RushwaNiAduiwaHaki
Member
- Jan 25, 2012
- 13
- 2
Katika mzunguko wa maisha, nilibahatika kukutana na binti mmoja ambaye taratibu tulianza urafiki wa kawaida, kutokana na mfumo wa urafiki wetu ilifika mahali tukakubaliana kuanzisha uhusiano wa kimapenzi.Lakini wakati uhusiano huu wa kimapenzi ukiwa ndio umeanza nililazimika kuendelea na shughuli na ratiba zangu na nikajikuta nipo mbali na yeye kidogo. Hilo halikuathiri mahusiano yetu kwani kila mmoja aliridhia kuwa ni katika harakati za kujiletea maendeleo. Kipindi tulikutana, ilikuwa ni jijini Mwanza, lakini mimi nikiwa mkazi wa Kilimanjaro na yeye akiwa mkazi wa Njombe Iringa. Siku zilipita na mapenzi yaliendelea na tuli-share kila kitu kuhusiana na maisha yetu, background, interest na hobbies pamoja na matarajio kulingana na kudra za Mwenyezi Mungu. Kwa upande wangu nilikuwa muwazi kabisa bila kuficha nikimueleza kila kitu kuhusiana na mimi, na yeye alinieleza na nilimuamini ingawa siwezi fahamu kuwa alinieleza yote na kama yalikuwa ya kweli. Siku, wiki na miezi ikapita tukiwa na mawasiliano mazuri na marafiki zetu wa karibu wa pande zote mbili wakifahamu kila kinachoendelea. Kuna mambo ilibidi niyabadilishe katika misimamo yangu ili at least kukidhi misimamo yake, Mathalani, Yeye alitaka tuoane 2015 mie nikaona itakuwa mapema sana lakini baada ya majadiliano tukakubaliana iwe 2017 na hapa ni baada ya kuangalia ni nini kinahitajika ili mtu afunge ndoa kwa kina na kuona kuwa Mungu akitubariki basi 2017 tutakuwa tumekamilisha kila kitu, Kuhusu uzazi wa mpango yeye alikuwa anapendelea zaidi watoto watatu, mie nilipendelea mtoto mmoja, na mwisho tulijadiliana na kukubaliana tutazaa watoto wawili kwa kudra za Mwenyezi Mungu,Na pia alitaka apate mtoto wa kwanza kabla ya ndoa, hilo nililipinga kabisa, kwa sababu ni kinyume na maadili yetu.
Muda ulipita na ikafikia wakati anataka kwenda kwao Iringa, nikamuambia kwa kuwa unao ndugu Moshi basi ni vyema ukapitia Moshi angalao tusalimiane kabla hajaenda Iringa kutokea mwanza. Alikubali, lakini tatizo likaja ni kuwa alitaka kufikia ninapoishi mimi katika chumba cha kupanga, nilipinga hilo wazo kwa kuwa niliona si jambo la kimaadili kufanya ''cohabition'' na mchumba wangu huyu, lakini baada ya kusisitiza sana nililazimika kukubaliana naye na ikafika siku akaja na kuishi na mimi kwa siku 5 badala ya 3 tulizopanga awali. Kwa uwazi bila kificho ni kuwa tuliishi kama mtu na mke wake ingawa kila mara nilijitahidi kuhakikisha natumia CONDOM katika tendo la uzinifu. Siku ziliisha na alielekea kwao Iringa, na mapenzi yakaendelea kama kawaida[Long Distance Relationship]. Siku, wiki na mwezi ukapita na nikapata kazi nyingine jijini Arusha na Dar es Salaam, na nikashauriana naye na mwisho niliamua kufanya Arusha, siku c nyingi nikapata kazi nyingine yenye maslahi zaidi katika Mkoa wa Rukwa, Sumbawanga mjini, nilishauriana naye na kila jambo likawa sawa, lakini kabla sijaenda kureport kwenye kazi yangu mpya, nikaanza kuona mabadiliko kwenye mahusiano yetu, kuna siku nilimpigia simu ikawa ipo bussy kwa masaa matatu na ilikuwa usiku, niliamua kumuandikia sms kumtakia usingizi mwema na nikalala, na kesho yake akanijibu kwa sms kuwa sms yangu ameiona na akatoa maelezo kuwa usiku ule alikuwa amemuazima simu mdogo wake, nami nikaridhia kwa moyo mmoja ingawa wala sikuomba maelezo yale, labda kwa sababu aliona missed call zangu nyingi sana. Lakini, hali ikaendelea kuwa hivyo, na nikataka maelezo kwani hali ilibadilika sana, na akaniambia kuna matatizo nyumbani aki-settle ataniambia. Sikuona tatizo sana, ila baadaye alinieleza kuwa kuna kaka ambaye walianza uhusiano tangu 2005, baadaye waka-break up kwa sababu ni yeye ndiye alimkosea yule kaka na alilazimika kumuomba msamaha. Akasema kuwa kaka alimsamehe lakini mahusiano hayakurudia tena, sasa wakati huu alipoenda nyumbani ndio kaka amemfuata akamuambia waendelee. Kwa kuwa tayari kaka alikuwa anafahamika nyumbani kwao na alimtambulisha huyo binti kwao basi inamuwia vigumu kuamua. Nikajitahidi kuwa mpole, na nikamuambia,,,Wewe umeamua nini sasa? Akaniambia bado hajaaamua, nami nikamuambia afanye uamuzi sahihi juu ya hilo jambo, nikaenda mbali zaidi kumueleza kuwa,''Hakuna uamuzi muhimu kama uamuzi wa ni nani utakayeoana naye katika maisha''. Nikamuambia pia na uamuzi sahihi si lazima uwe upande wangu, unaweza ukawa kwangu au against mimi. Lengo langu hapa, ilikuwa ni kuangalia ni kiasi gani dada huyu ananipenda!! Na ikumbukwe kuwa, katika uhusiano wetu hakuwahi kuniambia kabisa hii story. Nikiwa tayari nipo Sumbawanga, na yeye akiwa njiani kurudi Mwanza nikamuuliza ameamua nini? Akaniambia nisubiri ataniambia, nikawa nimeelewa kila kinachoendelea, na nikaendelea kutumia njia za kifalsafa kufahamu ukweli, na ndipo akaniambia kuwa ''Inabidi iwe hivyo, kwa sababu alitambulishwa na kaka alikuwa tayari kutoa mahari kipindi hiki lakini akaahirisha mpaka mwakani, na Mungu akijalia atatoa hiyo mahari''.Na akaendelea kunidanganya kuwa,'Atanipenda milele daima, kwa kuwa alinipokea kwa mikono miwili' nami nikaona isiwe shida, nimpishe aendelee na maisha na mie njipange kizingine, kwa sababu haya maisha yapo tuu. Nikamwambia, nakutakia kila la heri and ''You'll Never Walk Alone''
Muda ulipita na ikafikia wakati anataka kwenda kwao Iringa, nikamuambia kwa kuwa unao ndugu Moshi basi ni vyema ukapitia Moshi angalao tusalimiane kabla hajaenda Iringa kutokea mwanza. Alikubali, lakini tatizo likaja ni kuwa alitaka kufikia ninapoishi mimi katika chumba cha kupanga, nilipinga hilo wazo kwa kuwa niliona si jambo la kimaadili kufanya ''cohabition'' na mchumba wangu huyu, lakini baada ya kusisitiza sana nililazimika kukubaliana naye na ikafika siku akaja na kuishi na mimi kwa siku 5 badala ya 3 tulizopanga awali. Kwa uwazi bila kificho ni kuwa tuliishi kama mtu na mke wake ingawa kila mara nilijitahidi kuhakikisha natumia CONDOM katika tendo la uzinifu. Siku ziliisha na alielekea kwao Iringa, na mapenzi yakaendelea kama kawaida[Long Distance Relationship]. Siku, wiki na mwezi ukapita na nikapata kazi nyingine jijini Arusha na Dar es Salaam, na nikashauriana naye na mwisho niliamua kufanya Arusha, siku c nyingi nikapata kazi nyingine yenye maslahi zaidi katika Mkoa wa Rukwa, Sumbawanga mjini, nilishauriana naye na kila jambo likawa sawa, lakini kabla sijaenda kureport kwenye kazi yangu mpya, nikaanza kuona mabadiliko kwenye mahusiano yetu, kuna siku nilimpigia simu ikawa ipo bussy kwa masaa matatu na ilikuwa usiku, niliamua kumuandikia sms kumtakia usingizi mwema na nikalala, na kesho yake akanijibu kwa sms kuwa sms yangu ameiona na akatoa maelezo kuwa usiku ule alikuwa amemuazima simu mdogo wake, nami nikaridhia kwa moyo mmoja ingawa wala sikuomba maelezo yale, labda kwa sababu aliona missed call zangu nyingi sana. Lakini, hali ikaendelea kuwa hivyo, na nikataka maelezo kwani hali ilibadilika sana, na akaniambia kuna matatizo nyumbani aki-settle ataniambia. Sikuona tatizo sana, ila baadaye alinieleza kuwa kuna kaka ambaye walianza uhusiano tangu 2005, baadaye waka-break up kwa sababu ni yeye ndiye alimkosea yule kaka na alilazimika kumuomba msamaha. Akasema kuwa kaka alimsamehe lakini mahusiano hayakurudia tena, sasa wakati huu alipoenda nyumbani ndio kaka amemfuata akamuambia waendelee. Kwa kuwa tayari kaka alikuwa anafahamika nyumbani kwao na alimtambulisha huyo binti kwao basi inamuwia vigumu kuamua. Nikajitahidi kuwa mpole, na nikamuambia,,,Wewe umeamua nini sasa? Akaniambia bado hajaaamua, nami nikamuambia afanye uamuzi sahihi juu ya hilo jambo, nikaenda mbali zaidi kumueleza kuwa,''Hakuna uamuzi muhimu kama uamuzi wa ni nani utakayeoana naye katika maisha''. Nikamuambia pia na uamuzi sahihi si lazima uwe upande wangu, unaweza ukawa kwangu au against mimi. Lengo langu hapa, ilikuwa ni kuangalia ni kiasi gani dada huyu ananipenda!! Na ikumbukwe kuwa, katika uhusiano wetu hakuwahi kuniambia kabisa hii story. Nikiwa tayari nipo Sumbawanga, na yeye akiwa njiani kurudi Mwanza nikamuuliza ameamua nini? Akaniambia nisubiri ataniambia, nikawa nimeelewa kila kinachoendelea, na nikaendelea kutumia njia za kifalsafa kufahamu ukweli, na ndipo akaniambia kuwa ''Inabidi iwe hivyo, kwa sababu alitambulishwa na kaka alikuwa tayari kutoa mahari kipindi hiki lakini akaahirisha mpaka mwakani, na Mungu akijalia atatoa hiyo mahari''.Na akaendelea kunidanganya kuwa,'Atanipenda milele daima, kwa kuwa alinipokea kwa mikono miwili' nami nikaona isiwe shida, nimpishe aendelee na maisha na mie njipange kizingine, kwa sababu haya maisha yapo tuu. Nikamwambia, nakutakia kila la heri and ''You'll Never Walk Alone''