Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imetupilia mbali pingamizi alilowekewa mgombea ubunge wa jimbo la Karagwe kupitia Chadema, Deusdedith Kahangwa.
Kwa mujibu wa barua ambayo gazeti hili limeona kivuli chake, mrufani, amerejeshwa rasmi kuwa mgombea halali wa ubunge katika jimbo hilo.
Awali Kahangwa aliwekewa pingamizi hilo na CCM na NCCR Mageuzi ambavyo vilidai kuwa mgombea huyo hakudhaminiwa na chama chake na kuwa alijaza majina yake katika sehemu iliyotakiwa kujazwa na Katibu wa chama hicho.
Madai mengine katika pingamizi hilo ni kutodhaminiwa na wanachama, ambayo yamepuuzwa na Nec kuwa hayana msingi.
Kama wanachama walirubuniwa kumdhamini, basi walipaswa kupeleka malalamiko yao kwa Msimamizi wa Uchaguzi kabla ya pingamizi kupelekwa kwa msimamizi huyo, ilieleza barua hiyo ya Nec.
Kuhusu madai kwamba mgombea hakudhaminiwa na wapiga kura, Nec imesema kuwa fomu zinaonesha kuwa Kahangwa amedhaminiwa na wapiga kura 31 na msimamizi wa uchaguzi alithibitisha hivyo.
Kushinda rufaa kwa Kahangwa jimboni humo, kunatazamiwa kuleta chachu ya ushindani wa kisiasa kwani Chadema inaonekana kuwa na nguvu zaidi ya vyama vingine vya upinzani jimboni humo.
Kwa mujibu wa barua ambayo gazeti hili limeona kivuli chake, mrufani, amerejeshwa rasmi kuwa mgombea halali wa ubunge katika jimbo hilo.
Awali Kahangwa aliwekewa pingamizi hilo na CCM na NCCR Mageuzi ambavyo vilidai kuwa mgombea huyo hakudhaminiwa na chama chake na kuwa alijaza majina yake katika sehemu iliyotakiwa kujazwa na Katibu wa chama hicho.
Madai mengine katika pingamizi hilo ni kutodhaminiwa na wanachama, ambayo yamepuuzwa na Nec kuwa hayana msingi.
Kama wanachama walirubuniwa kumdhamini, basi walipaswa kupeleka malalamiko yao kwa Msimamizi wa Uchaguzi kabla ya pingamizi kupelekwa kwa msimamizi huyo, ilieleza barua hiyo ya Nec.
Kuhusu madai kwamba mgombea hakudhaminiwa na wapiga kura, Nec imesema kuwa fomu zinaonesha kuwa Kahangwa amedhaminiwa na wapiga kura 31 na msimamizi wa uchaguzi alithibitisha hivyo.
Kushinda rufaa kwa Kahangwa jimboni humo, kunatazamiwa kuleta chachu ya ushindani wa kisiasa kwani Chadema inaonekana kuwa na nguvu zaidi ya vyama vingine vya upinzani jimboni humo.