MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,565
- 836
Somoe Ng`itu
Hatimaye juzi kipa mahiri nchini, Juma Kaseja alisaini fomu za kujiunga na klabu ya Simba kwa ajili ya kuichezea katika msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara na mashindano ya kimataifa.
Akizungumza jana kwenye ukumbi wa mgahawa wa Hadees, Kaseja, alisema kuwa amesaini mkataba wa miaka miwili na anawataka viongozi, wachezaji, wanachama na mashabiki wa klabu ya Simba kumpa ushirikiano ili aweze kuitumikia vyema timu hiyo.
Kaseja alisema kuwa ameamua kurejea katika klabu yake hiyo ya zamani baada ya kushawishiwa na rafiki yake, Dionis Malinzi na viongozi wa Kamati ya Usajili ya Simba ambayo wote wameridhishwa na uwezo aliokuwa nayo.
"Mimi Juma Kaseja nimesaini mkataba wa miaka miwili wa kuichezea Simba, hii imetokana na ushawishi mkubwa wa rafiki yangu Dionis Malinzi ambaye ameshanifanyia mambo mengi makubwa," alisema Kaseja.
Aliongeza kuwa amefanya maamuzi hayo kutokana na uongozi wa Simba kuonyesha kumkubali na anawashukuru viongozi, wachezaji na wanachama wa Yanga kwa ushirikiano waliompatia katika msimu mmoja aliokuwa anaichezea timu yao.
Alisema pia anaamini yeye ni kipa bora na maamuzi yake ya kuondoka Yanga hayatokani na kuogopa ushindani na Mserbia, Obren Curkovic kama inavyotafsiriwa na baadhi ya wadau wa soka nchini.
Kaseja alisema kuwa yeye ndiye kipa aliyecheza mechi nyingi katika timu hiyo msimu uliopita na kuongeza kuwa hatishwi na maneno yanayosemwa na mashabiki kuhusiana na upinzani uliokuwepo katika nafasi hiyo dhidi ya Obren.
Aliahidi kuwa amerejEa kuisaidia Simba kurejesha heshima yake kwa kufanya vizuri kwenye Ligi Kuu ya Bara na mashindano ya Kombe la Shirikisho mapema mwakani.
NIPASHE
Hatimaye juzi kipa mahiri nchini, Juma Kaseja alisaini fomu za kujiunga na klabu ya Simba kwa ajili ya kuichezea katika msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara na mashindano ya kimataifa.
Akizungumza jana kwenye ukumbi wa mgahawa wa Hadees, Kaseja, alisema kuwa amesaini mkataba wa miaka miwili na anawataka viongozi, wachezaji, wanachama na mashabiki wa klabu ya Simba kumpa ushirikiano ili aweze kuitumikia vyema timu hiyo.
Kaseja alisema kuwa ameamua kurejea katika klabu yake hiyo ya zamani baada ya kushawishiwa na rafiki yake, Dionis Malinzi na viongozi wa Kamati ya Usajili ya Simba ambayo wote wameridhishwa na uwezo aliokuwa nayo.
"Mimi Juma Kaseja nimesaini mkataba wa miaka miwili wa kuichezea Simba, hii imetokana na ushawishi mkubwa wa rafiki yangu Dionis Malinzi ambaye ameshanifanyia mambo mengi makubwa," alisema Kaseja.
Aliongeza kuwa amefanya maamuzi hayo kutokana na uongozi wa Simba kuonyesha kumkubali na anawashukuru viongozi, wachezaji na wanachama wa Yanga kwa ushirikiano waliompatia katika msimu mmoja aliokuwa anaichezea timu yao.
Alisema pia anaamini yeye ni kipa bora na maamuzi yake ya kuondoka Yanga hayatokani na kuogopa ushindani na Mserbia, Obren Curkovic kama inavyotafsiriwa na baadhi ya wadau wa soka nchini.
Kaseja alisema kuwa yeye ndiye kipa aliyecheza mechi nyingi katika timu hiyo msimu uliopita na kuongeza kuwa hatishwi na maneno yanayosemwa na mashabiki kuhusiana na upinzani uliokuwepo katika nafasi hiyo dhidi ya Obren.
Aliahidi kuwa amerejEa kuisaidia Simba kurejesha heshima yake kwa kufanya vizuri kwenye Ligi Kuu ya Bara na mashindano ya Kombe la Shirikisho mapema mwakani.
NIPASHE