Josh Michael
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,523
- 77
Salma Said, Zanzibar
KATIKA kile kinachoonyesha kuimarika kwa uhusiano kati ya rais wa Zanzibar, Amani Karume na katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad, viongozi hao wawili jana walikutana tena faragha Ikulu ya Zanzibar.
Habari zilizolifikia gazeti hili jana na kuthibitishwa na mkurugenzi wa mambo ya nje wa CUF, zinasema kuwa kukutana kwa viongozi hao ni mwendelezo wa yale waliyozungumza walipokutana kwa mara ya kwanza Novemba 5 mwaka huu.
"Ni kweli, katibu mkuu wa CUF amekwenda Ikulu na kukutana na Rais Karume. Walichozungumza bado ni siri. Lakini ni mwendelezo wa mazungumzo yao ya awali ya kutafuta maridhiano ya Wazanzibar na kuyaimarisha," alisema Jussa.
Jussa alisema kuwa kama walivyoeleza viongozi hao wakuu wa vyama vikuu vya siasa visiwani Zanzibar, mazungumzo hayo ni endelevu na kwamba hiyo ni hatua ya pili.
Ingawa kilichozungumzwa na viongozi hao kimefanywa siri, taarifa za awali ambazo Mwananchi imezipata zinaeleza kuwa pamoja na mambo mengine, Seif aliwakilisha kwa Karume majina mawili ya wanachama wa CUF ambao chama hicho kimewapendekeza kuwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.
Hata hivyo, habari zaidi zinasema kuwa anayepaswa kuwasilisha majina hayo kwa Rais Karume ni kiongozi wa upinzani kwenye Baraza la Wawakilishi.
Tangu Karume aingie madarakani, Maalim Seif alikuwa hajawahi kukanyaga Ikulu na mara ya mwisho alikwenda kwenye makazi hayo ya rais wa Zanzibar wakati wa utawala wa Dk Salmin Amour.
Ziara ya safari hiyo ilifanyika siku chache baada ya kiongozi huyo wa upinzani kurejea visiwani Zanzibar akitokea katika ziara ndefu ya barani Ulaya, ambako imeelezwa kuwa alieleza hali ya kisiasa inavyozidi kudorora.
Baada ya mazungumzo hayo ya Novemba 5 si Ikulu ya Zanzibar wala CUF iliyotoa taarifa kwa vyombo vya habari wala kwa wanachama wake kuelezea kuwepo kwa mazungumzo kati ya Karume na Seif ambao vyama vyao vina upinzani mkubwa.
Hata hivyo, siku chache baadaye Maalim Seif aliitisha mkutano wa hadhara na kutangaza kumtambua Karume kuwa rais wa Zanzibar, tamko lililoamsha hasira kwa wanachama wa CUF ambao walimzomea.
KATIKA kile kinachoonyesha kuimarika kwa uhusiano kati ya rais wa Zanzibar, Amani Karume na katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad, viongozi hao wawili jana walikutana tena faragha Ikulu ya Zanzibar.
Habari zilizolifikia gazeti hili jana na kuthibitishwa na mkurugenzi wa mambo ya nje wa CUF, zinasema kuwa kukutana kwa viongozi hao ni mwendelezo wa yale waliyozungumza walipokutana kwa mara ya kwanza Novemba 5 mwaka huu.
"Ni kweli, katibu mkuu wa CUF amekwenda Ikulu na kukutana na Rais Karume. Walichozungumza bado ni siri. Lakini ni mwendelezo wa mazungumzo yao ya awali ya kutafuta maridhiano ya Wazanzibar na kuyaimarisha," alisema Jussa.
Jussa alisema kuwa kama walivyoeleza viongozi hao wakuu wa vyama vikuu vya siasa visiwani Zanzibar, mazungumzo hayo ni endelevu na kwamba hiyo ni hatua ya pili.
Ingawa kilichozungumzwa na viongozi hao kimefanywa siri, taarifa za awali ambazo Mwananchi imezipata zinaeleza kuwa pamoja na mambo mengine, Seif aliwakilisha kwa Karume majina mawili ya wanachama wa CUF ambao chama hicho kimewapendekeza kuwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.
Hata hivyo, habari zaidi zinasema kuwa anayepaswa kuwasilisha majina hayo kwa Rais Karume ni kiongozi wa upinzani kwenye Baraza la Wawakilishi.
Tangu Karume aingie madarakani, Maalim Seif alikuwa hajawahi kukanyaga Ikulu na mara ya mwisho alikwenda kwenye makazi hayo ya rais wa Zanzibar wakati wa utawala wa Dk Salmin Amour.
Ziara ya safari hiyo ilifanyika siku chache baada ya kiongozi huyo wa upinzani kurejea visiwani Zanzibar akitokea katika ziara ndefu ya barani Ulaya, ambako imeelezwa kuwa alieleza hali ya kisiasa inavyozidi kudorora.
Baada ya mazungumzo hayo ya Novemba 5 si Ikulu ya Zanzibar wala CUF iliyotoa taarifa kwa vyombo vya habari wala kwa wanachama wake kuelezea kuwepo kwa mazungumzo kati ya Karume na Seif ambao vyama vyao vina upinzani mkubwa.
Hata hivyo, siku chache baadaye Maalim Seif aliitisha mkutano wa hadhara na kutangaza kumtambua Karume kuwa rais wa Zanzibar, tamko lililoamsha hasira kwa wanachama wa CUF ambao walimzomea.