Kanuni zavunjwa tena Arusha...hii ndiyo bongoland.

Kama ni kweli, kilichofanywa na hawa madiwani wa CDM ni uhuni. Huwezi kujiorodhesha kwenye mahudhurio baadaye ukataka kufuta jina lako. Bila shaka barua za kuwaalika ziliwajulisha wanakwenda kufanya nini. Wanapaswa kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwani wanatoa picha mbaya kwa chama ambacho watu tumeanza kukiamini.
 
..bado sijaridhishwa na utaratibu wa kupitisha bajeti bila majadiliano wala kura.

..haileti mantiki uamuzi wa msingi kama bajeti ya jiji linaloheshimika kama Arusha eti inapitishwa kwa kusaini kitabu cha mahudhurio.
 
Ukisusa wenzio wala siungi mkono ususiaji wa madiwani wa CHADEMA katika masuala muhimu nadhani dhani nzima ya ususiaji inakosa maana kabisa.Bejeti itagusa maeneo nyeti kama Hospital,elimu,ujenzi wa barabara na nk ukisusa maana yake shughuli zote hizo zisimamishwe kisa unataka nafasi ya umeya.

CHADEMA wananchi wanajua hila na ghiliba za uchaguzi wa Meya wa jiji la Arusha kususia sidhani kama ni jambo muhimu kwa wakati huu.Zipo mahakama kwanini hamataki kwenda huko.Shughuli za maendeleo lazima zienziwe na madiwani wote wa CHADEMA na CCM na vyama vingine vyote,Tanzania ni kubwa kuliko vyama vyenu.

KUDOS!!!!
Na soon wananchi watawachoka, mnashupalia umeya kama nini vile???!!!!
 
Hahaahahaha hii nayo imekaa kiaina yani madiwani wa chadema wangejua wasinge jiandikisha hapo inge kua safi! Sasa walijua wasipo jiandikisha hawata chukua posho kumbe wenzao wanataka waweke column! Mumuliwa Chadema kila siku CCM wana wapiga bonge la mchakachuo! Tatizo wenzenu CCM wanatumia brain nyie manguvu tu na slogan ya mpaka kieleweke na Mbunge Lema nae kazidi kutumia nguvu badala ya Akili!
 
Think tank ya CDM iko bogus!....hao CCM waandae mnuso tu,mtaona CDM wakishake hands na meya kama mwenyekiti wao alivyofanya kwa JK,what a bunch of loonies!
 
Think tank ya CDM iko bogus!....hao CCM waandae mnuso tu,mtaona CDM wakishake hands na meya kama mwenyekiti wao alivyofanya kwa JK,what a bunch of loonies!
whether they shake hands or legs,but it remains clear that there still a big comflict here.It has to be solved to make things smooth.bila hivyo wananchi wa arusha hatutakuwa na amani.wengi tunahisi kuna siku vurugu zitaibukaa tena.
 
Comments nyingine huku zinatia kinyaa! Kwa hiyo Chadema wakae na kukubali mwizi au vipi? Yani wapinge alafu wakibanwa kidogo waachie? Mbona mnakuwa hamna misimamo nyie?
 
Tuache ushabiki madiwani wa CDM wawe na uchungu kwa maendeleo ya wananchi, wataendelea kususia vikao vya madiwani mpaka lini??
Je ccm wataendelea kupotosha haki za wananchi mpaka lini? bajeti isiwe sababu ya kuwahalalishia hawa manyang'au udhalimu wao!!!!!!
Rubish!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Waliingia kuonesha dhamili zao za kuwatumikia wana wa arusha. Walitoka mara baada ya anayeitwa meya kusimama kuonesha hawamtambui kama meya halali wa arusha. Mmeelewa???
Nakuunga mkono ndugu ni wajinga tu ndo hawaelewi, kwani ikiwa ccm wanauchungu na maendeleo ya wanaArusha wangeheshimu maamuazi yao ya kutaka uchaguzi wa meya urudiwe!!!! hapo hadangajiki mtu.
 
Mnachoshindwa kuelewa ni kuwa watu hawajali sana hizo politics zenu,nendeni mahakamani kama mmeonewa,la sivyo kubalini mmeshindwa na siku 21 zimeshapita.Tuondoleeni siasa mbuzi hapa!
 
kwa hapo nami siungani nao hao madiwani wa cdm. ni uhuni sasa. i dont see kwa nini basi waliingia ndani na kuandikisha majina yao, ni dhahiri hawajui taratibu, hata unapokuja kukata majina sijui ndo kufanya nn sasa. hao jamaa hakika wanapotosha dhana nzima ya kuwa mpinzani.

Upinzani, miaka yote CCM hawakua na upinzani hivyo hawaelewi!

Ili kupinga kwanza unaleta hoja yako ambayo una uhakika ina tija kwa watu. Unailezea kiundani na kisayansi lakini madiwani wa CCM wanapinga ili mradi wewe si CCM. Sasa inafika mahala hata kupiga masumbwi inakuwa sehemu ya upinzani, lazima kuwaamsha kwa masumbwi wakati mwingine la sivyo Arusha itabakia ile ile ya 54.
 
chadema huo siyo uongozi...kwa nini mlifika mkajiorodhesha..then mnatoka wakati mnajua kitendo cha nyie kufika na kujiorodhesha..mnakamilisha idadi inayotakiwa..!why!?..kwanini mnawapa watu sababu..?????????????? tafakari.!
 
Thats good na huo ndio msimamo wa kweli kabisa, nimependa hatua ya kutoka nje aliposimama kuadi Gaudence Lyimo na kudhibitisha hoja yao kuwa shida ni Meya na sio halmashauri
 
[FONT=Helvetica, sans-serif]Baraza la Madiwani Jiji la Arusha limepitisha bajeti ya zaidi ya Sh. bilioni 48.1 kwa mwaka huu wa fedha wa 2011/ 2012, licha ya madiwani 11 wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema ) kususia kikao hicho kilichofanyika jana kwa kutoka ukumbini. [/FONT]

[FONT=Helvetica, sans-serif]Baraza hilo likiwa na wajumbe 16 kutoka vyama vya CCM na TLP, lililazimika kuendelea na kikao na kupitisha bajeti hiyo, huku baadhi ya wajumbe wa baraza hilo kutoka vyama hivyo viwili wakishutumu hatua ya madiwani wa Chadema kususia kikao hicho.[/FONT]

[FONT=Helvetica, sans-serif]Awali, baada ya wajumbe wote kuingia katika ukumbi, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Estomiah Chang’a, alitoa taarifa ya idadi ya madiwani waliokuwa ukumbini wakiwemo wa Chadema, CCM na TLP kuwa ni 25.[/FONT]

[FONT=Helvetica, sans-serif]Alisema idadi hiyo ni zaidi ya akidi ya theluthi mbili ya wajumbe wote 32 wanaotakiwa kuhudhuria kikao hicho. [/FONT]

[FONT=Helvetica, sans-serif]Lakini wakati Meya wa Jiji la Arusha, Mstahiki Gaudence Lyimo, aliposimama kwa ajili ya kufungua kikao hicho, madiwani wa Chadema wakiongozwa na John Bayo wa kata ya Elerai walinyanyuka vitini na kutoka nje ya ukumbi.[/FONT]

[FONT=Helvetica, sans-serif]Hata hivyo, Chang’a, alisema kanuni na taratibu zinaelekeza kwamba iwapo mjumbe yeyote wa kuchaguliwa atapata wito na akaitikia na kufika ukumbini ni dhahiri mjumbe huyo atakuwa amehudhuria kikao hicho na hivyo kuchangia kufikia idadi ya wajumbe wanaotakiwa kufikisha akidi ya kikao ya theluthi mbili hata kama atakuwa ameondoka ukumbini. [/FONT]

[FONT=Helvetica, sans-serif]Mbali na wadiwani wa Chadema kuingia ukumbini na kujiorodhesha katika kitabu cha mahudhurio, Bayo, aliamua kuchukuwa rejesta ya majina na kukatakata majina yao.[/FONT]

[FONT=Helvetica, sans-serif]Akizungumza mara baada ya kupitishwa kwa bajeti hiyo, Diwani wa TLP kutoka kata ya Sokoni One, Maiko Kivuyo, alisema wamepitisha bajeti ya jiji kwa manufaa ya wananchi wa Arusha.[/FONT]

Viongozi wekeni mbele maslahi ya taifa kwanza kwa ajili ya ustawi wa jamii.
 
CCM mnafanya kazi nzuri sana ya kujibu hoja hapa jukwaani. Muda si mrefu mtaliteka jukwaa zima la JF. Jitahidini huenda mkafanikiwa!!!!
 
Nakuunga mkono ndugu ni wajinga tu ndo hawaelewi, kwani ikiwa ccm wanauchungu na maendeleo ya wanaArusha wangeheshimu maamuazi yao ya kutaka uchaguzi wa meya urudiwe!!!! hapo hadangajiki mtu.

Wao wangapi??? Ni kundi la majobless wachache tu ndio wanapiga kelele.
Mtu mwenye kazi yake dont care meya ni CCM au CDM, kwani mwisho wa siku hakulishii familia yako.
So stop generalizing, ingekuwa watu wa Arusha hatumtaki meya hasingekaa hata siku saba ktk ofisi hiyo.
 
Back
Top Bottom