Quemu
JF-Expert Member
- Jun 27, 2007
- 984
- 128
Abiria wako kwenye ndege ambayo imetekwa nyara na wahudumu (Flight Attendants) wa ndege hiyo. Wahudumu hao wakishirikiana na kapteni (au pengine wamemrubuni kapteni) wamefanikiwa kuiteka ndege hiyo na kuipeleka siko ndiko.
Abiria wanahangaika kutafuta njia ya kujikomboa. Wanawasihi watekaji nyara either wawafikishe salama wanakokwenda au watue chini kwa dharura ili abiria wapate kutafuta kapteni na wahudumu wengine ambao watafaa kuwapeleka wanakotaka kwenda.
Ombi la abiria linaleta mkanganyiko. Mgongano baina ya watekaji nyara (wahudumu na kapteni) unaanza kuleta mgawanyiko kati yao. Zoezi la utakaji nyara linaelekea (au linaonekana kuelekea) njia panda.
Abiria wanazidi kuweka msukumo wa kutaka waachiwe huru….
Kapteni, kwa siri, anapeleka ujumbe kwa abiria. Ujumbe huwa unasema hivi:
"Ndugu abiria, kwanza napenda kuomba msahama kwa adha yote hii mliyoipata toka muda tuliopaa angani. Kwa kweli ninajisikia vibaya sana kuona kwamba, mimi kama kapteni wenu, nimeshindwa kuiongoza hii ndege katika hali inayotakiwa. Badala yake nimeshirikiana na nimeendekeza tamaa za timu yangu ya wahudumu kuiyumbisha safari yenu. Sahamanini kwa hilo."
Kisha ujumbe unaendelea:
"Niko tayari kujirudi. Niko tayari kutumia nguvu zangu za ukapteni na kuiokoa ndege hii. Kwa baraka, rukhsa, na ushirikiano wenu; ningeomba nianze kuwapa adhabu wahudumu wangu hawa ili niweze kuifikisha safari yenu kunakotakiwa."
Ujumbe huo unaendelea tena:
"Nina ombi mmoja kubwa kwenu. Kutokana na mimi mwenyewe kuwa sehemu ya utekaji nyara huu, nina wasiwasi kuwa mfikapo mwishoni mwa safari yenu, mnaweza kuniadhibu na mimi pia. Kwa hiyo, ili niweze kutekeleza uokoaji wa ndege hii kwa usanifu mkubwa, ningeomba mniondolee wasiwasi wa kuniadhibu."
Je watanzania tunaweza kumsamehe JK pindi akiomba ‘immunity' ili aweze kuwashughulikia mafisadi? Je tuko tayari kumlinda kama akiwageuka marafiki zake ambao wanatumia urafiki huo kum-control na kutumia resources zetu kwa manufaa yao binafsi?
Tuko Tayari?
Abiria wanahangaika kutafuta njia ya kujikomboa. Wanawasihi watekaji nyara either wawafikishe salama wanakokwenda au watue chini kwa dharura ili abiria wapate kutafuta kapteni na wahudumu wengine ambao watafaa kuwapeleka wanakotaka kwenda.
Ombi la abiria linaleta mkanganyiko. Mgongano baina ya watekaji nyara (wahudumu na kapteni) unaanza kuleta mgawanyiko kati yao. Zoezi la utakaji nyara linaelekea (au linaonekana kuelekea) njia panda.
Abiria wanazidi kuweka msukumo wa kutaka waachiwe huru….
Kapteni, kwa siri, anapeleka ujumbe kwa abiria. Ujumbe huwa unasema hivi:
"Ndugu abiria, kwanza napenda kuomba msahama kwa adha yote hii mliyoipata toka muda tuliopaa angani. Kwa kweli ninajisikia vibaya sana kuona kwamba, mimi kama kapteni wenu, nimeshindwa kuiongoza hii ndege katika hali inayotakiwa. Badala yake nimeshirikiana na nimeendekeza tamaa za timu yangu ya wahudumu kuiyumbisha safari yenu. Sahamanini kwa hilo."
Kisha ujumbe unaendelea:
"Niko tayari kujirudi. Niko tayari kutumia nguvu zangu za ukapteni na kuiokoa ndege hii. Kwa baraka, rukhsa, na ushirikiano wenu; ningeomba nianze kuwapa adhabu wahudumu wangu hawa ili niweze kuifikisha safari yenu kunakotakiwa."
Ujumbe huo unaendelea tena:
"Nina ombi mmoja kubwa kwenu. Kutokana na mimi mwenyewe kuwa sehemu ya utekaji nyara huu, nina wasiwasi kuwa mfikapo mwishoni mwa safari yenu, mnaweza kuniadhibu na mimi pia. Kwa hiyo, ili niweze kutekeleza uokoaji wa ndege hii kwa usanifu mkubwa, ningeomba mniondolee wasiwasi wa kuniadhibu."
Je watanzania tunaweza kumsamehe JK pindi akiomba ‘immunity' ili aweze kuwashughulikia mafisadi? Je tuko tayari kumlinda kama akiwageuka marafiki zake ambao wanatumia urafiki huo kum-control na kutumia resources zetu kwa manufaa yao binafsi?
Tuko Tayari?