EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Wewe ni mwajiri na unataka kumwajiri Project Manager wa kusimamia miradi ya utoaji huduma ya ushauri (consulting service delivery projects) kwenye kampuni yako. Umepokea CVs kwa ajili ya hii nafasi na katika kuzichambua unakutana na CVs za David and Simon.
CV ya David inaonyesha kuwa ni Consultant na Project Manager kwenye kampuni nyingine ambayo ni mpinzani mkubwa sana kibiashara kwa kampuni yako. Amefanya kazi kwenye hiyo kampuni pinzani kwa mudawa miaka kumi. CV ya Simon inaonyesha kuwa ameshawahi kuwa Consultant na Project Manager kwenye sekta mbalimbali za biashara kwa muda wa miaka kumi lakini ana experience ndogo sana kwenye sekta ya biashara ya kampuni yako.
Kielimu, David and Simon wamesomea vitu tofauti kabisa. David ana BS in Business, MBA na certificate in PMP (Project Management Professional). Simonana BS in Computer Science na MS in Marketing. Kati ya David na Simon unatakiwa uchague mmoja tuu kwa ajili ya interview. Utamchagua yupi na kwa sababu zipi?