MotoYaMbongo
JF-Expert Member
- Jan 7, 2008
- 2,146
- 884
Mgombea ubunge wa Urambo Magharibi kupitia CCM Prof. Juma Kapuya ana hali ngumu sana katika jimbo la Kaliua, hali ambayo imemlazim kutegemea vyombo vya dola kudhibiti wapinzani. Hakika wananchi hawamtaki kabisa kutokana na tabia ya wafuasi wake kuwapiga wananchi wanapouliza maswali magum kwenye mikutano yake ya kampeni, kwa madai kuwa wananchi hao eti wametumwa. Wiki jana imetokea fujo kubwa sana Kaliua baada ya kijana mmoja kuuliza swali gumu, ambapo Kapuya aliposhindwa kujibu alimtukana "******" ndipo wananchi wakachachamaa na kuanzisha fujo kubwa, polisi wa kaliua wakapiga risasi zaidi ya 10 hewani lakini wapi, ikabidi waombe msaada Polisi Urambo, nao wakaenda wakapiga mabomu na risasi zaidi ya 30 kutisha watu, wananchi wakatawanyika, ikawa sasa mtu yeyote anayeonekana amevaa nguo za CCM ni kichapo tu, hali iliyopelekea watu kutembea vifua wazi kwa usalama wakati wanaelekea makwao, Jana yamepita magari ya Jeshi(JWTZ) yanaenda Kaliua, hali ya hatari imetangazwa hapa kaliua, mwisho wa kutembea ni saa mbili usiku, ukikamatwa unawekwa ndani, Kapuya anatumia ubabe sana, HATAKIWI, anaetakiwa ni mgombea wa CUF Anayeitwa KIRUNGI. hivi jamani hii ni HAKI?