Karume aizima NEC Dodoma

Ngongo

JF-Expert Member
Sep 20, 2008
18,920
31,161
NGUVU ya Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, imeanza kukitikisa Chama Cha Mapinduzi (CCM), na sasa kimeahirisha kikao cha Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) ili kukabili mmeguko wa wajumbe wa Bara na Visiwani uliosababishwa na ushabiki wa baadhi yao kwa Rais Karume.

Duru za kisiasa kutoka ndani ya Sekretarieti ya CCM inayoandaa vikao hivyo zilisema tayari suala la kutaka Uchaguzi Mkuu Zanzibar uahirishwe ili Rais Karume aongezewe muda limewagawa wajumbe wa NEC. Wanaotoka Visiwani wanaunga mkono hoja hiyo; wajumbe wa Bara wanaipinga.

Kutokana na hali hii, wajumbe wa NEC watokao Zanzibar wamekataa kwenda Dodoma kwenye vikao hivyo, hadi wamalize kikao cha Baraza la Wawakilishi, ambacho pamoja na mambo mengine, kitajadili hoja binafsi ya kumtaka Karume aongezewe muda wa kukaa madarakani.

Hoja hiyo inatarajiwa kuwasilishwa na Kiongozi wa Upinzani katika Baraza hilo, Abubakar Khamis Bakary (CUF), anayetaka uchaguzi mkuu visiwani humo uahirishwe, ili Karume apate muda wa kuandaa mazingira mazuri ya uchaguzi.

Hoja hiyo imeanzishwa na makundi ya wana CCM wa Zanzibar, na sasa imekuzwa na uongozi wa CUF, baada ya Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad, kuibebea bango na kuungwa mkono na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohammed.

Uongozi wa juu wa CCM umeshtushwa na ushabiki wa ghafla wa CUF kwa Rais Karume na kuleta mtikisiko ambao umeilazimisha Sekretarieti ya CCM kuahirisha kikao cha NEC hadi wajumbe wa Zanzibar watakapokuwa wamehitimisha mjadala juu ya hatima ya urais wa Karume, ambaye ni Makamu wa Pili wa Mwenyekiti wa CCM.

Vyanzo vya habari vimedokeza kwamba uongozi wa juu wa CCM umesema vikao vya CC na NEC haviwezi kufanyika sasa, kulingana na hali ya sasa ya kisiasa, bila Karume na wapambe wake kushiriki.

Kwa sababu hiyo, Sekretarieti ya CCM, chini ya uenyekiti wa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba, akishirikiana na manaibu katibu wakuu, Saleh Ramadhan Feruzi (Zanzibar) na George Mkuchika (Bara), itafanya vikao hivyo kuanzia Februari 7, mwaka huu.

Kabla ya hapo, ratiba hiyo ya awali ilionyesha kuwa Kamati ya Maadili ilipangwa kukutana Januari 23 asubuhi na siku hiyo hiyo mchana, kungekuwa na kikao cha Kamati Kuu, wakati NEC ilitarajia kukutana kwa siku mbili kuanzia Januari 25 na 26.

Wajumbe wengine wa sekretarieti hiyo ni Katibu wa NEC Taifa wa Oganaizesheni, Kidawa Yusuf Himid, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa Itikadi na Uenezi, John Chiligati, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Bernard Membe na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa Uchumi na Fedha, Amos Makala.

Ratiba ya awali ilionyesha kuwa tayari sekretarieti imeshaketi kupanga ratiba na ajenda za mkutano huo uliotarajiwa kufanyika wiki ijayo.

NEC imeahirishwa na sababu kubwa ni kutaka kuhakikisha wajumbe wote kutoka Zanzibar wanashiriki kikamilifu, maana ratiba ya sasa inagongana na vikao vya Baraza la Wawakilishi, alisema mmoja wa wajumbe wa Sekretarieti ya CCM ambaye hakutaka kutajwa jina lake.

Makamba alipoulizwa kwa njia ya simu kuhusu kubadilishwa kwa ratiba ya NEC, alisema yeye ndiye anayepanga ratiba za mikutano na ikifika wakati atawajulisha wananchi.

Hata hivyo alisema hawezi kuzungumzia kwa undani ratiba ya vikao vya NEC kwa vile alikuwa msibani.

Ingawa suala la kutaka uchaguzi Zanzibar uahirishwe halikuwa sehemu ya ajenda ya kikao cha NEC, ni wazi kuwa lingeibuka na kuzua mjadala mzito kutokana na tofauti za mitizamo ya kisiasa.

Vikao hivyo ndivyo vitakavyojadili pia taarifa ya Kamati ya Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, iliyoundwa kuchunguza na kuutafutia tiba mgogoro kati ya wabunge wa CCM na serikali yao.

Kwa mujibu wa habari hizo, baadhi ya wajumbe wa NEC wameanza kufanya ushawishi miongoni mwao ili kuwa na msimamo wakati wa kuichambua ripoti ya kamati ya mzee Mwinyi.

Makundi hayo ni lile la wabunge wanaojiita wapiganaji wa vita dhidi ya ufisadi linaloongozwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Samuel Sitta na jingine ni majeruhi wa vita hiyo, akiwamo aliyepata kuwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete, Edward Lowassa.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima umebaini kuwa kila kundi linatembea kifua mbele likitamba kwamba haliwezi kuguswa na ripoti hiyo.

Ingawa taarifa ya kamati hiyo imebaki kuwa siri kubwa, baadhi yao wanasema huenda ikaja na mkakati wa kuwajibishana ndani ya CCM kutokana na sababu mbalimbali, zikiwamo za baadhi ya vigogo kuunda mitandao ya kisiasa, kuhusika na vitendo vya ufisadi na wengine kutoa matamko makali nje ya vikao vya chama hicho.

Mambo mawili makubwa yanatarajiwa kujitokeza ndani ya ripoti hiyo. Mosi, vigogo watuhumiwa wa ufisadi kuchukuliwa hatua za kinidhamu na kisheria.

Pili, wenye kutoa kauli kali nje ya vikao vya chama hicho, wakiwamo baadhi ya wabunge kupewa onyo na kutakiwa kuwa makini.

Tayari mkakati huo umeanza kupata upinzani miongoni mwa watu ndani ya CCM na hata baadhi ya wajumbe wa Sekretarieti, CC na NEC.

Kwa mujibu wa habari zilizotufikia, katika kikao cha sekretarieti hiyo, sehemu kubwa ya wajumbe wanaunga mkono chama kuwawajibisha watuhumiwa wenye kashfa za ufisadi, wakiwamo wanachama wake ambao wanaelekea kuwa mzigo baada ya kuchukuliwa hatua na vyombo vingine.

Lakini wakati hali ikiwa hivyo, inaelezwa kuwa vigogo wa juu serikalini wanaunga mkono uamuzi huo mgumu ili kumtenga Rais Kikwete na chuki zinazoweza kuibuka.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa hali ya kujadiliwa kwa watuhumiwa wa ufisadi wakitajwa kuwa na mikakati yao binafsi ambayo kwa kiasi kikubwa imekuwa ikikisumbua chama hicho, imewakera na kuwachosha viongozi wengi waadilifu serikalini.

Vyanzo vyetu vya habari vilivyo karibu na viongozi waandamizi nchini vimedokeza kuwa hatua hiyo inachukuliwa ili kuisafisha CCM mbele ya majukwaa ya kampeni baadaye mwaka huu.

Kamati ya Mwinyi inayowashirikisha Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa na mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Abdulrahman Kinana, iliundwa na NEC katika kikao chake kilichopita mjini Dodoma ili kutoa mapendekezo ya kumaliza kile kilichotajwa kuwa uhasama miongoni mwa wabunge wa chama hicho pamoja na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar waliowahi kupishana kauli na viongozi wa juu wa Serikali ya Muungano.

Mwishoni mwa mwaka jana, Kamati ya Mwinyi iliwahi kuripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa imeanza kuparaganyika, ikielezwa kuwa sehemu ya mapendekezo katika taarifa yake ya pamoja kwa ajili ya kuwasilishwa NEC-CCM imevuja.

Katika habari hizo ilielezwa kuwa baadhi ya viongozi wa CCM wamedokezwa kuhusu mapendekezo ya kamati hiyo, yaliyodaiwa kuwa ni pamoja na kuwangoa madarakani baadhi ya watuhumiwa.

Kutokana na mapendekezo hayo ya kungoana, baadhi ya vigogo wanatajwa kuwa na mwelekeo wa kupingana na kamati, kwa madai kuwa hiyo ni hatua kali, bila kujali kuwa wanaotakiwa kuachia madaraka ili wabaki wanachama wa kawaida walikwisha kufanya hivyo kwa kuacha nyadhifa zao serikalini.

Source: Tanzania Daima

My take,

Kunaviashiria CCM bara inapenda mgogoro wa CUF na CCM Zanzibar uendelee kuwepo sijui kwa faida ya nani.Nimekuwa nikijiuliza mara kadha ni kwanini maridhiano ya Maalim Seif na Dr Aman Karume yanawapa taabu sana baadhi ya watendaji wakuu wa CCM huku Tanzania bara.Mwanzoni nilidhani kulikuwa na juhudi hasa kutoka bara kuhakikisha mgogoro uliodumu kwa muda mrefu unamalizwa ili kuipa Tanzania taswira nzuri katika anga za kimataifa.

Nawashauri viongozi wote tuwe makini sana katika maamuzi yetu kwa faida ya vizazi vijavyo,Maalim Seif na Dr Aman Karume wahakikishe makubaliano yao hayakiuki katiba ya Zanzibar na ile ya JMT.
 
Hapa kinachoendelea bana ni kwamba Seif na Karume wameshaona Muungano uzushi, wanataka wavuruge hali ya hewa ili wachukue nchi yao...You will see things soon!

Nyie hamkuona hata kwenye sherehe za Mapinduzi jinsi Karume alivyoomba kwa JK mambo ya mafuta yaachwe kwa Wazanzibari?

Inaleta picha gani hii?

Kalagabaho.
 
Hapa kinachoendelea bana ni kwamba Seif na Karume wameshaona Muungano uzushi, wanataka wavuruge hali ya hewa ili wachukue nchi yao...You will see things soon!

Nyie hamkuona hata kwenye sherehe za Muungano jinsi Karume alivyoomba kwa JK mambo ya mafuta yaachwe kwa Wazanzibari?

Inaleta picha gani hii?

Kalagabaho.
kwa vyovyote tunaelekea huku.........!
jamaa wameona upumbav mtupu!lol
 
Hapa kinachoendelea bana ni kwamba Seif na Karume wameshaona Muungano uzushi, wanataka wavuruge hali ya hewa ili wachukue nchi yao...You will see things soon!

Nyie hamkuona hata kwenye sherehe za Muungano jinsi Karume alivyoomba kwa JK mambo ya mafuta yaachwe kwa Wazanzibari?

Inaleta picha gani hii?

Kalagabaho.

Heshima kwako PakaJimmy,

Tanzania ina dhahabu na gesi naomba kujuzwa Zanzibar inapewa share kiasi gani,msije mkadhani wazanzibar ni wajinga wakubaliane na mambo yasisiyo na maana.Ikiwa zanzibar wanapata mgao wa mapato ya dhahabu na gesi nitawashangaa kulazimishwa waachiwe mafuta yao ambayo hata hivyo bado hayajagunduliwa.

Zanzibar ni nchi ndogo ndani ya muungano pengine hatutaki kuwasikiliza kwasababu tu ya udogo wao.
 
Hapa kinachoendelea bana ni kwamba Seif na Karume wameshaona Muungano uzushi, wanataka wavuruge hali ya hewa ili wachukue nchi yao...You will see things soon!

Nyie hamkuona hata kwenye sherehe za Muungano jinsi Karume alivyoomba kwa JK mambo ya mafuta yaachwe kwa Wazanzibari?

Inaleta picha gani hii?

Kalagabaho.

Waachieni hako ka nchi kao, kwani tutapa hasara gani? By the way Muungano uliletwa na vita baridi ya Wamarekani na Warusi. Vita hiyo sasa imeshakwisha kwa hiyo wala hatuuhitaji tena huo Muungano.

Halafu kama ni rasimali, sisi tunazo nyingi zaidi kuliko wao! Tunawabeba sana lakini hawabebeki!
 
Waachieni hako ka nchi kao, kwani tutapa hasara gani? By the way Muungano uliletwa na vita baridi ya Wamarekani na Warusi. Vita hiyo sasa imeshakwisha kwa hiyo wala hatuuhitaji tena huo Muungano.

Halafu kama ni rasimali, sisi tunazo nyingi zaidi kuliko wao! Tunawabeba sana lakini hawabebeki!


Heshima kwako Masaki,

Ningepewa nafasi ya kuwa kiongozi wa wa Tanzania kitu cha kwanza kufanya ni kuvunja muungano wa Tanzania bara na Zanzibar mara moja.Mazingira ya sasa hakuna sababu ya kulazimisha muungano ambao kwa kiasi kikubwa Tanzania bara wameubeba mzigo mkubwa.
 
Huu muungano unakera.....watanganyika tunang'ang'ania nini? Tuwaache wenyewe wapelekane wanapotaka kwenda.
 
Ukiona ndugu wanataka kupatana halafu jirani presha ina panda na kushuka ujue ana jambo!
 
Ukiona ndugu wanataka kupatana halafu jirani presha ina panda na kushuka ujue ana jambo!
Lakini wenyewe wameshasema kule .Hivi sasa kipaumbele kwao ni Zanzibar , maslahi na mustakabala wake. Sasa mnawashangaa nini kukataa wito wa Dodoma wakati huu muhimu wa kukaa kwa Baraza lao la Wawakilishi?
 
Hapa kinachoendelea bana ni kwamba Seif na Karume wameshaona Muungano uzushi, wanataka wavuruge hali ya hewa ili wachukue nchi yao...You will see things soon!

Nyie hamkuona hata kwenye sherehe za Mapinduzi jinsi Karume alivyoomba kwa JK mambo ya mafuta yaachwe kwa Wazanzibari?

Inaleta picha gani hii?

Kalagabaho.

Naunga mkono kwa 100% muungano uvunjwe. Acha wazanzibar wajitegemee. Kila mara wanawekwa nyuma sana na wameshagundua hilo. Nashauri tuwaache peacefully kuliko waanze kuingia msituni kudai haki zao na International Moslem ikiiwaunga mkono tumekwisha.

Imagine hata ule mgawo wa samaki tuliwabemenda hadi ikabidi waziri wao atake kujua kulikoni na ikazimwa kimya kimya. Ni mbaya hii.

Karume na Maalim Seif, kaza uzi msirudi nyuma, chukueni nchi yenu kwa amani.
 
Hapa kuna ABCs kadhaa! Kama Wazenj wana mpango wa kuvuna Muungano halali sioni sababu kwa nini SMT isifuatilie! Njia za kuvunja Muungano zimeewekwa kwenye Katiba ya JMT. Vinginevyo utakuwa ni uhaini na unatakiwa ushughulikiwe ipasavyo!
 
katika vitu vitanipa raha ya milele maishani mwangu ni siku ambayo hili lidubwana muungano litakapovunjika....
 
Naunga mkono kwa 100% muungano uvunjwe. Acha wazanzibar wajitegemee. Kila mara wanawekwa nyuma sana na wameshagundua hilo. Nashauri tuwaache peacefully kuliko waanze kuingia msituni kudai haki zao na International Moslem ikiiwaunga mkono tumekwisha.

Imagine hata ule mgawo wa samaki tuliwabemenda hadi ikabidi waziri wao atake kujua kulikoni na ikazimwa kimya kimya. Ni mbaya hii.

Karume na Maalim Seif, kaza uzi msirudi nyuma, chukueni nchi yenu kwa amani.

Mkuu,

Hapo kwenye NYEKUNDU ndiyo kuna matatizo.

Nina wasiwasi kuwa mara wakijitenga, zitaanza kupigwa na ni sisi Tanganyika itabidi tuende kuviunga hivyo vipande vipande kama yaliyotokea huko kwa Wangazija.

Sijui wamekubaliana nini ila naona inaweza kuwa Unguja kwao na Pemba kwao. Tatizo haya makubaliano ni ya watu wawili tu na asilimia 70 wanakwenda kulingana na upepo.

Inabidi tuwape NUSU uhuru na wakiendelea vema basi baada ya miaka 5 tujitoe kabisaaa. Nina wasiwasi kuwa wakianza kupigana, ni sisi tutaenda kutuliza vita na hapo tutatowa hela nyingi.

Hili la kuongezeana muda, Karume alikuwa wapi miaka mingi? Nina wasiwasi kuwa jamaa atageuka kuwa Mbabe na akatae kuondoka. Watamfanya nini huko mbeleni na hasa ukichukulia kuwa jamaa atakuwa ndiye RAIS wa nchi?

Ohh, MIE PIA NI MPINZANI WA MUUNGANO ohhh!!!!!
 
Heshima kwako PakaJimmy,

Tanzania ina dhahabu na gesi naomba kujuzwa Zanzibar inapewa share kiasi gani,msije mkadhani wazanzibar ni wajinga wakubaliane na mambo yasisiyo na maana.Ikiwa zanzibar wanapata mgao wa mapato ya dhahabu na gesi nitawashangaa kulazimishwa waachiwe mafuta yao ambayo hata hivyo bado hayajagunduliwa.

Zanzibar ni nchi ndogo ndani ya muungano pengine hatutaki kuwasikiliza kwasababu tu ya udogo wao.

Zanzibar wanapata mgao wa dhahabu na gesi kwani mapato yote yatokanayo na gesi na dhahabu yanapelekwa hazina , na wao wanapata 4.5% ya mapato hayo!!! je haitoshi!!??? Kama haitoshi basi tujadiri jinsi gani na kiasi gani kinawatosha kulingana na uwingi wao.
 
This is an easy riddle. Viongozi wetu wengi wakishatumbukia madarakani wanatafuta kila mbinu wabakie milele. Karume ameongoza Zanzibar miaka zaidi ya 10 na amekataa kukubaliana na CUF. Umefika wakati wa kuondoka ameona mbinu sasa ni kuitumia CUF ili aendelee kuwepo madarakani. CUF wameununua huo mzoga lazima utawatafuna tuu. Hivi huyu Karume aliyegeuka ghafla na kuwa kipenzi cha CUF hadi wanataka kututoa macho kumtaka aendelee kuwa rais si yule yule ambaye amekuwepo madarakani toka Mwaka 2000 huku akiwaona CUF kama wazushi??

Salmini alitaka kubaki madarakani lakini mbinu yake ikatibuliwa! Sasa Karume ameona ujanja wa kubaki ni kuwatumia CUF kwani ndani ya CCM hakuna atakayekubaliana naye kwani timu iliyokuwa inaunga mkono kuendelea kwa Salmin bado ipo!

Hapa tusidanganyane oooh muafaka oooh wazanzibari sasa wanataka amani ...... tuangalie ukweli halisi. KARUME ANATAKA KUSALIA MADARAKANI NA AMEFANIKIWA KUINUNUA CUF. ALICHOAHIDIANA NA SEIF NI SIRI YAKE.

Lakini ukweli unabaki pale pale kwamba wanachama wa vyama vyao waliobaki wanawaona tu SEIF na KARUME. Lakini iko siku nia yao halisi itafanikiwa (hata kama ni kuvunja muungano na wavunje tuu). Ni wazanzibari wangapi wanajua kwa nini Karume na Seif walikuwa hawakubaliani miaka yote 10 iliyopita ila wamekubaliana Mwaka wa mwisho wa utawala wa Karume???? Tunapanda na kupalilia migogoro ili hatimaye tuje kuitumia kuendeleza kile tunachokipenda zaidi .... MADARAKA.
 
Sikonge umesema vema sana, haya mapatano ya watu wawili chumbani Ikulu mie naona hayana heri. Na bahati mbaya 70% fata upepo inaafiki kirahisi.

Kuna kila dalili ya kuwa CCM Zenj ilishatosheka na ubabaishaji wa huku Bara (Makamba & co) na sasa wanataka ku- team up with opposition kwa malengo maalum.

Hata hivyo uchangaji wa karata hizi mwisho wa yote kati ya CUF na CCM lazima mmoja ATALIA kwa rafu atakayochezewa, na ndio hapo yatakapotokea mambo mabaya ambayo hata kama muungano umevunjika lazima tugharamike kwenda huko kuweka mambo sawa kwa gharama yetu.
 
Hapa kinachoendelea bana ni kwamba Seif na Karume wameshaona Muungano uzushi, wanataka wavuruge hali ya hewa ili wachukue nchi yao...You will see things soon!

Nyie hamkuona hata kwenye sherehe za Mapinduzi jinsi Karume alivyoomba kwa JK mambo ya mafuta yaachwe kwa Wazanzibari?

Inaleta picha gani hii?

Kalagabaho.

Kama vile ulikuwepo hao watu wana lao jambo na nina amini Tanzania bara wamejaribu kuwatuma mashushu kuchunguza jambo linalo endelea huko, ni lazima tuu kuna mambo mambo yanaendelea, How can Seif akurupuke from no where na kusema hayo maneno ooooh aongezewe muda akihisi kuwa akiondoka karume lazima tu kunapandikizi chafu likiwekwa muafaka kushinehi faster
 
This is an easy riddle. Viongozi wetu wengi wakishatumbukia madarakani wanatafuta kila mbinu wabakie milele. Karume ameongoza Zanzibar miaka zaidi ya 10 na amekataa kukubaliana na CUF. Umefika wakati wa kuondoka ameona mbinu sasa ni kuitumia CUF ili aendelee kuwepo madarakani. CUF wameununua huo mzoga lazima utawatafuna tuu. Hivi huyu Karume aliyegeuka ghafla na kuwa kipenzi cha CUF hadi wanataka kututoa macho kumtaka aendelee kuwa rais si yule yule ambaye amekuwepo madarakani toka Mwaka 2000 huku akiwaona CUF kama wazushi??

Salmini alitaka kubaki madarakani lakini mbinu yake ikatibuliwa! Sasa Karume ameona ujanja wa kubaki ni kuwatumia CUF kwani ndani ya CCM hakuna atakayekubaliana naye kwani timu iliyokuwa inaunga mkono kuendelea kwa Salmin bado ipo!

Hapa tusidanganyane oooh muafaka oooh wazanzibari sasa wanataka amani ...... tuangalie ukweli halisi. KARUME ANATAKA KUSALIA MADARAKANI NA AMEFANIKIWA KUINUNUA CUF. ALICHOAHIDIANA NA SEIF NI SIRI YAKE.

Lakini ukweli unabaki pale pale kwamba wanachama wa vyama vyao waliobaki wanawaona tu SEIF na KARUME. Lakini iko siku nia yao halisi itafanikiwa (hata kama ni kuvunja muungano na wavunje tuu). Ni wazanzibari wangapi wanajua kwa nini Karume na Seif walikuwa hawakubaliani miaka yote 10 iliyopita ila wamekubaliana Mwaka wa mwisho wa utawala wa Karume???? Tunapanda na kupalilia migogoro ili hatimaye tuje kuitumia kuendeleza kile tunachokipenda zaidi .... MADARAKA.

Mkuu uliyokuwa nayo ni dhana tu hakuna uthibitisho wowote. Unajua ni mambo gani yalikuwa kikwazo huko mbele na kutekeleza mambo haya mwishoni mwa kipindi chake? Hakuna anaejua sababu. Lakini kitu ambacho kiko wazi CCM bara hawataki kuona CCM Zanzibar inaungana na CUF.

Ikiwa mkuu wa nchi JK alishatoa kauli kuwa mpasuko wa Zanzibar ataushughulikia mwenyewe kwa kuwa athari zake ni kubwa mno, Iweje yeye mwenyewe alipokwenda Pemba na kuwaambia mutake musitake mupende musipende mtatawaliwa na CCM milele!! Unapata picha gani hapo??

Ninachokiunga mkono kwa nguvu zote ni kupatikana amani ya kudumu visiwani ifike wakati mambo mengine CCM Zanzibar waamue mambo wenyewe mazingira ni tofauti sana na bara.

Muungano uendeleee kuwepo ila kuna baadhi ya mambo yanapaswa yabadilike kutokana na mazingira halisi yanayotuzunguka!!

Sijui ni sababu gani za msingi walizokuwa nazo CCM bara Kuona Zanazibar inaendelea kuwepo bila amani ya kudumu. Ninashindwa kuelewa kabisa!! Au kuna watu wanaona faraja wenzao wakiendelea kuishi kwa chuki na uhasama?

Kinachotafutwa na kilichoombwa na Maaalim Seif na CUF kwa ujumla ni uchaguzi usogezwe mbele kwa angalau mwaka mmoja na nusu na siyo kuwa Karume aongezewe kipindi cha tatu kwa nia tu maridhiano yapewe muda ili kujenga mazingira mazuri ya hali ya kisiasa na amani kwa kizazi kijacho. Sasa tatizo liko wapi??
 
Pamoja na wengi kuwa na wasiwasi kwa makubaliano haya lakini mimi bado naona kuna mwanga kwa mbele.

Tatizo kubwa la CUF na CCM kutofikia mwafaka ni CCM-bara kila wanapokaribia kuelewana CCM-bara walikuwa wanaingilia, tuliona mwafaka 2 ulivyozimwa kule Butiama.

Baada ya wazanzibar kuliona hilo wakasema tuanzishe mwafaka wetu bila kuwahusisha bara ndiyo maana ukawa siri, baada ya CCM-bara kupigwa chenga ya mwili ndiyo haya yote mnayaoyasikia ya kuvunja katiba utadhani wao huwa hawavunji katiba.

Hivi kuvunja katiba ni kuahirisha uchaguzi tu mbona hawasemi ZEC inavunja katiba kutowaandikisha wazanzibar wenye sifa ya kupiga kura? jamani tusiwe doublestandard kuona upande mmoja pekee.

Tuwaache jirani zetu na ndugu zetu wauguze vidonda vya uchaguzi bado havijapona wameona ni bora vipone kabisa badala ya kulazimisha uchaguzi mwingine utakaotonesha makovu yao tena.
 
Mkuu,

Hapo kwenye NYEKUNDU ndiyo kuna matatizo.

Nina wasiwasi kuwa mara wakijitenga, zitaanza kupigwa na ni sisi Tanganyika itabidi tuende kuviunga hivyo vipande vipande kama yaliyotokea huko kwa Wangazija.

Sijui wamekubaliana nini ila naona inaweza kuwa Unguja kwao na Pemba kwao. Tatizo haya makubaliano ni ya watu wawili tu na asilimia 70 wanakwenda kulingana na upepo.

Inabidi tuwape NUSU uhuru na wakiendelea vema basi baada ya miaka 5 tujitoe kabisaaa. Nina wasiwasi kuwa wakianza kupigana, ni sisi tutaenda kutuliza vita na hapo tutatowa hela nyingi.

Hili la kuongezeana muda, Karume alikuwa wapi miaka mingi? Nina wasiwasi kuwa jamaa atageuka kuwa Mbabe na akatae kuondoka. Watamfanya nini huko mbeleni na hasa ukichukulia kuwa jamaa atakuwa ndiye RAIS wa nchi?

Ohh, MIE PIA NI MPINZANI WA MUUNGANO ohhh!!!!!

Mkuu wangu hapo penye bold ndiyo penyewe. Majuzi wazee wa Pemba waloweka wazi kuwa wanataka wawe huru, wawe na nchi yao ya Pemba!! Ila kwa jinsi hali ilivyo kisiasa Zanzibar hata katika Baraza la Wawakilishi, Pemba na Unguja stands on its own. CCM haina nguvu Pemba hali kadhalika CUF haina nguvu Unguja. Kwa nini kulazimishana kama hawataki kuwa na serikali ya pamoja? Tumechoshwa na hawa Zanzibar, after all tunawagharimia sana mambo mengi, yaani wanafaidi sana resources za Muungano kuliko sisi wenyewe.

Sema wasiwasi wangu ni kuwa wakiwa nchi inayojitegemea kama Zenz au kama nazo zitajitenga wao kwa wao, usalama wetu Tanganyika utakuwa mdogo sana, nahisi watataka walipize kisasi!!! Sehemu kubwa ya wananchi wake wana hasira sana na Tanzania Bara. Wanaona tunawakatalia mambo mengi hasa suala la OIC na Kadhi!!! Achilia mbali mambo ya kichama ambayo sitataka kuyasema hapa.
 
Back
Top Bottom