kati ya hawa nani mkali?....na kwa nini?

Ninakubaliana na wewe kuwa Dr Lick ni mchambuzi mzuri na huenda akawa na kipaji, kipaji ninachosema mimi nikipaji cha kusoma mambo kwenye mitandao na kuweza kuyaelezea yakaleta maana na mvuto. Kumbe ili uwe mchambuzimzuri lazima uwe mfuatiliaji wa soka uwanjani na kwenye vyombo vya habari kama magazeti, mitandao, TV na Redio. Zaidi ya yote uwe na uwezo wa kuchambua/kuchanganua soka kulingana na wakati. Suala la kwamba wengine wanabase kwenye mitandao ningesema Dr. Lick ndoo msomaji mzuri wa kwenye mtandao kuliko wengine hao na ndo maana anauwezo wa kuja na update hizo unazozisikia. Otherwise tupo pamoja.
 
Wale wa ATN ndo funga kaz! Mtangazaj ndo mchambuaji, bas full kizungumkuti.
 
Daah ebwana Dauda yupo juu kupita maelezo, tena pande zote. Ukiangali mtu kama Dr. Abdalah ni mkali wa kuchambua mchezaji mmoja mmoja na historia yake, then kumwembe yupo kotekote ila hamfikii sheff mwana wa Dauda
 
Shafii na Kumwembe wao wanajua soka la England U man U na u arsenal ndio wanaoujua.Lik kiboko anajua soka.Huyo Shafii alishasema ligi ya England ndio bora kukiko zote duniani sasa mchambuzi anajua nini huyo?
 
Rishard, Mziray wanafiki no 1. Wakati ule wa fainali za kombe la mataifa ya Africa waliniudhi mbaya, kuna mechi moja refa aliboronga vibaya mno wao wakati wa uchambuzi wote wakasisitiza kuwa maamuzi ya utata yote yalikuwa sawa, yaani walinikera kidogo nipasue lunìnga... Ajabu baada ya siku mbili yule refa akaadhibiwa kwa kuboronga mechi ile!! Aliyekula Mayai na Matembele naye kila sentensi moja utasikia 'unless otherwise' hana lolote... Mtu ambaye ni kiboko ni Dk Licky tu, pamoja na vyombo vya habari vya bongo kuonekana kama vinambania siku hizi.
 
Kwa hapa bongo hakuna anayemfikia Dr Riki hata kwa asilimia 50,Riki na mpira ameanza miaka chungu nzima alianza kufuatilia mpira enzi hizo alikuwa ananunua magazeti ya mambo ya mpira amabayo kwa kipato cha enzi zile yalikuwa aghali sana na hayo magazeti yalikuwa yana toka Ulaya na yalikuwa na mambo mengi ya uchambuzi,kuna wakati hao Wekundu wa Msimbazi walimtaka awe coach wao
 
shafii hamna kitu, anasema vitu ukienda mtandaoni unaviona Kwa urahisi unaingia goal.com inaviona bila kuhangaika kutafuta , Dr. ni mkali kushinda wote, anakuelezea kabisa maybe nani atatoka sub nani ataingia kocha atafanya nini kipindi cha pili .. Dr ukimsikiliza hukosi tabasamu usoni....
 
Kama mwenye Data na Breaking news za ukweli Eddo Kumwembe yuko juu: anacheza sana na mitandao kutafuta Info na yuko makini kwa kile anachokiongea ''anaenda na matukio kabisaa''.
Dr. Licky kwa adithi za kale ktk soka hapo ndo kwake kiasi kwamba uchambuzi wake umebeba sana matukio ya siku za nyuma sana kwa wale ambao wanaelewa wanamuona kama vile amepitwa na wakati japo anasifika kwa mbwembwe katika uchambuzi wa soka.

Shafii Dauda, huyo bado ajakomaa kabisa, upenzi na ushabiki unamtawala kwa sana, uchambuzi wake ni wa Ligi ya Vodacom.

Hivyo basi viwango viko hivi:-
1. Eddo Kumwembe(0„6)
2. Dr. Licky
3. Shafii Dauda
---------------------------------------------
 
Back
Top Bottom