Elections 2010 Karagwe: Matokeo kutangazwa?

Saaaafi wanakaragwe! Bukoba mjini ndo wame to-let down! Labda nken'ge watathibitisha usomi wao na si wa kufodge udoctor kama mbunge wao aliyepita kamara!
 
Chadema kamnyoa ccm bila huruma karagwe ni deusdedit wa chadema tuuuuu

mimi nakuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuufa nipe rubisi

UKITAKA KUAMINI AMINI KAMA HUTAKI ACHA ILA HUTAZUIA sherehe maana ZINAENDELEA

SOURCE: WADOGO ZANGU WAPO ENEO LA TUKIO KAYANGA KARAGWE NA SHEREHE INAENDELEA

Sina shaka na huu ushindi ingawaje Chadema imedhulumiwa viti na mafisadi wa CCM..............
 
Tusubiri, if Deus wins, he will be another John Mnyika. A new star in the making. Vipaji kama hivi vitawaangamiza CCM for good!
 
Kuna utata kule karagwe kiasi kwamba wamepelekwa askari wa FFU toka Bukoba kule na sasa hivi nasikia wanapiga mabomu ya machozi wakitawanya watu waliokusanyika kudai haki zao pale Kayanga. Matokeo bado!
 
Karagwe wananchi wanapigwa mabomu kwa kuzunguka ofisi za Halmashauri wakihofia kuwa wanataka kutangazwa mbunge wa CCM anayemaliza muda, Blandes
 
Wana Jamvi

Niko jimboni Karagwe kama mwangalizi wa Uchaguzi (TEMCO).
Hivi sasa kikosi cha FFU kutoka Bukoba kimeingia na kuanza kurusha mabomu ya machozi mengi.
Kuna watu wapatao kama elfu kumi wamezingira ofisi ya tume wakidai itangaze matokeo ya ubunge.
Mabomu yameisha na sasa polisi wanatumia risasi za moto hewani. Watu wameumizwa na wengine wanakimbizwa hopsitalini.

Kuna tetesi kuwa Mgombea wa Chadema DEUSDEDITH JOVIN KAHANGWA amemshinda BLANDES GOSBERT wa CCM, lakini wakubwa wanakataa asitangazwe, bali Blandes ndiye atangazwe. Msimamizi wa Uchaguzi amejitahidi kukataa pressure kutoka kwa wakubwa lakini yaelekea sasa ananyonya mikono ili atangaze ushindi bandia kwa CCM. Hapahitajiki mabomu kumtangaza mgombea Chadema hapa maana maelefu ya watu wamekodi mafuso kuja kumlaki mbunge wao waliyemchagua.
 
Peoples Powerrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr!
Wakomae hapohapo, mabomu yataisha, lakini haki yao ni lazimaipatikane...
This is not nineteen kweusi bana!
 
Wana Jamvi

Niko jimboni Karagwe kama mwangalizi wa Uchaguzi (TEMCO).
Hivi sasa kikosi cha FFU kutoka Bukoba kimeingia na kuanza kurusha mabomu ya machozi mengi.
Kuna watu wapatao kama elfu kumi wamezingira ofisi ya tume wakidai itangaze matokeo ya ubunge.
Mabomu yameisha na sasa polisi wanatumia risasi za moto hewani. Watu wameumizwa na wengine wanakimbizwa hopsitalini.

Kuna tetesi kuwa Mgombea wa Chadema DEUSDEDITH JOVIN KAHANGWA amemshinda BLANDES GOSBERT wa CCM, lakini wakubwa wanakataa asitangazwe, bali Blandes ndiye atangazwe. Msimamizi wa Uchaguzi amejitahidi kukataa pressure kutoka kwa wakubwa lakini yaelekea sasa ananyonya mikono ili atangaze ushindi bandia kwa CCM. Hapahitajiki mabomu kumtangaza mgombea Chadema hapa maana maelefu ya watu wamekodi mafuso kuja kumlaki mbunge wao waliyemchagua.

Ee Mungu uliyeumba dunia, wakumbuke watu hawa kama wa Ubungo Dar es Salaam.

Wauwaji na waumizaji watu wenye haki washindwe kwa jina la Yesu!
 
hii hatari hawa jamaa kwanini wasiwe waungwana wakubali kuwa watu wamechoka nao....haya ni manyunyu mvua inakuja.....:nono:
 
tuko pamoja sana majirani zetu na ndugu zetu pande za izo
mwanza tuliweza,dar imewezekana na hapo itafikiwa tu hatma
msife moyo,mkiwaachia tu mwanya wamebeba matokeo!!
 
Hii habari ni kweli nimemaliza kuongea na Karagwe kwenye simu sasa hivi. Ninawaomba Wananchi wa Karagwe komaeni. Hakikisha tume inamtangaza mshidi halali. Kama Deus au Balndes. Msikubali kunyang'anywa haki yenu. Polisi hawataweza kuua Maana Kikwete katika moja ya Ahadi zake nyingi aliahidi kuwa damu haitamwagika baada ya uchaguzi. Komaa kama ilivyokuwa Dar, Arusha na Mwanza. Msifanye yaliyofanyika Shinyanga.

MUNGU AWE NANYI.
 
Huu ujinga wa dola utasababisha ghasia nchi hii. Kwa nini wanataka kubaka haki za wananchi?
 
Afu hawa polisi ni wapuuzi kweli,hawana akili hata kidogo...badala wamuache mpiganaji apite ili aje awasaidie coz wana shida kibao!
Look at their houses...
 
Back
Top Bottom