Karibu: Chuo cha Maji Ubungo, Dar es Salaam

Slim5

JF-Expert Member
Jan 7, 2014
28,108
37,644

Water Development and Management Institute (WDMI) ama chuo cha usimamizi na maendeleo ya Maji, zamani Water Resources Institute (WRI) kilianzishwa mwaka 1974 kama kitengo ndani iliyokuwa wizara ya maji na nishati mnamo mwaka 1974.

Lengo kuu la uanzishwaji wa chuo hiki ilikuwa kukidhi mahitaji ya wataalamu wa maji wa ngazi ya kati katika uliokuwa mpango mkubwa wa miaka 20 wa program ya usambazaji maji nchini Tanzania kati ya (1971-1991).

Ilipofika mwaka 1980, chuo kilibadilisha jina na kuitwa Taasisi ya Rasilimali za Maji ya Rwegarulila ama Rwegarulila Water resources Institute. Chuo kimelenga katika kuandaa wataalamu mbali mbali wa sekta ya maji kupitia program zake za mafunzo, ushauri na tafiti chini ya sera husika ya wizara ya Maji, kwa sasa chuo kinatambulika rasmi kama Chuo cha Usimamizi na Maendeleo ya Maji, Water Development and Management Institute.

Chuo kinatambuliwa na TCU, kwa sasa chuo kinatoa kozi moja tu ya ngazi ya degree, ambayo wanafunzi wake, wanapata mkopo kutoka HESLB.

Bachelor degree in Water Resources and Irrigation engineering

Chuo ni cha Serikali, chini ya Wizara ya Maji, kozi zote za diploma zinazotolewa na chuo hiki, zinatambuliwa kwa usajili wa NACTE.

1. Diploma in Irrigation engineering
2. Diploma in Meteorology and hydrology
3. Diploma in Hydrology and water well drilling
4. Diploma in water supply and sanitation engineering
5. Diploma in water quality laboratory

Chuo kinatoa kozi mbali mbali za ngazi ya cheti. Chuo kwa kushirikiana na serikali, wanaandaa mkakati ili wanaomaliza masomo yao katika chuo hiki, waajiriwe moja kwa moja na serikali kupitia wizara ya Maji.

Chuo kina scholarship/sponsorship kwa watanzania katika ngazi ya diploma, kupitia WATER TECHNICIAN FUND, ofisi zao zipo ndani ya chuo cha Maji Ubungo.

Chuo kipo Dar es salaam, eneo la Ubungo, kutoka barabara ya Sam Nujuma kuelekea barabara ya chuo kikuu, inayopitia geti Maji.

Karibu Chuo cha Maji Ubungo, Dar es salaam.

 
Karbuni me mwaka wa pili diploma water supply and sanitation eng.
 
Nilikua na ndoto za kuingia pale coet but nimeishia getini. Irrigation eng. n water resources management pale chuo cha maji. Afu nacho si wangekifanya kua college mojawapo ya udsm wanatutamanisha kweli.
 
Nilikua na ndoto za kuingia pale coet but nimeishia getini. Irrigation eng. n water resources management pale chuo cha maji. Afu nacho si wangekifanya kua college mojawapo ya udsm wanatutamanisha kweli.
hawawezi fanya hivyo coz kiko chini ya wizara i think .by the way tupo pamoja. Mazingira yakoje ?
 
Nilikua na ndoto za kuingia pale coet but nimeishia getini. Irrigation eng. n water resources management pale chuo cha maji. Afu nacho si wangekifanya kua college mojawapo ya udsm wanatutamanisha kweli.
met vp kuhusu ada zao na tarehe ya kufungua? Coz website yao iko kimya. Na je mkopo tutapata ktk hii course?
 
Duh,kuna mwenye tetes zozote kuhusu kufungua chuo kwa wale wa Degree? Maana kimya kizito ktk web yao.
 
Pole sana kwa kuchaguliwa kusoma kwenye taasisi na sio chuokikuu
dogo nakuheshimu 7bu someone hinted that you attended TBR school. Ningekutoa shoo. Nimesoma pale miaka 6 usiangushe shule ile.haijawah kutoa kituko.nimefuata aina ya kozi cjafuata jina la chuo. Nataka nikimaliza niitwe engineer. Ww utaitwa nani? Nimeangalia future ya irrigation naona ipo na ni eneo ambalo ntatoe mchango wangu vzuri ktk ujenzi wa taifa langu ipo damuni. Naheshimu machaguo ya wengine ukiwemo ww mdogo wngu. By the way mi ni kakako mkubwa sn .
 
Pole sana kwa kuchaguliwa kusoma kwenye taasisi na sio chuokikuu
dogo nakuheshimu 7bu someone hinted that you attended TBR school. Ningekutoa shoo. Nimesoma pale miaka 6 usiangushe shule ile.haijawah kutoa kituko.nimefuata aina ya kozi cjafuata jina la chuo. Nataka nikimaliza niitwe engineer. Ww utaitwa nani? Nimeangalia future ya irrigation naona ipo na ni eneo ambalo ntatoe mchango wangu vzuri ktk ujenzi wa taifa langu ipo damuni. Naheshimu machaguo ya wengine ukiwemo ww mdogo wngu. By the way mi ni kakako mkubwa sn .
Salimia muccobs.
 
Back
Top Bottom