habi alex
Member
- Dec 1, 2011
- 90
- 12
Kwa muda mrefu nimekuwa sifurahishwi kabisa na tabia ya viongozi wa Tanzznia kuwarisisha uana siasa watoto wao. Mfano wa wanasiasa waliorithi uana siasa wa baba zao ni pamoja na Amani Abeid Karume, Husein Mwinyi, Vita Kawawa, Adamu Malima, January Makamba,....
Napenda kutoa rai kwa Watanzania wenzangu tusikubali kuendeleza usultani wa hawa wanasiasa uchwara, wapo hapo kulinda maslahi yao binafsi na ya baba zao na ndugu zao wengine. Naamini kuwa nchi hii inao watu wengi wenye akili na uwezo wa kuongoza, na iwe mwisho na mwiko mwanasiasa kumwambukiza mtoto wake uana siasa.
Kwa kuanzia uchaguzi wa mwaka 2015 tuwapige chini watoto wote wa vigogo wanaozani ni wao tu ndio wanaweza kuongoza.
Aidha, wabunge wote waliokwisha tumikia wananchi kwa vipindi viwili nao iwe mwisho wao kugombea. Na tuwape fursa na wengine wakajaribu umaskini wa bingeni kama alivyosema spika Makinda. Hili litasidia kuondoa usultani katika nchi hii na kuwafanya viongozi wawe na hofu ya wananchi na hofu ya Mungu pia.
Naomba kutoa hoja.
Napenda kutoa rai kwa Watanzania wenzangu tusikubali kuendeleza usultani wa hawa wanasiasa uchwara, wapo hapo kulinda maslahi yao binafsi na ya baba zao na ndugu zao wengine. Naamini kuwa nchi hii inao watu wengi wenye akili na uwezo wa kuongoza, na iwe mwisho na mwiko mwanasiasa kumwambukiza mtoto wake uana siasa.
Kwa kuanzia uchaguzi wa mwaka 2015 tuwapige chini watoto wote wa vigogo wanaozani ni wao tu ndio wanaweza kuongoza.
Aidha, wabunge wote waliokwisha tumikia wananchi kwa vipindi viwili nao iwe mwisho wao kugombea. Na tuwape fursa na wengine wakajaribu umaskini wa bingeni kama alivyosema spika Makinda. Hili litasidia kuondoa usultani katika nchi hii na kuwafanya viongozi wawe na hofu ya wananchi na hofu ya Mungu pia.
Naomba kutoa hoja.