Kashfa nzito chuo cha polisi moshi hadi kifo cha askari polisi

Ngumi

New Member
Oct 3, 2012
1
0
:embarassed2:Habari ambazo nimezipata toka kwa kaka yangu anayehudhuria mafunzo ya kupandishwa cheo katika Chuo Cha Polisi Moshi (CCP). Ni kuwa siku ya jana chuoni hapo ilikuwa ni majonzi makubwa kwa askari wanaohudhuria course mbalimbali chuoni hapo. Majonzi hayo na vilio vilitawala pale mwili wa askari mwenzao aliyekuwa akihudhuria mafunzo ya ngazi ya corpolo kutokea mkoani Manyara. Askari huyo alifariki dunia kwa prssure na kisukari. Sasa basi kilichipelekea kuwepo na vilio vingi na lawama za hapa na pale ni kwamba: Askari huyo ambaye kwa sasa ni marehemu na mungu amlaze mahali pema, hakuhudhuria kipindi chuoni hapo kwa vile alikuwa na mapumziko aliyopewa na daktari wa Chuo ( ED ). Baada ya kutafutwa wasiohudhuri vipindi ikaonekana na yeye hakuhudhuria hivyo Afisa mmoja aliyetajwa kwa jina la JB IBRAHIM mwenye Cheo cha Mrakibu mwandamizi (ASP), na ambaye ni Adjutant hapo Chuoni. Afisa huyo bila hata kumsikiliza askari huyo na bila hata kuangalia cheti toka kwa daktari kama kweli amepewa mapumziko. Pamoja na kulalamika kuwa anayo ED bila huruma na bila ubinadamu na bila kutumia busara na bila kutumia akili kama afisa wa polisi mwenye cheo na madaraka makubwa kama hayo. Afisa huyo aliamuru askari huyo awekwe mahabusu kwa kosa hilo. Kitendo cha kuwekwa mahabusu askari huyo kilipelekea afya yake kubadilika ghafla na akiwa ndani ya mahabusu hiyo ni wenzake ambao walitoa taarifa kuwa kuna mgonjwa ndani amezidiwa na ndipo askari waliokuwa zamu wakatoa taarifa na kumkimbiza hospital ambako ndiko alikotwaliwa na Muumbaji na ikwa ndiyo mwisho wake.
Kutokana na hali hiyo wanafunzi waliopo Chuoni hapo wamehuzunika sana na baadhi yao wamesikika wakisema ni vyema mkuu wa jeshi afanye uchunguzi wa kina wa swala hilo. Inasemekana pia afisa huyo ameonyesha kutokuwa na uelewa wa maamuzi yake katika kila kona ya chuo hicho na kuonekana kama antafuta sifa au kujipendekeza kupandishwa cheo haraka. Pamoja na hayo wameomba kwamba mara mkuu wa polisi atakapofika chuoni hapo wiki hii kuhitimisha mafunzo ni vyema akaondoka na ofisa huyo na kwenda kumpa kazi nyingine huku akifanya uchunguzi wa jambo hilo. Kuendelea kuwepo hapo chuoni ni kuharibu nidhamu ya askari na jeshi zima la polisi. Kitendo cha kumuweka askari mwenzake mahabusu huku akiwa mgojwa na ugonjwa ambao tayari daktari amethibitisha ni kufundisha nini askari ambao watakwenda sasa kuwa karibu na wananchi na endapo watamkamata mwananchi ana kosa na ni mgonjwa je atasalimika. Naomba ndugu zangu hasa waandishi wa habari mlioko humu mnisaidie kupaza sauti ili tukomeshe tabia kama hizi. huyu ni kiongozi ambaye anatoa mafunzo kwa askari wa nchi nzima. je kuna haja ya ofisa huyo kuendelea kuwepo chuoni hapo? Tafadhalini tusaidiane.
 
Hayatuhusu hata kidogo. Mwambie huyo kaka yako hajakomaa kama askari.
 
Hayatuhusu hata kidogo. Mwambie huyo kaka yako hajakomaa kama askari.

mimi nilishafuta kwamba kuna binadamu anaweza kuwa polisi. Huwa nahisi napishana na midudu fulani inayotembelea miguu miwili na imevaa sare.
 
Poleni kwa msiba!
Kwanza upo kwenye hiyo kozi na sio kaka yako!
Pili jeshini unatekeleza adhabu kwanza kulalamika badae!
Tatu tamu kwa nguruwe kwa binadamu chungu ati!
Angalao sasa mtoa mada keshajua tamu ya chungu!
 
Umekuwa Guest kwa Muda mrefuuu....post yako ya kwanza tu, umekuja na lawama! Tusalimu basi hata kwanza, ndo ustaarabu wetu kusalimiana kabla ya kupeanza taarifa za matatizo!
 
Kazi yake mola haina makosa kamanda!hili ni jambo la kawaida amekufa tena akiwa amepumzika ataenda kuwapigisha kwata malaika huko mbinguni!hebu kumbuka arusha walivyotutesa kumbuka iringa kifo cha mwanahari kumbuka mwanza morogoro singida mabwepande kule dar hii yote ni vitu vizito vinaua geukaneni kabisa tena bora amekufa huenda angekuja kuua tena vijana wetu na huenda aliua mmoja ya wale waandamanaji kule arusha akiwa katokea manyara
 
Pole sana wafiwa napiga picha ndio mtoto wako au ndugu yako wa karibu...anakufa kwa upuuzi wa limtu fulani ambae anafikiri afya ya mtu inapimwa kwa ukatili wake,Mungu atamlipa hapa hapa duniani.....nidhamu ya jeshi imepotea na uzalendo ulishaisha zamani,sasa imekuwa mazoea tu,utakuta huyo 'muuaji'atapandishwa cheo soon!!
 
Yalisha wahi kunenwa Maskini tuta uwana wenyewe...... ndio kama hivyo
 
vigezo vya kujiunga na jeshi la Polisi lazima uwe na element za uuaji, ujambazi na uhalifu uliokubuhu
 
Ukimtendea mwenzio mabaya nawe utapata ubaya....

Wewe uko mafunzoni kwa nini usimwambie Mkuu wako unataka raia wapaze sauti hali uanajau haitofika kokote na zaidi wewe ndio utakae tumwa kuzimwangosi hizo sauti
 
:embarassed2:Habari ambazo nimezipata toka kwa kaka yangu anayehudhuria mafunzo ya kupandishwa cheo katika Chuo Cha Polisi Moshi (CCP). Ni kuwa siku ya jana chuoni hapo ilikuwa ni majonzi makubwa kwa askari wanaohudhuria course mbalimbali chuoni hapo. Majonzi hayo na vilio vilitawala pale mwili wa askari mwenzao aliyekuwa akihudhuria mafunzo ya ngazi ya corpolo kutokea mkoani Manyara. Askari huyo alifariki dunia kwa prssure na kisukari. Sasa basi kilichipelekea kuwepo na vilio vingi na lawama za hapa na pale ni kwamba: Askari huyo ambaye kwa sasa ni marehemu na mungu amlaze mahali pema, hakuhudhuria kipindi chuoni hapo kwa vile alikuwa na mapumziko aliyopewa na daktari wa Chuo ( ED ). Baada ya kutafutwa wasiohudhuri vipindi ikaonekana na yeye hakuhudhuria hivyo Afisa mmoja aliyetajwa kwa jina la JB IBRAHIM mwenye Cheo cha Mrakibu mwandamizi (ASP), na ambaye ni Adjutant hapo Chuoni. Afisa huyo bila hata kumsikiliza askari huyo na bila hata kuangalia cheti toka kwa daktari kama kweli amepewa mapumziko. Pamoja na kulalamika kuwa anayo ED bila huruma na bila ubinadamu na bila kutumia busara na bila kutumia akili kama afisa wa polisi mwenye cheo na madaraka makubwa kama hayo. Afisa huyo aliamuru askari huyo awekwe mahabusu kwa kosa hilo. Kitendo cha kuwekwa mahabusu askari huyo kilipelekea afya yake kubadilika ghafla na akiwa ndani ya mahabusu hiyo ni wenzake ambao walitoa taarifa kuwa kuna mgonjwa ndani amezidiwa na ndipo askari waliokuwa zamu wakatoa taarifa na kumkimbiza hospital ambako ndiko alikotwaliwa na Muumbaji na ikwa ndiyo mwisho wake.
Kutokana na hali hiyo wanafunzi waliopo Chuoni hapo wamehuzunika sana na baadhi yao wamesikika wakisema ni vyema mkuu wa jeshi afanye uchunguzi wa kina wa swala hilo. Inasemekana pia afisa huyo ameonyesha kutokuwa na uelewa wa maamuzi yake katika kila kona ya chuo hicho na kuonekana kama antafuta sifa au kujipendekeza kupandishwa cheo haraka. Pamoja na hayo wameomba kwamba mara mkuu wa polisi atakapofika chuoni hapo wiki hii kuhitimisha mafunzo ni vyema akaondoka na ofisa huyo na kwenda kumpa kazi nyingine huku akifanya uchunguzi wa jambo hilo. Kuendelea kuwepo hapo chuoni ni kuharibu nidhamu ya askari na jeshi zima la polisi. Kitendo cha kumuweka askari mwenzake mahabusu huku akiwa mgojwa na ugonjwa ambao tayari daktari amethibitisha ni kufundisha nini askari ambao watakwenda sasa kuwa karibu na wananchi na endapo watamkamata mwananchi ana kosa na ni mgonjwa je atasalimika. Naomba ndugu zangu hasa waandishi wa habari mlioko humu mnisaidie kupaza sauti ili tukomeshe tabia kama hizi. huyu ni kiongozi ambaye anatoa mafunzo kwa askari wa nchi nzima. je kuna haja ya ofisa huyo kuendelea kuwepo chuoni hapo? Tafadhalini tusaidiane.

Acha siasa hapo ni jeshini Kwani ni bora kuvuja jasho jingi wakati huu wa amani ili wakati wa nchi kuingia vitani iwe jambo dogo kwao
 
Du si kesi ya kwao waache wataimaliza tu maana hapo hakuna chama cha siasa
 
Yaani mimi nimefikiri amechukua bomu akamlipua kama mbwa. Nimefikiri amepigwa kwa kitu kizito hivyo mkuu wa chuo na wenziwe wanafanya uchunguzi kuona ni nini kimetokea.
Kwa kweli polisi hawana heshima yeyote hapa Tanzania kwa sasa. Wanaonekana kama mbwa wanaojipitisha uchi mitaani wakiombaomba rushwa bila kujali wanaipata kwa mjane, mzee, mgonjwa, mtoto yatima, au nani. Wanabanbikizia watu makesi na kuwatupa rumande bila kuangalia hali zao. Vilio vya hao wajane, wazee, wagonjwa, na wenye shida wanaotendewa unyama na polisi kinamfikia Mola. Tuache utani hata Biblia inasema kilio cha mjane na yatima kitanifikia. Kilio cha watoto wa Mwangosi, wale wanaouwawa huku Tarime, wale waliouawa kule Dar wakitokea Morogoro, kina Munishi wa Bomang'ombe, na wengine wengi tu kinamfikia Mungu. Huwezi kumwua mtu asiye na hatia eti umetumwa kutetea mikate ya mafisadi au unataka kumwibia then unamsingizia jambazi. Damu za watu zinawalilia sasa mtauana wenyewe kwa wenyewe wala msilalamike huku jamvini!
 
Back
Top Bottom