thereitis
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 297
- 41
Naibu waziri Tamisemi anayeshughulikia elimu aliyasema hayo leo asubuhi kupitia kipindi cha jambo Tanzania kinachorushwa na TBC1. Amesema walimu na watumishi wa kada nyingine ambao wamesoma chuo kwa muda mfupi ukilinganisha na madaktari wanastahili mshahara huo.
Kwa mtazamo wangu naibu waziri Majaliwa hayupo sahihi. Nafikiri si sawa kumlipa mtumishi mshahara mkubwa au mdogo eti kwa kuangalia kigezo cha muda aliotumia alipokuwa chuoni. Watumishi wote wa serikali wanafanya kazi ya kuwatumikia watanzania kwa kutumia taaluma zao; wote wanamahitaji ya kibinadamu yanayolingana; wote wanaishi katika nchi moja yenye mfumuko mkubwa wa bei ya bidhaa.
Naomba michango yenu wakuu.
Kwa mtazamo wangu naibu waziri Majaliwa hayupo sahihi. Nafikiri si sawa kumlipa mtumishi mshahara mkubwa au mdogo eti kwa kuangalia kigezo cha muda aliotumia alipokuwa chuoni. Watumishi wote wa serikali wanafanya kazi ya kuwatumikia watanzania kwa kutumia taaluma zao; wote wanamahitaji ya kibinadamu yanayolingana; wote wanaishi katika nchi moja yenye mfumuko mkubwa wa bei ya bidhaa.
Naomba michango yenu wakuu.