Karume1+karume2+karume3=ufalme?

Katika viongozi wote TZ ni Ali Karume pekee alietamka kuwa, iwapo atachaguliwa kuwa Prez Zanzibar ataanzisha serikali ya Mseto. Alisema hayo hata kabla ya Makubaliano ya Muafaka kuwekwa hadharani.

Unazi unawazidi sasa hii ni sera ya CUF hata Balozi Ali hajatamka hayo au kwa msemo wako Kiongozi wa Tz ni anayetoka CCM tu na tunavyowajua CCM tamko la mtu mmoja halisaidii kitu tumeyaona yalotokea Butiama, Mwenyekiti wao alijipiga kifua mbele kuwa atamaliza mzozo wa Znz kazidiwa hoja na Karume sasa ameuzidisha kuwamgogoro zaidi.
 
Kama nimemsoma vizuri huyu Karume ana maana moja mbaya sana.. Yaani kuigawa Zanzibar ktk utawala wa serikali mbili kutokana na mgogoro wa visiwani wenyewe. Huu ni mfano wa Marekani walivoigawa Iraq ktk majimbo ya kiutawala kidini ili wapate kuwatawala hali imeongeza chuki zaidi ktk serikali kuu.
Hivyo basi nawausia Wazanzibar kuwa nia ya Karume ni chafu sana, haihusiani na Muungano wa nchi hizi mbili (bara na visiwani) ila utawala wa serikali ya visiwa vya Zanzibar..
Nafasi ya Zanzibar Kitaifa hakuizungumzia..na ndilo tatizo kubwa la wananchi wapiga kura wa visiwa hivyo sio swala la Uongozi wa visiwa hivi viwili..
Kwa maneno mengine hata muafaka wa mwaka huu ni bomu?
 
Unazi unawazidi sasa hii ni sera ya CUF hata Balozi Ali hajatamka hayo au kwa msemo wako Kiongozi wa Tz ni anayetoka CCM tu na tunavyowajua CCM tamko la mtu mmoja halisaidii kitu tumeyaona yalotokea Butiama, Mwenyekiti wao alijipiga kifua mbele kuwa atamaliza mzozo wa Znz kazidiwa hoja na Karume sasa ameuzidisha kuwamgogoro zaidi.

Hebu soma hapa chini vizuri:
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imeshauriwa kuunda serikali ya umoja wa kitaifa kama suluhisho pekee la kumaliza misuguano ya kisiasa kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF).
Ushauri huo umetolewa jana na Balozi wa Tanzania nchini Italia, Ali Abeid Karume, alipozungumza na waandishi wa habari visiwani hapa. Alisema vyama vikuu vilivyopo Zanzibar ni CCM na CUF ambavyo vina nguvu sawa.

Alisema Zanzibar bila ya kuundwa serikali ya umoja wa kitaifa, hali ya migororo haitaweza kuepukika, kutokana na kuwa CCM kimejikita zaidi katika Kisiwa cha Unguja na CUF kuwa na ngome yake kisiwani Pemba.

Balozi Karume alisema serikali ya umoja wa kitaifa pia itamaliza mpasuko wa kisiasa uliopo hivi sasa, kwani nchi imeshindwa kuwa na maendeleo kutokana na migogoro ya kisiasa isiyokwisha visiwani.

“Watu wengi hawapendi kusema ukweli, lakini ndio ukweli wenyewe ….hali ya kisiasa iliyopo katika visiwa vyetu ni ngumu sana, Pemba CUF ina nguvu sana na CCM ina nguvu Unguja, sasa suluhisho la yote haya ni kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa,” alisisitiza mwanadiplomasia huyo.
 
lazydog,
Nimetumia swala la Karume ili kusherehesha yale yaliyoyangulia maanake sikusema NDIVYO TULIVYO pasipo sababu..

Mkuu nadhani kweli una miss the point hapa pamoja na kuzungusha kwangu kote..Ila basi jiulize mwenyewe kwa nini sisi Waafrika tumeshindwa kwenda mbele?.. haiwezeknai kila nchi duniani hata Vietnam leo wanapuyanga!... Na kama alivyosema mwalimu Adui yetu mkubwa ni Umaskini unaotokana na Uzembe na Kupuuza - Je, how many out there wanakubaliana na hili!..

Waridi uniwie radhi kwa kukuvurugia topic yako.
Hii ni quote toka kwa Augustine Moshi
"...Mwisho, natoa onyo: Hakuna kitu kibaya zaidi ya inferiority complex. Inafisha jumuiya. Wale ambao mnajisikia inferior, basi leleeni hiyo complex kikwenu, msieneze huo ugonjwa kwa wengine."

Umesema una sababu zako, ...nami nimejaribu kueleza sababu zangu. Please understand that I'm not against you, but the view of ALL who misuse the use of those two terms.

Nisingependa mjadala ubadilike, mwenye interest na issue ya NDIVYO TULIVYO aende kwenye thread hii nilokwisha itaja. Zipo nyingine pia, tumia search.
 
Kwa maneno mengine hata muafaka wa mwaka huu ni bomu?

T'aabaan. Muafaka kama ungelikuwa kama walivyotaka CUF (Mh. Seif) bila ya shaka ungekuwa ni BOMU. Kwani ungekuwa muafaka wa kuleta rehma kwa kundi la wachache (viongozi- pengine wa pande zote), lakini sio wa faida kwa wananchi ambao ndio waathirika wakuu wa hali ya hivi sasa. CCM ilichofanya ni kuuokoa muafaka huo (kwa yale mapendekezomya maerekebisho) ili kuurejesha katika njia ya faida kwa wananchi wote badala ya ku-focus kwa viongozi tu na hatma zao, na ndio maana ikataka hatimaye wananchi washirikishwe kwa ukamilifu katika kuamua mustakabali.
 
Hebu soma hapa chini vizuri:

Hii habari unayoinakili ni mahojiano yalofanyika baada ya Balozi Karume kuondoshwa ubalozini Ujerumani akisubiri kupangiwa kazi na Bosi wake Kikwete - mimi niliyaoma mahojiano yote hayo.Kutumia recently citation kutaka kupindisha ukweli haisaidii.
CUF walisema wataunda serikali ya Umoja tokeo wakati wa Kampeni za Uchaguzi.
 
Back
Top Bottom