Kasheshe la Mafuta: Dar kimeanza kuwaka, vituo kadhaa vyaanza kutoa mafuta!

Naamini pamoja na kauli hii umegundua kuwa HALI SI NZURI na hata kuwashawishi watu wakuelewe ni ngumu sana.

Hapa ndo inapokuwa ngumu mtu kuitetea serikali, yawezekana wana vitu vya kuufanya umma uiamini lakini wamevikalia wao, wanabaki kudai 'kazi ya wananchi ni kulalamika tu' sijui wakitarajia tukavunje makabati yao kujua nini kipo kwenye files?

Pole mkuu, inachosha kuwatetea hawa jamaa.

Mkuu mie hata siamini kama wanachochote kwenye makabati, tatizo lao kubwa ni wakati wa kushughulikia matatizo akili yao inakuwa kwenye 10%, kamwe suluhisho la kweli la matatizo haliwezi kupatikana
 
Nchi inayumba - CCM haina mwongozo na inasambaratika! Ilikuwa ni comedy ya CCM tu jana huko Bungeni Dodoma. Makamba Mbunge wa CCM na Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini apendekeza hoja juu ya swala hili.

Waziri Mkuu akaa kimya; Kamati ya Uongozi ya Bunge yakubaliana na wazo wa kujadili hoja; Wabunge wajadili hoja kwa jazba kubwa - mwishowe waziri Ngeleja [CCM] atoa tamko la Serikali.

Jee kulikuwa na haja ya kwenda through usanii huu - Waziri Ngeleja anangojea mpaka hoja iletwe ndio atoe Tamko la Serikali kwa issue ya dharura kwa taifa kama hili? CCM haioni kama hii ni hali ya hatari kwa nchi? Serikali na CCM wameshindwa kuendesha nchi - Nafikiri kuna haja ya kuwa na Tahariri Squarev ya Tanzania.
 
Serikali ya ccm haiwezi kuwagusa wafadhiri wa chama chao lasivyo makubwa zaidi yatafumuka na watakuwa uchi wa mnyama. Kama wangekuwa watu wakawaida, mbona tamko la EWURA lilikuwa linatosha? kULIKUWA NA HAJA GANI WAZIRI KUTOA TAMKO LA PILI WAKATI TAASISI ILIYO CHINI YAKE ILISHATOA TAMKO KAMA HILO NA HALIKUTEKELEZWA?

Nadhani pia kwa mjibu wa ngereja, solution yao ni kuwapa lesseni sijui COPEC wafanye biashara hiyo wakati walikuwa wamekalia maamuzi haya kwa miaka minne sasa. Hii inaonyesha wafanyabiashara hawa wana nguvu na ndiyo wenye maamuzi ya nani apewe leseni ya biashara ya mafuta. Kama ndivyo inategemea COPeC watapata wapi hela ya harakaharaka ya kuleta mafuta wakati watoaji wa hiyo hela ni viongozi walewale ambao ndiyo wenye makampuni yaliyogoma?

Hapa kuna sinema fulani tusubiri kwa kuwa sisi ni wapole na wanyenyekevu wa moyo mapaka itakapoisha.

Natamani kuchangia lakini najizuia nisije nikaongea bila busara.kwakuwa siwezi kusema yaliyoko moyoni naomba mgomo wa wauza mafuta uendelee mpaka kieleweke.Labda kwa njia hii watanzania watapata akili za ziada na kufanya maamuzi magumu.
 
Hivi huna habari kuwa wanajeshi na sisiemu lao moja. Kwani hujasikia yale ya ufisadi wa trilioni tatu, na lile la kila mwanajeshi kukatwa Tshs 500 kwenye mshahara.

Mbona wamekaa kimya sembuse haya yasiyowahusu, wao cha msingi wanapanda ile mibasi iliyotaifishwa (ambayo yalikuwa ya fisadi waitara) ukichukulia wao wana visima vyao kwenye makambi yao ya jeshi.

HAYAWAHUSU BAAAAAAAAABU, siyo masihara jamani, inaudhi sana.
 
Naona tumuache MUNGU wa watu apumzike, haya bado yako with our reach, haya yanayotokea hata shetani hahusiki ni uendawazimu wa wajinga wachache tu....hebu taumua leo tufanye kitu cha maana uone baraka toka mbinguni zitakavyomiminika, kwa mfano;

Unasubiri MUNGU aingilie kati hata suala la Wabunge kupelekwa na Barrick kwenda kumkagua Barrick? Yaani mwizi akutumie Tax akulipe na gharama zote za usumbufu ili ukamkamate....washenzi wakubwa wale, nauridia tena, washenzi wakubwa wale, na tena wapuuuzi wakubwa wale. Na waalaaniwe, mimi ningeomba zile ndege zingeanguka wafe wote.
Eee Mungu Baba, sikia kilio changu, hali hii ieendelee hivi hata miezi sita, watanzania wengi wamekuwa wagumu kutambua kuwa CCM imeshindwa, wanahitaji kujinza kwa vitendo zaidi hivyo hali hii itasaidia watanzania kutambua ukweli.
 
Leo kuna promosheni ya matusi kwa serikali tu....itumie fasta, fursa hii inaisha baada ya mgomo wa mafuta kuisha miezi miwili ijayo, wapuuzi wakubwa hawa, ndio maana wanafikiria kwa kutumia naninihii
Natamani kuchangia lakini najizuia nisije nikaongea bila busara.kwakuwa siwezi kusema yaliyoko moyoni naomba mgomo wa wauza mafuta uendelee mpaka kieleweke.Labda kwa njia hii watanzania watapata akili za ziada na kufanya maamuzi magumu.
 
Kelele zote za jana juu ya uuzaji wa mafuta zimeishia wapi??leo naona wamekaa wanakula kiyoyozi wameshamaliza kazi ilhali mgomo bado unaendelea na wananchi tunaendelea kutaabika

na hii ilitokea hata kwenye bajeti ya uchukuzi hivi juzi tuu,kelele nyingii mpaka wengine wakasema mawaziri wanyongwe lakini mwisho wakalegea na kukubali bajeti ile ikapita kilaini

ndio maana dr.didas masaburi akasema wabunge wanatumia makalio kufikiria na sio akili,na mimi naanza kuamini maneno ya dr,didas masaburi wabunge wetu huenda wanatumia makalio kuzungumza ,kama walivyopiga kelel jana na leo hali bado ni ngumu ila wao wamekaa kimya wanakula kiyoyozi sisi tuendelee kufa

acheni kutumia makalio tumieni akili
 
Kiukweli mambo yamekuwa magumu, huwa najiuliza hivi watz tumerogwa au ni laana? Huwezi amini tumekaa kimya, tunaongelea kwa keyboard na smartphone. Mida hii tulitakiwa tuweko barabarani kuupinga huu ukoloni mamboleo.

Tanzania si nchi huru, uhuru wetu uko wapi? Hatuna maji, hatuna makazi bora, hatuna nishati, hatuna chakula, tumebaki kufurahia mitumba michafu na wageni kuchukua ardhi yetu. People we need to rise and say NOOOO, to this kind of humiliation.
 
Ninatokea kibamba kuelekea town. Vituo vyooote havijafunguliwa.

Hivi ule mkwara wa ngeleja ulikuwa geresha tuuuuuu? Aaaaagh!


attachment.php


Mh Kikwete bado anatafakari.
 

Attachments

  • 262893_196193920440523_187249878001594_536404_2580864_n.jpg
    262893_196193920440523_187249878001594_536404_2580864_n.jpg
    9.5 KB · Views: 132
Barking dogs never bite! Tanzania hakuna waandamanaji wa kuitoa CCM madarakani. Ni watu wanaoweza kutoa matusi mitandaoni na kupiga makelele meeengi bila utekelezaji. Labda mkodi waarabu wawasaidie.
 
Hv chadema wapo wapi muda kama huu?me sielewi kwann hawajaanda maandamano mpk saiv,zaidi ya siku 7??au wao maandamano wanaandaa kma wakiwa wanataka madaraka tu? Suala la jailo wapo kimya suala la mafuta wapo kimya,jaman mananiangusha chadema,andaeni maandamano jmn tuwashinikize hawa wahuni watoke madarakani,imefika muda tuwe kama watu wa london kwa kuchoma hivi vituo vya mafuta na mali za mafisdi pai

Tuliza Munkari mdogo wangu. Naweza kukuthibitishia kuwa weekend hii wabunge wote wa CHADEMA watakuwa na kikao kizito eidha Dar au Dodoma. Nadhan baada ya hapo tutaelezwa maandamano ni lini.
 
Nashukuru kwa comment hii - Maana tangia saa 11 alfajiri nipo hapa Africana kwenye "foleni ya mafuta"!

Tumedhubutu - Tumeweza - Tunasonga Mbele!

Mbona JK aliweza kuita wazee wa dar es salaam akawakoromea wafanyakazi kwa mkwala na shubunga, leo mbona anashindwa kuwachimba mkwala wenye vituo vya mafuta? Hii issue ingemfaa kamanda Lowassa, he is good on this, basi tu sio PM tena, I love Lowassa darely.

Aliwatimulia mbali City water, that was bold decesion, angekuwa PM hii issue ya mafuta ingeshakuwa history. Pinda sura ngumu loh, hakuna kitu yupo yupo tu.

Inachukua miezi kadahaa kwa shehena ya mafuta kuingia nchini yakiagizwa leo, leseni inayotolewa leo inamfaa nini mtu mmweney shida ya mafauta sasa hivi, that is not how to solve problem
 
Watanzania kusema inatosha sio dhambi, kumbukeni kupinga udhalimu ni utiifu kwa mungu. kwanini tumekuwa wajinga kiasi hiki, raisi wa nchi yupo au amekwenda likizo? madhara ya nidhamu ya uoga ndiyo yanayotugharimu, tunaumia huku tukinung'unika. eeh mungu tusaidie!!!!!
 
Mi nadhani ushauri wa zitto uzingatiwe jeshi litumike vituo na maghala yafunguliwe na mafuta yatolewe bure. La sivyo wananchi tuandamane tuvamie vituo hivyo na kujichotea mafuta kwa nguvu.

short term solutions! what about long term plan? Inasemekana viongozi wengi wa serikali hii dhalimu wako kwenye payroll ya wawekezaji wa mafuta, wanalipwa monthly.

Ndo hao hao tunategemea watoe maamuzi magumu kuhusu wawekezaji!!! inawezekana kweli? Kuna wabunge wawili last two weeks walikuwa wanajigamba bungeni kuwa wao ni waingizaji wakubwa wa mafuta nchini i.e.

Kaijage na mwenzake wa asili ya kiasia jimbo moja la shinyanga/mwanza. do you think hawa walikuwa pamoja na kauli za akina Zitto bungeni??definetely they are not. Conflict of interest kila sehemu...hii ndo serikali legelege, kama kuna mtu duniani hajui serkali legelege aje TZ leo ataijua kisawaswa.

My wish ni kwamba wagome completely ili hata watu wanaosema siasa ni mchezo mchafu wafeel impact yake...watu hawapigi kura, wanapigia mijitu midhalimu, hawajihusishi na chochote kuhusu nchi ila ni kujijali wenyewe.....sasa tukikosa umeme kwa pamoja na wao washindwe kuwasha magenerator, watatia akili.
 
Back
Top Bottom