustep up ili kuendelea kudumu.

Kwa hiyo mkuu ukiangalia kiundani tatizo letu ni kwamba we lack competition na more importantly competition among politicians and political parties. Sasa hivi kuna viongozi au chama kinacho dhani hata wafanyeje ushindi ni wao tu. Cushion hiyo ikishaondoka tu basi kitakacho fuata hapo ni siasa za kweli na juhudi za kweli . Lakini so far sijaona chama chochote kinacho weza kuichallenge CCM. Vyana vyote vina fight for second place.
 
Huu upuuzi utakwisha lini?..
Kiongozi mzima cha chama ambaye anaweza kuwa rais anakuja kuelezea ushindani wa viongozi waliochemsha. Mkapa kafanya mazuri yapi zaidi ya uzushi mtupu. Matumizi ya Macroeconomics hayakuanzishwa na Mkapa to our advantage, hivyo sioni sifa ya kuiga Macroeconomics ya kitabuni ku apply ktk nchi yenye mazingira tofauti kuwafilisi..na sidhani kama kuna mmoja wenu anaweza kunambia faida zake zilikuwa zipi kama sii hadithi za Alinacha za GDP.

Sifa kubwa anayopewa ni utaratibu wa ukusanyaji kodi ambao ni mbaya sijawahi kuona..Hizo barabara za lane moja au mbili wakati magari nimara kumi ya uwezo sijui ndio tumefanya kitu gani. Barabara zote kuu kwenda miji ya mikoani ni mtego wa mauti kuwa na lane moja twoway traffic hazina mitaro ya maji na ikipita katikati mijini na vijijini, jambo ambalo hadi leo tumeshindwa kuelewa sababu ya vifo vingi barabarani.

Labda sisi ni wepesi sana wa kusahau kwamba kufikia mwaka 1999 deni la External Payment Arrears (EPA) lilifikia Usd 677 millioni ambazo tulishindwa kuzilipa, na through Paris Club tulipata msamaha kushusha deni hilo hadi kufikia Usd 233/m ambazo kati ya hizo Usd 133/m watu wamelamba. wala hatujui kama deni lilizobakia lilipwa au kulimbikizwa.

Ni wakati wa Mkapa Barricks Gold wameingia nchini 1999 na kuchukua Bulyanhulu kwa kuua wachimbaji wadogo wadogo...ama kweli hakujali maneno ya watu, but what have we gained.
Ni wakati wa Mkapa viongozi wote walijichotea mali na kujilimbikiza Utajiri hali wananchi wakifa njaa mikoa ya kati, kanda ya ziwa wakila mapanki (mabaki ya samaki) utadhani mipaka chume.
Ni wakati wa Mkapa tumeona mauaji ya kinyama toka Wapinzani (Pemba) na Bara, Uhuru alokuwa huyo Lipumba hakuwa nao kabisa.
Ni wakati wa Mkapa ameweka ushuru mkubwa kwa wananchi wafanya biashara wadogowadogo hali akiwapa nafuu matajiri wageni ambao hadi leo miaka 15 baadaye hawajalipa kodi zilizotakiwa.
QUOTE]

uwezo wa serikali kujenga barabara hata za lane 4 upo ..tatizo hata saa resource hazitoshi inabidi wagawe mijini wapate angalau lane mbili na maeneo mengine pia wapate....

kuhusu suala la barrick -bulyanhulu ...lilianzia wakati wa mzee mwinyi.....na waziri aliyesimamia kuwaondoa wananchi pale ili muwekezaji wa mwanzo achukue eneo kabla ya yule mwekezaji kuja kuwauzia barrick ni Maj Jakaya mrisho Kikwete[enzi hizo akiwa waziri wa nishati na madini]..hata mradi ule contraversial unaotafuna taifa hadi leo wa VIP engineering 5%[mabibo beer],na kampuni ya kimalaysia95%....ya ule mradi wa kuzalisha umeme kule tegeta ambao kila siku una matatizo ....jakaya ndiye aliyeingia mkataba hata baada ya world bank kuwashauri kuwa mradi ulikuwa wa gharama kubwa na ingekuwa faida zaidi kwa serikali kukununua mtambo mpya kwa dola milioni 60 [enzi hizo]...ikumbukwe kuwa mradi ule waliovercharge wakasema wamenunua mtambo kwa dola milioni 120...na akamshauri mzee mwinyi ..akaridhia......tangu wakati huo [1992] hadi sasa jamaa wanastahili dola milioni 3 kwa mwezi ....kama capacity fee[umeme ufuliwe au usifuliwe]...ni juzi tu baada ya richmond ndio serekali imeanza kukataa kuwalipa.....but inakuwa kama arrears ...mwisho tutawalipa tu wakati wa ku wind up......
mikataba mibovu ya madini nakubali ni kosa la mkapa .....pamoja na kuwa yeye alikuwa anajitetea kuwa attractiveness ya nchi enzi hizo kwa uwekezaji ilikuwa chini mno..so yeye ilikuwa ngumu kupata fair deal....na alifanya akijuwa kuwa baadaye wakishaanza kufaidika itakuwa rahisi kurekebisha..and that is what kikwete get to do now...tayari Tanzania inagombewa na wawekezaji ..we can negotiate better deals...hakuna kitu kinaniuma kama wawekezaji wanavyouziana shares huko wallstreet sisi hatupati kitu...sijui sheria mpya inasemaje...labda kwa kuwa mh zitto ni mjumbe kule aje atuambia....lakini wenzetu uganda sheria yao nimemsikia museveni anasema juzi kuwa ...pale wawekezaji wanapoamua kuuziana makampuni..juu kwa juu basi uganda wana charge 30% corprate tax kwenye mauzo.....na karibuni watatengeneza dola milioni 400 kwa kuwa Tullow Oil wanauza interest zao kwenye mradi wa mafuta uganda kwa almost dola bilioni 1.5 .[imagine hadi sasa hao tullow wametumia below usd 200 m kwenye mradi...just see they are making a profit of over 800m..just in four years]...so its proven hapo uganda watakula 30% ya mauzo.....tungekuwa na sheria hii hapa na namna waweekezaji wanavyouziana makampuni hapa kwetu...tusingekuwa na matatizo tuliyonayo ya kushindwa huduma muhimu...

Tanzania hapa kwetu haya makampuni yanayotafuta gesi na hata madini yanatuibia sana kuna amabo kazi yao ni exploration tu....wakishapata haoo wanakimbilia kwenye masoko ya hisa na kutangaza...wanapata wanunuzi ....haoo wanapepea wanabadilisha jina la kampuni ..imetoka...change of ownership tayari..!!!...kama walikuwa mkuranga ...wanahamia mtwara.....kuendelea na utafiti!!!..sidhani kama TPDC wanashindwa kuwa na hizo information na kuzitumia kuuzia huko nje..na yet wakapata pesa na serikali ikapata hisa nzuri!!
 
Philemon Michael,
Mkuu sijakuelewa hata kidogo..Unaposema resources za ujenzi wa barabara hazitoshi inabidi wagawe mijini, hapa sikuelewi tunapozungumzia mazuri ya kiongozi..
Pili, Barricks waliingia nchini wakati wa Mkapa tena basi yeye ndiye alikwenda kuzindua ufunguzi wake baada ya kushinda uchaguzi awamu ya pili ..Ni baada ya Nyerere kufa pia nakumbuka vizuri kuwa Barricks waliingia mkataba mpya kabisaa sio ule wa Sutton baada ya Mkapa kulegeza sheria zetu - source hii hapa. Sasa sijui kama kweli JK alikuwa waziri wa madini au Mambo ya nje but all I know is the buck stops where.

Pia issue ya IPTL nimeisoma sana na tumejadiliana sana humu JF tukafikia kufahamu Ukweli kwamba Mwinyi aliondoka deal halijakubalika ila alipoingia Mkapa ndipo tukaweka sahihi mkataba ule.. iwe JK alikuwa waziri au nani bado baraka za Mkapa ndizo zinahesabika..Yooote madudu yanayotokea wakati wa JK ni madudu yake yeye mwenyewe iwe kupitia Lowassa na Richmond, Tunavyoendeshwa TRA, office za serikali, mashuleni makazini na kadhalika yote ni ktk hesabu ya Uzembe wa JK. Tena Udini na Ukabila umerudi kwa kasi kubwa sana siwezi kuwalaumu Mapadre na Masheikh!

Kwa taarifa tu - Je wakuu zangu mnayo habari kwamba mafuta yamepatikana offshore Mtwara na yatachimba na kampuni kutoka Brazil ambayo tayari imesha sajiliwa?
 
Phillemon Mikael,
Ukitaka kujua mchawi katika sakata la madini usiangalie mbali ya uhusiano wa Kikwete na Sinclair. Hata huo mkataba mpya unahusu tu kampuni zitakazokuja baadaye. Haumgusi Sinclair kabisa. Na leseni zote za uchimbaji madini Tz kishazikamata Sinclair, kwa hiyo hata ikija kampuni mpya anayelipwa license fee si serikali ya Tanzania bali Sinclair.
 
Mnafikiri mtabadilisha nchi kwa kulinganisha viongozi kwenye mitandao. Kafanyeni kazi acheni longolongo.:becky::becky::becky::becky:
 
Mnafikiri mtabadilisha nchi kwa kulinganisha viongozi kwenye mitandao. Kafanyeni kazi acheni longolongo.:becky::becky::becky::becky:
Zakumi,
Good to see you again. I have a brand new pair of shoes for you:-
 
Philemon Michael,
Mkuu sijakuelewa hata kidogo..Unaposema resources za ujenzi wa barabara hazitoshi inabidi wagawe mijini, hapa sikuelewi tunapozungumzia mazuri ya kiongozi..
Pili, Barricks waliingia nchini wakati wa Mkapa tena basi yeye ndiye alikwenda kuzindua ufunguzi wake baada ya kushinda uchaguzi awamu ya pili ..Ni baada ya Nyerere kufa pia nakumbuka vizuri kuwa Barricks waliingia mkataba mpya kabisaa sio ule wa Sutton baada ya Mkapa kulegeza sheria zetu - source hii hapa. Sasa sijui kama kweli JK alikuwa waziri wa madini au Mambo ya nje but all I know is the buck stops where.

Pia issue ya IPTL nimeisoma sana na tumejadiliana sana humu JF tukafikia kufahamu Ukweli kwamba Mwinyi aliondoka deal halijakubalika ila alipoingia Mkapa ndipo tukaweka sahihi mkataba ule.. iwe JK alikuwa waziri au nani bado baraka za Mkapa ndizo zinahesabika..Yooote madudu yanayotokea wakati wa JK ni madudu yake yeye mwenyewe iwe kupitia Lowassa na Richmond, Tunavyoendeshwa TRA, office za serikali, mashuleni makazini na kadhalika yote ni ktk hesabu ya Uzembe wa JK. Tena Udini na Ukabila umerudi kwa kasi kubwa sana siwezi kuwalaumu Mapadre na Masheikh!

Kwa taarifa tu - Je wakuu zangu mnayo habari kwamba mafuta yamepatikana offshore Mtwara na yatachimba na kampuni kutoka Brazil ambayo tayari imesha sajiliwa?


mkuu kuhusu barrick nimekusoma..lakini kama umenisoma vema nimesema kuwa kikwete akiwa waziri hakusimamia uhamishaji wa wananchi bulyanhulu ili waingie barrick ...bali alisimamia uhamishaji wa wachimbaji wadogo ...ili aingie muwekezaji ambaye yeye ndiye alikuja kuwauzia barrick.......na nikaongelea kuwa kwa namna sheria zetu zilivyo mbaya.....hatukuambulia chochote kwenye mauzo yao.....nikasema nchi nyingiene ie uganda huwa wana charge 30% hata kama mauzo yamefanyika nje ya nchi ..juu kwa juu....

suala la IPTL ni kweli ni moja ya hoja za mwanzo kabisa hapa jamvini na wote tunajuwa ushiriki wa jk...na katibu mkuu patrick ntabanzibwa.....walivyotofautiana.....

kwa kifupi niseme hakuna mwenye afadhali...walichokuwa wanakosea ma operatives wa jk...na kibaya ni ile juhudi ya makusudi waliyokuwa wakiifanya kumchafua mkapa hata pasipostahili....ina wa cost sasa kwa sababu wananchi wanaanza kufananisha....na kuona bora ZIMWI LIKUJUALO........hii haiondoi ukweli kuwa yote haya ni MAZIMWI!!!
 
Phillemon Mikael,
Ukitaka kujua mchawi katika sakata la madini usiangalie mbali ya uhusiano wa Kikwete na Sinclair. Hata huo mkataba mpya unahusu tu kampuni zitakazokuja baadaye. Haumgusi Sinclair kabisa. Na leseni zote za uchimbaji madini Tz kishazikamata Sinclair, kwa hiyo hata ikija kampuni mpya anayelipwa license fee si serikali ya Tanzania bali Sinclair.

SO JE SHERIA MPYA INACHARGE KODI KWENYE MAUZO YA HAYA MAKAMPUNI KWENYE MASOKO YA HISA???.....Maana hapa kati hawa barrick wameuziana share na kubadilisha ownership wanavyotaka....kama walivyophamishia milki ya barrick kwenda ABL [african barrick]...ilikuwa wakati muafaka kwa serikali kupewa hisa za bure..pale..lakini kimiya....

Hili la mafuta mukandara ni kweli ...wanachofanya kama nilivyokuambia hao watafutaji mafuata wakisha drill rig,,,,wakikuta mafuta wanafunika....wanatafuta mteja wanauza Juu kwa juu.....uganda hilo hawajakubali.....ndio maana hata mafuta hayajaanza wananza kunusa pesa!!
 
Back
Top Bottom