kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
KIPA wa Simba na timu ya taifa 'Taifa Stars', Juma Kaseja amesema hawezi kuzungumza chochote juu ya suala lolote linalohusu klabu yake au timu ya taifa.
Nimeamua kufumba mdomo na kuuchunga sana ili nisiongee kwani kuna watu wana mpango wakunichafua kupitia mdomo wangu, kila ninapofungua mdomo kuzungumza wananilisha ya kwao hivyo kwa sasa sihitaji kuzunguza chochote mpaka ligi itakapoanza,alisema Kaseja.
Msimamo huo wa Kaseja umekuja siku chache baada wadau mbalimbali wa soka nchini kudai mchezaji huyo ameshuka kiwango na kwamba yawezekana akakosa hata usajili katika timu yake ya Simba msimu ujao.
Ingawa Kaseja ni kati ya magolikipa wazuri nchini wenye rekodi nzuri ya kufanya vizuri, lakini kauli na tabia za watanzania za kumzomea mchezaji kila anapofanya kosa uwanjani ndiyo inayomfanya mchezaji huyo abebeshwe lawama kila kukicha.
Wakati huohuo winga wa Taifa Stars, Julius Mrope amesema wachezaji wa Tanzania ni wavivu kiasi cha kushindwa kujituma uwanjani.
Mrope alitoa kauli hiyo ikiwa ni siku moja tangu alipoitwa katika timu ya taifa kwa ajili ya kuziba nafasi ya Mrisho Ngassa ambaye ni majeruhi wa paja.
Wachezaji watanzania hawajitumi kiasi kwamba wamekuwa wavivu ndiyo maana wakipewa nafasi wanashindwa kuzitumia ipasavyo na hii ndiyo sabu Mrisho Ngassa anawazidi na ang'ara kila kukicha,alisema Mrope.
Alisema yeye binafsi anamkubali Ngassa kwa sababu ni mchezaji mwenye kiwango cha juu kuliko wachezaji wote nchini na sababu ya kuwa juu ni kwa kuwa anajituma kila anapokuwa uwanjani.
Hii ni mara ya pili kwa Mrope kuitwa katika kikosi cha Stars ya Kocha Jan Poulsen, mara ya kwanza aliitwa katika mechi ya kirafiki dhidi ya Palestina iliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na Stars kushinda bao 1-0 lililofungwa na Ngassa.
Nimeamua kufumba mdomo na kuuchunga sana ili nisiongee kwani kuna watu wana mpango wakunichafua kupitia mdomo wangu, kila ninapofungua mdomo kuzungumza wananilisha ya kwao hivyo kwa sasa sihitaji kuzunguza chochote mpaka ligi itakapoanza,alisema Kaseja.
Msimamo huo wa Kaseja umekuja siku chache baada wadau mbalimbali wa soka nchini kudai mchezaji huyo ameshuka kiwango na kwamba yawezekana akakosa hata usajili katika timu yake ya Simba msimu ujao.
Ingawa Kaseja ni kati ya magolikipa wazuri nchini wenye rekodi nzuri ya kufanya vizuri, lakini kauli na tabia za watanzania za kumzomea mchezaji kila anapofanya kosa uwanjani ndiyo inayomfanya mchezaji huyo abebeshwe lawama kila kukicha.
Wakati huohuo winga wa Taifa Stars, Julius Mrope amesema wachezaji wa Tanzania ni wavivu kiasi cha kushindwa kujituma uwanjani.
Mrope alitoa kauli hiyo ikiwa ni siku moja tangu alipoitwa katika timu ya taifa kwa ajili ya kuziba nafasi ya Mrisho Ngassa ambaye ni majeruhi wa paja.
Wachezaji watanzania hawajitumi kiasi kwamba wamekuwa wavivu ndiyo maana wakipewa nafasi wanashindwa kuzitumia ipasavyo na hii ndiyo sabu Mrisho Ngassa anawazidi na ang'ara kila kukicha,alisema Mrope.
Alisema yeye binafsi anamkubali Ngassa kwa sababu ni mchezaji mwenye kiwango cha juu kuliko wachezaji wote nchini na sababu ya kuwa juu ni kwa kuwa anajituma kila anapokuwa uwanjani.
Hii ni mara ya pili kwa Mrope kuitwa katika kikosi cha Stars ya Kocha Jan Poulsen, mara ya kwanza aliitwa katika mechi ya kirafiki dhidi ya Palestina iliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na Stars kushinda bao 1-0 lililofungwa na Ngassa.