Kanye West aomba pesa kutoka kwa Zuckerberg

Primier

Member
Dec 16, 2015
86
14
151011084601_kanye_west_624x415_reuters.jpg
Image copyright Reuters
Image caption Kanye West alisema majuzi kwamba anadaiwa $53m
Mwanamuziki Kanye West amemuomba hadharani mwaanzilishi wa Facebook Mark Zuckerberg ampe usaidizi wa kifedha.


West anataka Zuckerberg awekeze $1bn (£700m) katika miradi yake akisema yeye binafsi hana “rasilimali za kutosha” kuunda kile ambacho “anaweza”.

160215150343_kanyewestzuckerbergtweet.jpg

Ametoa ombi hilo siku chache tu baada ya kutangaza kwamba ana deni la $53m (£36m) alipokuwa akitoa albamu yake mpya.


West alijitetea kupitia msururu wa jumbe kwenye Twitter.

Waandishi wa BBC Newsbeat wamewasiliana na maafisa wa Facebook ambao wamesema: “Hatuna lolote la kusema kwa sasa.”

Jambo la kushangaza ni kwamba Kanye West amemuomba Zuckerberg usaidizi kupitia Twitter ambao ni mtandao unaoshindana na Facebook.
 
Back
Top Bottom